Showing posts with label Huyu na Yule. Show all posts
Showing posts with label Huyu na Yule. Show all posts

Monday, May 7, 2018

Kipindi cha JUKWAA LANGU. Mei 7, 2018

Katika kipindi cha JUKWAA LANGU hii leo ndani ya Kilimanjaro Studios, wageni wetu studioni ni kutoka mashirika yasiyo ya kiserikali yanayoitumikia jamii ya wahitaji nchini Tanzania.
Katika saa la kwanza tutakuwa na uongozi wa SHINA INC ambao tangu mwaka 2002 wamekuwa wakisaidia jamii zenye uhitaji nchini Tanzania. Wana mengi ya kutushirikisha

Kwenye saa la pili tutakuwa na wakuu wa Help for Underserved Communities Inc. (HUC-USA) ambao wanajishughulisha kutoa textbooks mashuleni, VETA Scholarships na kusaidia matibabu ya macho nchini Tanzania.

Lakini tutaanza na mrejesho wa maadhimisho ya TANZANIA DAY 2018 yaliyofanyika Dallas Texas.

Ni kipindi cha JUKWAA LANGU, leo Jumatatu (Mei 7, 2018) na kila Jumatatu kuanzia saa 12 kamili jioni mpaka 2 kamili usiku kwa saa za Marekani Mashariki (6:00 - 8:00pm ET)
Ni kupitia Facebook live (Mubelwa Bandio na Kwanza Production) ama Kwanza Radio kwenye TuneIn
http://tun.in/sfwyf ama piga simu 202-683-4570
*******************************
PRODUCER: Mubelwa Bandio

Wednesday, June 28, 2017

Mahojiano ya Mubelwa Bandio na Shose Kombe kuhusu Diaspora

Karibu katika mahojiano kati ya Mubelwa Bandio na Mkuu wa Mawasiliano wa Diaspora kutoka KCB Bank Shose Kombe.
Mahojiano haya yalifanyika ndaninyabKilimanjaro Studio iliyopo Beltsville, Maryland nchini Marekani

Sunday, March 19, 2017

Mahojiano na Dj D - Ommy ndani ya Kilimanjaro Studios U.S.A


Machi 16 2017, Mubelwa Bandio na Viola walipata nafasi ya kufanya mazungumzo na Dj D-Ommy katika studio za Kilimanjaro Studios.
Dj D-Ommy ambaye alikuwa katika ziara ya kikazi nchini Marekani amezungumza mengi kuhusu maisha, kazi na tasnia nzima ya muziki.
Pia akapata fursa kuzindua rasmi kifaa kipya cha kazi kwa studio yetu, Pioneer DDJ SZ2
Karibu usikilize

Tuesday, April 5, 2016

[VIDEO] Mahojiano ya Mubelwa Bandio na mgombea uwakilishi nchini Marekani Will Jawando

Photo Credits: @wjawando
Mgombea uwakilishi katika Bunge la Marekani William Jawando alihojiwa na Mubelwa Bandio katika studio za Kilimanjaro zilizopo Beltsville, Maryland nchini Marekani. Mbali na mambo mengine, alizungumzia kuhusu mikakati yake katika kuisaidia diaspora ya Afrika katika eneo lake na Marekani kwa ujumla. Ikumbukwe kwamba 10% ya wazaliwa wa Afrika wanaoishi Marekani, wapo katika jiji la Washington DC
Karibu ufuatilie mahojiano haya

Monday, May 25, 2015

Ana kwa Ana na Nape Nnauye (Pt II)

Karibu katika sehemu hii ya pili na ya mwisho ya mahojiano yetu na Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye.
Kazungumzia mambo mbalimbali, hasa suala la uchaguzi
Karibu

Monday, May 18, 2015

Ana kwa Ana na Nape Nnauye Pt I

Karibu kwenye sehemu ya kwanza kati ya mbili za mahojiano yetu na Katibu Uenezi na Itikadi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Tanzania.
Ameeleza mengi akianza na Hali ya chama hivi sasa.
KARIBU

Sunday, May 10, 2015

Mahojiano na Mhe. Alhaj Ali Hassan Mwinyi kuhusu KISWAHILI

Kiswahili inaaminika kuwa lugha asili ya Afrika inayozungumzwa na watu wengi zaidi kusini mwa jangwa la Sahara.
Ni lugha ya taifa kwa nchi za Kenya na Tanzania na pia yazungumzwa kwenye nchi za Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, Burundi, Rwanda, Uganda, Visiwa vya Comoro na nchi nyingine
Ikizungumzwa na watu wanaokadiriwa kufikia milioni 100 hivi sasa, Kiswahili ndio lugha pekee ya kiAfrika iliyo miongoni mwa lugha rasmi za Umoja wa Afrika.
Ni lugha muhimu katika habari, shule, kazi za kiofisi, kidiplomasia na hata usalama miongoni mwa mataifa. Lakini , licha ya ukubwa wake, lugha hii inakabiliwa na changamoto mbalimbali.
Hivi karibuni, Chama cha Ukuzaji Kiswahili Duniani (CHAUKIDU) kilifanya mkutano wake wa nne, ambapo mgeni rasmi alikuwa Rais wa pili wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Ali Hassan Mwinyi. Na amekuwa mkarimu sana kujiunga nasi kuzungumzia juu ya lugha ya Kiswahili na changamoto zake.
KARIBU

Thursday, May 7, 2015

Miaka 90 ya Rais Ali Hassan Mwinyi

Leo, Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Ali Hassan Mwinyi anatimiza miaka 90.
Tulipata fursa ya pekee kuketi naye akatueleza mambo machache kuhusu maisha yake
UNGANA NASI

Sunday, April 26, 2015

Mahojiano na mbunifu mavazi Linda Bezuidenhout (LB) Pt II

Karibu katika sehemu ya pili na ya mwisho ya mahojiano na mbunifu wa kimataifa wa mitindo mwenye asili ya Tanzania, Linda Bezuidenhout
 Ameeleza mengi kuhusu kazi yake na familia kwa ujumla.
Anavyokabiliana na kazi zake, changamoto za afanyalo, tuzo alizopata nk
Na pia, kaeleza kuhusu mtazamo wake juu ya waTanzania (hasa wa Diaspora) na ushauri kwa kinamama wote
KARIBU

Sunday, April 19, 2015

Mahojiano na Linda Bezuidenhout (LB) Pt I

Karibu katika sehemu ya kwanza ya mahojiano na mbunifu wa kimataifa wa mitindo mwenye asili ya Tanzania, Linda Bezuidenhout.
Ameeleza mengi ikiwa ni pamoja na historia yake kwa ufupi, safari yake kwenda nje ya nchi, alivyorejea na kuanza harakati zake za mitindo
Nani alimfanya ashawishike na fani hii?
Maisha yake kimahusiano je?
Familia yake sasa na inavyokabiliana na kazi zake?
KARIBU

Katika kipindi cha "HUYU NA YULE" kesho (Jumatatu), usikose kujua UNDANI wa maisha ya Linda

NI MENGI AMEZUNGUMUZA AMBAYO MIMI NA WEWE HATUKUYAJUA
Kesho Jumatatu katika kipindi cha huyu na yule cha mahojiano na mwanamitindo mbunifu wa LB kutoka Atlanta, Georgia atakapoelezea historia yake yenye milima na mabonde historia ya maisha yake yenye huzuni na furaha wakati mwingine Linda akitokwa na machozi kwa kukumbuka maisha aliyopitia. Je Mume wake Mali walijuana nae wapi? na mengine mengi kuhusu maisha yake ikiwemo kampuni yake ya LB na malengo yake ya kupeperusha bendera ya Tanzania anga za kimataifa. USIKOSE mahojiano yaliyofanywa na mwakilishi wa Vijimambo na kwanza production Michigan Alpha Igogo ambae alitaka kujua undani wa maisha ya mwanadada Linda

Alpha Igogo akifanya mahojiano na Linda jijini Atlanta
Maswali yalikua moto Linda akipumua na kumkumbatia Alpha Igogo baada ya mahojiano kufikia mwisho

Sunday, March 8, 2015

Mazungumzo na Mhe Samuel Sitta......Wizara na Kugombea Urais

Karibu katika sehemu hii ya pili ya mazungumzo na Mhe. Samuel Sitta (Mb)
Aliyekuwa Mwenyekiti wa Bunge Maalum la Katiba ya Jamhuri ya Muungano waTanzania mwaka 2014.
Aliketi nasi kuzungumzia kuhusu kazi zake kama Waziri wa Uchukuzi na pia nia yake ya kugombea Urais katika uchaguzi mkuu wa mwaka huu (2015)
Karibu

Thursday, February 12, 2015

Mazungumzo na Mhe. Balozi Mustafa Nyang'anyi Pt II

Karibu sana na asante kwa kujiunga nasi katika kipindi hiki cha HUYU NA YULE
Tumepata fursa ya kuongea na Mhe. Balozi Mustafa Nyang'anyi
Tumefanya mazungumzo naye ya sehemu nne, kueleza safari yake kimaisha
Tunaendelea na sehemu ya pili ya mazungumzo yetu, ambapo Mhe Balozi Nyang'anyi anaanza kuelezea namna
1: Alivyoingia kwenye siasa (ubunge mwaka 1970)
2: Alivyopata taarifa za kwanza za uteuzi wake serikalini. Hapa napo pana mvuto wake kusikiliza.
3: Nafasi alizoshika kama naibu waziri na waziri kamili
4: Nafasi ya ukuu wa mkoa
5: Na hata harakati zake na pia alivyopata nafasi ya kuja kusoma Chuo Kikuu Havard
KARIBU
Kama ulikosa sehemu ya kwanza ya mazungumzo yetu, bonyeza READ MORE

Wednesday, February 4, 2015

Mazungumzo na Mhe. Balozi Mustafa Nyang'anyi (Pt 1)

Karibu sana na asante kwa kujiunga nasi katika kipindi hili cha HUYU NA YULE
Tumepata fursa ya kuongea na Mhe. Balozi Mustafa Nyang'anyi ambaye ametueleza mengi juu ya safari yake kimaisha
Katika sehemu hii ya kwanza, Mhe. Balozi Nyang'anyi anaelezea
1: Historia yake.
 2: Aliposoma na alivyosoma.
 3: Namna alivyofika / kupata kazi Shirika la Utangazaji Tanganyika (TBC)
 4: Alivyoingia kwenye masuala ya diplomasia na kisha.....alivyoiona nafasi ya ubunge kwa mara ya kwanza 1970. Hii ni safari ndeefu ambayo kwa hakika utapenda kuisikia.
 KARIBU

Thursday, January 22, 2015

[AUDIO]: Mahojiano na JhikoMan kuhusu wimbo wake mpya...Africa Arise

Karibu katika mahojiano kati ya Kwanza Production na Jhiko Manyika a.k.a JhikoMan aliyejiunga nasi moja kwa moja kutoka Bagamoyo Tanzania
Alizungumzia wimbo wake mpya wa Africa Arise, ambao amemshirikisha Peter Morgan wa kundi la Morgan Heritage.
Amezungumza mengi kuuhusu
Karibu usikilize hapa chini

Pia unaweza kurejea mahojiano kati yao wakati JhikoMan akiwa ziarani Ulaya mwaka 2014. Alizungumza mengi kuhusu muziki wa reggae Tanzania lakini pia aligusia "projects" mbalimbali ambazo ziko njiani kuja

Sunday, January 18, 2015

Huyu na Yule...........Mahojiano na Dr na Mama Williams

Karibu kwenye mahojiano ya Dr na Mama Williams.
Waasisi wa AHEAD Inc. Taasisi ambayo iliasisiwa mwaka 1985 na inajishughulisha kubadili maisha ya wengi nchini Tanzania kupitia Elimu, Stadi za Maisha, Afya ya Mama na Mtoto na pia kuzisaidia jamii mbalimbali..
Wamezungumzia mengi kuhusu namna walivyofika Tanzania kwa mara ya kwanza 1975. Kilichowapeleka, walivyoamua kubaki huko mpaka sasa, shughuli za Taasisi yao na mengine mengi
Karibu

Sunday, January 11, 2015

HUYU NA YULE......Mahojiano na Dr Talib Ali

Karibu katika kipindi cha HUYU NA YULE ambapo wiki hii tumeongea na Dk Talib Ali
Yeye ni mwanzilishi wa Avatar Dental Care iliyopo Leesburg Virginia.
Ameeleza mengi kuhusu kazi zake na mikakati aliyonayo baadae Pia, ametoa punguzo la 50% kwa waTanzania watakaoenda kutibiwa kwake, pamoja na mpango wa malipo ya awamu kuwezesha watu kumudu gharama hizo
Karibu

Thursday, January 8, 2015

Sunday, January 4, 2015

HUYU NA YULE.......Mahojiano na Dr Crispin Semakula

Karibu katika kipindi cha HUYU NA YULE ambapo wiki hii tumeongea na Dr Crispin Semakla.
Daktari wa mahgonjwa ya kisukari, shinikizo la damu na pia Mwalimu wa Afya katika Chuo Kikuu nchini Marekani
Pia ni mwanzilishi wa Access Medical and Dialysis Center iliyopo Dar Es Salaam
Ameeleza mengi kuhusu maradhi anayoshughulika nayo na pia kituo chake.

Huyu na Yule ni kipindi kinachotayarishwa na Vijimambo Blog na kuzalishwa na Kwanza Production
Kwa mawasiliano, maoni ama ushauri, tafadhali wasiliana nasi kupitia kwanzaproduction at gmail.com

Friday, October 24, 2014

Mahojiano ya Hashim Lundenga na Vijimambo / Kwanza Production

Mkurugenzi wa Lino Angency International Ltd Hashim Lundenga
Hivi karibuni kulifanyika mashindano ya kumsaka mrembo wa Tanzania kwa mwaka 2014 (Miss Tanzania 2014) ambapo Sitti Mtemvu alitangazwa kuwa mshindi.
Baada ya kutangazwa huko, kukawa na mambo mengi yaliyosemwa kumhusu. Kuanzia tetesi za kuwa kadanganya umri mpaka elimu. Kuwa kuna rushwa ilitumika mpaka kusemwa ana mtoto.
Mkurugenzi wa Lino Angency International Ltd Hashim Lundenga, anazungumza na mitandai ya Vijimambo na Kwanza Production kuweka bayana
KARIBU