![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEi-KqTU0BCunHdUEhB783IJ1LVHrDUlgLpE_G2aVMYE5F1hHH_24g5-RaOCl_uKjzQ672eOCl_qELjURQtzQ7irCAxtZ84Ua0ZwG-rWhNQ2oisouafN1LHieW0tv343KqBC48b_cPYs_YE/s280/Absence.jpg)
Kutokana na kupanga na kufuatilia masuala fulani ya mustakabali wa maisha, nategemea kuadimika kwa muda hapa. Haimaanishi kuwa sitakuwa naweka mabandiko, na si kwamba sitakuwepo kwa muda mrefu. Nitakuwa nikishughulikia mambo mengi na hivyo naweza kutokuwa na wakati wa kutosha kutazama mambo kwa "jicho la ndani" kuniwezesha kuyabandika hapa.
Najua ntapata nafasi ya kupitia "sebule" za wapendwa na pale niwezapo kuacha maoni yangu kwani hiyo ni SEHEMU YA RATIBA YA KILA SIKUKwa wakati huu wa u-adimiko langu, endelea kuwa salama, mwenye furaha na amani ndani na mazingirani mwako
UPENDO KWAKO
Ahsante kwa taarifa. Hivi ndivyo inavyotakia KUTOA TAARIFA:-) Kila la kheri
ReplyDeleteKila la heri kaka tupo pamoja.
ReplyDeleteTuombeane uzima.
ReplyDeletebyee
ReplyDeleteUpendo kwako pia Mkuu! Tuko pamoja!
ReplyDeleteAsante kwa taarifa.Inaeleweka kabisa kwamba kuna wakati mtu inabidi ukimbie kidogo kutoka bloguni ili kuweka sawa mambo mengine.Kila la kheri
ReplyDeleteNaamini kwamba unaadimika sasa ili uje upatikane huko mbele. Kwa hiyo yote ni sawa. Tutakusubiri!
ReplyDelete