Sunday, November 9, 2008

Buriani Mhe. RICHARD S. NYAULAWA Marehemu Mhe Richard Nyaulawa
Katika picha hii ya March 20 2008, Makamu wa Ris Dk Ali Mohamed Shein na Mama Mwanamwema Shein wakimfariji Mbunge wa Mbeya Vijijini Mheshimiwa Richard Nyaulawa ambaye alikuwa amelazwa katika Hospitali ya Indraprastha Apollo kwa matibabu ya Saratani (Cancer) ya utumbo wakati Dk Shein alipotembelea hospitalini hapo kuona huduma mbalimbali zinazotolewa na hospitali hiyo.

Nilipata bahati ya kumfahamu Mhe. Richard Nyaulawa kwa kufanya kazi katika kampuni ambayo alikuwa mmoja wa wakurugenzi wake ya Bussiness Times iliyo chini ya Bussiness Care Group of Comnpanies. Habari za kufariki kwake zilizotolewa leo zimekuwa za kusikitisha saana hasa ikizingatiwa kuwa alikuwa bado anaendelea kuitumikia jamii na hasa jimboni mwake. Mbali na ubunge pia alikuwa mjasiriamali aliyeheshimika saana kwa kusaidia kunazisha na kuongoza baadhi ya makampuni yaliyojihusisha na masuala ya biashara na uchumi na pia kama mhadhiri katika Chuo cha Biashara jijini Dar.
Amekuwa mbunge wa Jimbo la Mbeya Vijijini kwa awamu iliyoanza mwaka 2005.
Kila mtu anaweza kuwa na jema la kusema kuhusu Mhe. Nyaulawa, lakini kwa sasa naungana na ndugu, jamaa, marafiki, wanafunzi na wafanyakazi wenzake katika wakati huu mgumu na wa masikitiko.


MUNGU AILAZE ROHO YAKE MAHALI PEMA PEPONI

No comments: