Thursday, November 26, 2009

Kutoka Bloguni!!!! Twende majaridani na magazetini

Kakangu Albert wa blogu ya MWANGAZA aliwahi kuuliza kuhusu itakavyokuwa kama makala nono ziandikwazo kwenye blogu zetu zingeweza kufika kwenye magazeti. Tukawa tunawafikia kina Bibi yangu kule Bushasha na wengine mikoani. Lakini si jambo geni kwani tuliwahi kulijadili siku ileeeee ambayo Da Koero aliandika kuhusu Yasinta. Na binafsi nikachukua hatua moja mbele na kumwambikia mhusika wa Gazeti tuliloona lina nafasi kubwa ya kutuunga mkono kwani ni la mwana-blog na lina wana-blog wengi la KWANZA JAMII kuhusu hili.
Na leo nilipofungua hapa kwa Da Koero na kukuta anahamasika kusogea gazetini nikajumiisha na maandishi haya ya Kaka Matondo nikaona ni vema kukumbushana kuwa kutakuwa na manufaa na itawafaa JAMII ambayo tunahangaika kuielimisha na kuikomboa.
Barua yangu kwa KWANZA JAMII ilisema


Kutoka bloguni
Saturday, April 18, 2009 3:24 PM
From:
"Mubelwa T. Bandio"
View contact details
To:
habari@kwanzajamii.com
Amani, Heshima na Upendo kwenu nyote.
Natumai kuwa mu-wazima na mnaendelea vema na harakati za kuikomboa jamii. Kwanza niwapongeze kwa ujio wa gazeti jipya lenye uelimishaji. Gazeti lenye mchanganyiko wa chambuzi na kuonekana kuwa na mtazamo wa kuinusuru jamii.
Pia katika nililogundua ni kuwa gazeti hili lina timu ambayo wengi wao pia ni waandishi wa blogu mbalimbali za ki-chambuzi. Kwangu ni nyota njema kuwa waandishi wa blogu wana nafasi nzuri ya kuweza kusogeza habari kutoka kwenye mfumo huu kwenda kwenye uchapishaji (japo wengine ndiko walikoanzia). Lakini nakumbuka kuwa wiki chache zilizopita mmoja wa wana-blog (Dada Koero Mkundi wa www.koeromkundi.blogspot.com ) aliandika habari kumhusu binyi mmoja aitwaye Yasinta ( http://koeromkundi.blogspot.com/2009/03/kutana-na-yasinta-mjasiriamali.html) ambayo iliwagusa wasomaji wengi na kukawepo na maoni ya namna ya kuwezesha kufikisha habari kama hizo "nje ya blogs" na kuna waliosema wangekunadikia kuomba ufikirie hili. Sina haika kama walifanya hivyo, bali nami nimeona niandike kuona kama unaweza kufikiria kuwa na "kona" ya kutoka bloguni ambayo kwa kutumia waandishi wa blog wanaoandika kwenye Kwanza jamii mkaweza kuchagua habari kutoka blog mbalimbali mnazohisi zinaifaa jamii yetu.
Ni hayo tu na naamini utayafikiria.
Blessings

Wednesday, November 25, 2009

Labda "akutendeaye mabaya" ndiye akujaliye!!!!

Mara kadhaa katika blogu zetu za kimaandishi tumejadili kuhusu suala la UBAYA. Kuanzia kuuangalia kama upo mpaka kuona kama kile kiitwacho ubaya kama kina faida na kisha kuangalia kama tunahusisha lile liitwalo UBAYA na matukio halisi ya maisha yetu. Tumejadili pia kuhusu KUWAOMBEA WALE TUWAONAO KAMA ADUI ZETU kwa kuwa nao wana nafasi kuuubwa saana katika ukuaji wetu. Yaani wanapojitahidi kuhakikisha tunashindwa, wanatuongezea moyo na maarifa ya kufanya vema zaidi. Watu hawa pia ni muhimu saana kwetu. Lakini pengine la kujiuliza ni kuwa LIPI TUONALO KAMA UBAYA?? Unadhani tafsiri yako ya UBAYA inaweza kuwa na ukweli katika kuleta suluhisho la nani kakufanyia nini? Waswahili wanasema TENDA WEMA NENDA ZAKO, nami najiuliza kama ukitenda wema (ilhali atendewaye auona kama ubaya) kisha ukaenda zako unadhani mtendewa atagundua kuwa ni wema kama halitatokea baya zaidi ya ulilomtendea??
Ninavyozidi kuishi nazidi kugundua kuwa pengine akuibiaye sasa hivi shilingi laki moja anakukumbusha na kukuonya kuwa mahala hapo si salama na usiwe unabeba pesa hovyo kabla hujajenga tabia hiyo na kuanza kutembea na milioni kisha zikaibiwa.
Labda mkioana na kuachana ndani ya miezi michache si mkosi bali yaweza kuwa nafuu kuliko kusubiri baada ya miaka kumi ya kuchuma pamoja na watoto kadhaa kisha mmoja wenu analazimika kubaki kwa ajili ya "matunda" hayo mlovuna pamoja.
NI WAKATI AMBAO TUNATAKIWA KUTUMIA KILA KITUKUTACHO KUJIFUNZA NA SI KULAUMU NA KULALAMA
Labda nikukumbushe "hadithi" hii inayoweza kuoanisha vema nisemayo na "kichwa cha habari"

IF YOU ARE UNHAPPY.
Once upon a time, there was a noncomforming sparrow who decided not to fly south for the winter. However, soon the weather turned so cold that he reluctantly started to fly south. In a short tile ice began to form on his wings and he fell to earth in a barnyard, almost frozen. A cow passed by and crapped on a little sparrow. The sparrow thought it was the end. But, the manure warmed him and defrosted his wings. Warm and happy, able to breathe, he started to sing. Just then a large cat came by and hearing the chirping, investigated the sounds.
The cat cleared away the manure, found the chirping bird and promptly ate him.

THE MORAL OF THE STORY
1: Everyone who shits on you is not necessarily your enemy.
2: Everyone who gets you out of the shit is not necessarily your friend.
And
3: If you're warm and happy in a pile of shit, keep your mouth shut.

Tuesday, November 24, 2009

Hongera wana-STRICTLY GOSPEL

Kwa muda sasa tumekuwa tukijaribu kupiga hatua ya ziada kwenye uhabarishaji na uelimishaji wetu kuwagusa wengi wahitajio lakini hawana namna ya kupata habari ihizi kupitia mtandao. Tumejadili kuhusu kuweka makala na maandishi yetu kwenye MAGAZETI na MAJARIDA na bado naamini tutafanikisha jambo hili ili tuweze kuwafikia wengi zaidi.
Kwa sasa niwapongeze wanaSTRICTLY GOSPEL kwa kufanikiwa kuvuka kizingiti hiki kwa kuweza kuanza kuchapisha jarida lao liendalo kwa jina hilohilo.

Wamesonga hatua moja mbele kutoka wana-mtandao pekee (blog) mpaka mtandao na jarida.
JIANDAE KUPATA NAKALA YA JARIDA HILI HIVI KARIBUNI

Monday, November 23, 2009

Za Kale vs Maisha ya Sasa..........MWISHO WA MWEZI

Na hizi ndizo tarehe. Tarehe za UNDUGU KUKUA, tarehe za wengine kuzikimbia nyumba zao (halisi), tarehe za wengine kuvesha vimada, tarehe za kinamama wauza "pampula (pombe za kienyeji) kuona ongezeko la mapato, tarehe za watu kuzhelewa kurejea nyumbani, tarehe za nyimbo kuongezeka uziku toka kwa walevi wanaotoka vilabuni, tarehe za vipigo kuongezeka ndani ya nyumba (kwa kuwa tu fulani kauliza amechelewa wapi), tarehe za wezi kujiajiri zaidi (kwani wanajua mifuko imetuna), tarehe za wengine kuhatarisha maisha ya wengine.
Hivi nimesema kuhusu tarehe za wengi kuambukizwa maradhi (kwa kuwa tu wamelewa na kila aliye mbele yao ni mrembo hata kama kaathirika). Ndio zileee siku ambazo Prof Jay alisema ni "mwendo wa viti virefu jirani na nyama choma na toto mbili tatu ..........hii watu wa pombe wanasema ni kupoteza mawazo ingawa mara nyingi hutokea wakati unazo"
Ni mwisho wa mwezi. Wenye mambo na vijambo. Ambao kila ufikapo basi wengi twajua iwavyo. Ni "mishemishe" kila mahala, kila mtu ni "busy" kwa kwenda mbele na kwa hakika muda unaohitaji umakini kwani watu wanakuwa wanaendeshwa na pesa kuliko akili zao binafsi.

MWISHO WA MWEZI una mambo mengi na kama unashani yalianza sasa hivi, sikiliza Vijana Jazz Band (enzi za kina Hayati Hemedi Maneti na Eddie Sheggy) wanavyokukumbusha tangu enzi hizo jinsi mwisho wa mwezi ulivyokuwa.
** Zilipendwa ni kipengele kinachokujia siku za Jumatatu kukuletea muziki wa kale kuhusisha na maisha, muziki ama sanaa ya sasa katika nyanja mbalimbali. Unaweza kusikiliza nyimbo nyingine ndani ya kipengele hiki kwa kubofya hapa, ama mitandao shirika hapa**

Saturday, November 21, 2009

Penye raha pana karaha.....Kuwa makini

Sina hakika ni wangapi wanajua kuwa waajiri hutumia mitandao ya jamii (km facebook, myspace, hi5 na mingine) kuangalia SIFA za yule anayetafuta ajira kabla hawajafikiria kumuajiri?? Ukweli ni kuwa huwa wanafanya hivyo ili kusaka SIFA ZA ZIADA ambazo wengi wetu hatuzioneshi katika Resume na CV zetu za kuombea kazi. Hata namna tunavyojieleza kuwaomba watu watuachie VOICE MAIL huangaliwa na kuhusishwa na aina ya ajira unayoomba.
Ni kwa kutotambua hilo ama kwa kufikiri tumeweka "settings" zetu katika usiri wa kutosha, tunajikuta tukiendeleza maongezi na taswira ambazo kwa hakika ZINAONESHA UPANDE WA PILI wa sisi ambao si wakati wote upande huo unakuwa na manufaa kwetu.
Basi na iwe kumbukumbu kuwa TUNASTAHILI KUWA TULIVYO na kujitahidi kutokuwa na "taswira" zisizo zetu ama kutobeba kile ambacho hatuwezi kumudu gharama zake.
Ni vema kuishi kwenye mitandao hiyo kama ambavyo unaishi maisha ya kawaida ili kukuepusha na "moto-baridi" za maisha.
Nimekumbuka haya baada ya kusoma kisa cha mama mmoja ambaye amepoteza mafao yake baada ya taswira katika ukurasa wake wa facebook kumuonesha mwenye furaha kuliko alivyoandikishwa kazini. Hiki ni kisa cha kweli na mama huyo sasa anajuta kwa kuwa na picha hizo ambazo zimetibua malengo yake a maisha.
Unaweza kufuatilia kisa kamili HAPA
Tuwe makini tusije poteza yaliyo muhimu kwetu kwa raha za muda.
Kumbuka KILA PENYE RAHA KUNA UWEZEKANO WA KUWEPO KARAHA

SAVE ALBINO BENEFIT CONCERT

Blogu hii inapenda kuungana na ALBINO FULANI na washiriki wote katika onesho hili maalum la kuwachangia ndugu zetu wenye matatizo ya ngozi (ALBINO). Licha ya uhitaji wa kuzaliwa nao walionao ndugu zetu hawa, lakini wenye uchu wa mali na utajiri wamekuwa wakiwawinda ili kupata viungo vyao kujitajirisha. Hili limewafanya ndugu zetu hawa kuishi maisha ya kujificha ndani ya nchi yao kuwakwepa watu hawa wenye imani POTOFU za kishirikina.
ASANTE ALBINO FULANI NA WASHIRIKI WOTE KWA ONESHO HILI LA MANUFAA.

SCHOLARSHIP FORUM

Napenda kuwatangazia ndugu wadau wote kuhusu maboresho niliyoweka katika mtandao kuhusiana na mambo ya scholarships. Nimeanzisha SCHOLARSHIP FORUM ambayo ni http://www.scholarshipnetwork.ning.com/ Hii ukijiunga itakusaidia kupata updates za kila scholarship info ninayoiweka katika link hiyo. Kila tangazo la scholarship niki-post hapo utapata e-mail kukujulisha.

Pia blog http://www.makulilo.blogspot.com/ nayo itaendelea kuwa hewani kama kawaida.

Mdau
MAKULILO, Jr.
San Diego, CA

Kiswahili Wikipedia Competition

What is the Kiswahili Wikipedia Challenge?
This is your opportunity to bring Africa's information online by creating Wikipedia articles in Kiswahili.
You can participate by translating English Wikipedia articles into Kiswahili or by writing your own articles from scratch. You can choose your own topic to write about.

Are you a pursuing a degree in Physics?
Translate the entry for 'condensed matter' from English to Kiswahili.

Studying literature?
Write an entry on your favorite local author. Or translate an article about your favorite musician or sports team. Just think about what topics would be of interest to some of the 100 million Kiswahili speakers worldwide.

Read more about it at: http://www.wavuti.com/4/post/2009/11/kiswahili-wikipedia-competition.html



Subi: wavuti.com

Friday, November 20, 2009

Them, I & Them.....NEW SONG......Nasio


"HALI YA UCHUMI WA DUNIA NI MBAYA"
Kauli hii tumeisikia mara kwa mara na imekuwa ikitumika zaidi ya UHALISIA wake. Ni kauli ambayo inatumika kuwatisha wananchi na pia kutumiwa na WATAWALA KUKWEPA MAJUKUMU YAO.
Hivi sasa kila kitu kisichokamilika chaonekana kuwa na sababu hii ya "mvurugiko wa uchumi". Hata wabunge hawatembelei majimbo ya (japo wanapaswa kuishi huko) sababu hii

  • Wananchi hawapati maendeleo sababu ya mvurugano wa uchumi.
  • Sera za serikali ya awamu ya nne hazikamiliki kwa sababu hiyohiyo
  • Sitashangaa nikisikia kiongozi akisema WANAKULA RUSHWA SABABU HIYO.
LAKINI KUNA UKWELI KATIKA KAULI HII?
Ukweli ni kwamba WANASIASA hawana mipango endelevu na sasa wanatumia hili la uchumi kuharibika kama kisingizio. Ni kweli kuwa kuna mambo yaliyokwamishwa na mvurugano wa uchumi, lakini bado kuna mengi tunayoweza kufanya kwa NGUVUKAZI na kuwezesha kuibadili jamii.
Kujenga zahanati, Kuchimba mitaro, Kuchimba visima, Kutokomeza Rushwa, Kuchonga / kutengeneza madawati na mengine kama haya ni baadhi ya mambo yanayohitaji nguvukazi na ushirikiano kati ya WATAWALA na wananchi.
HUU SI WAKATI WA KUTISHANA. NI WAKATI WA KUELEZANA MAJUKUMU YETU NA KUPANGA NAMNA YA KUYAKABILI. Na kwa kuyakabili kwa umoja (licha ya ugumu wake) tutafanikiwa na kujivunia. Hizi ni nyakati ambazo wanasiasa wanapaswa kuwaeleza wananchi kuwa HALI YA UCHUMI ISEMWAYO SI MWISHO WA DUNIA na kisha kuwaonesha mahala pa kwenda kutua mzigo wao wa msongo wa mawazo (stress)
Sijui ni kwanini kila wazungumziapo KUONDOA STRESS wanahusisha na mto, lakini ukweli ni kuwa KILA MTU ANA "MTO" WAKE ANAOWEZA KWENDA NA KUTUA MZIGO WAKE NA KUANZA UPYA MAISHA MAPYA, MAISHA CHANYA NA KUFANIKIWA.
Leo hii tunaye Nasio Fontaine anayezungumzia kuhusu kutambua ulipo "mto" wako kisha kuelekea huko "kutua mzigo wako" kisha kuanza maisha mapya. Anasema anajua MUNGU NDIYE SULUHISHO PEKEE HATA KAMA UNAHISI KILA KITU HAKIENDI VEMA KWAKO.
Msome na kumsikiliza katika wimbo huu NEW SONG
Yeah!, we really wanna say now.
Come down to the river, lay down your burdens,
walk away and singing a New Song, sing a Brand New Song
Come to Mount Zion Jah Seh, lay down your burden
Walk away and singing a New Song
Sing a brand new song

I know your burdens feels so heavy,
you feel you couldn't carry no more,
yet here comes another hurdle,
higher than the one before,
and i know the road you trod,
is rough and rugged,
still i know,
the Lion of the Judah is the only solution"

Come down to the river, lay down your burdens,
walk away and singing a New Song, sing a Brand New Song
Come to Mount Zion you heavy laiden, lay down your burden
cause you've been burden for much too long

Journey is tough, the road is steep
And there's no rest for weary feet.
Yet here come another stumbling block
Greater than the one before
And i know that you've been through
Soo Much, Too Much
And HARDER THE BATTLE, TOUGHER THE FIGHT
SWEETER THE VICTORY

Come down to the river, lay down your burdens,
walk away and singing a New Song, sing a Brand New Song
Come to Mount Zion Jah Seh, lay down your burden
cause you've been burden for much too long
For much too long

Come, come, come come, come to mount Zion
Lay down your burden
Cause in my Father's House
There is many a Mansion

**Them, I & Them ni kipengele kikujiacho kila Ijumaa kinachoelezea kazi za wasanii (Them) kulingana na maono yangu (I) kwa ajili na manufaa ya hadhira (Them)**
Kwa nyimbo zaidi ndani ya kipengele hiki bofya hapa.
IJUMAA NJEMA

Thursday, November 19, 2009

TUWA-USA.......MASHUJAA WETU

Wasomi, wanaharakati wanaosaidia elimu nyumbani
"Do you see the smiles on their faces
after you have done what you do best.
Do you see satisfaction on their faces
after you have blessed them with your gift.
You don't think it's much
but to them it means the world.
They wake up in the morning and wish you were there
You don't have to lie to gain their trust.
You have never won a Nobel prize,
they have never seen you on the TV
your little contribution makes their lives a little bit better every day
YOU ARE A HERO, YOU ARE A HERO."


Haya maneno ndiyo aliyoanza nayo Phillip Lucky Dube katika wimbo wake HERO alipokuwa akitoa heshima kwa wale ambao wana nafasi ndogo katika jamii lakini wakizitumia ipasavyo kuleta MABADILIKO CHANYA KWA JAMII YAO. Nami leo sina ninaloweza kupunguza ninapowafikiria hawa wanacham awa Chama Cha Wanawake Wasomi wa kiTanzania waliopo nchini Marekani ama The Tanzanian University Women's Association (TUWA-USA)ambao hivi karibuni walifanikisha moja ya adhma zao kuu kwa kuwezesha kupatikana kwa madawati 32 yenye zaidi ya thamani ya shilingi 1,892,000 kwa shule ya msingi Mtakuja ambayo ni moja kati ya shule nyingi sana zenye uhaba wa madawati nchini. Mlezi wa TUWA-USA Meja Jenerali mstaafu Benjamin Msuya akimkabidhi Kaimu Afisa Elimu Manispaa ya Kinondoni Bwn Faustine Kikove moja ya madawati 32 yaliyochangwa.
Madawati hayo yaliyokabidhiwa na mlezi wa Chama hicho Meja Jenerali Mstaafu Benjamin Msuya ni hatua kubwa katika kusaidia kuimarisha mazingira ya elimu nchini hali itakayosaidia kuwafanya wanafunzi kufanya vema darasani. Si kwa wanafunzi tu, bali pia mchango huu uliwezesha ajira kwa mafundi seremala
Kinachonipa faraja zaidi ni namna ambavyo wanachama wa TUWA-USA wameweza kufanikisha hili licha ya MAJUKUMU MENGI waliyonayo kimaisha. Chama hiki kinaendeshwa kwa kujitolea na wanachama wake wana majukumu ya kifamilia zaidi (wengine wakiwa ni kinamama wanaolea familia na wengine wakisafiri kutoka majimbo ya nje ya hapa DC Metro ili uanikisha nia yao) na wamekuwa wakifanya hata mikutano kwa njia ya simu ili kufanikisha adhma yao. Leo hii kuona wanafanikisha hili katika mazingira magumu kama haya inaongeza furaha na kunikumbusha alichoimba Nasio Fontaine kuwa "harder the battle, yougher the fight, SWEETER THE VICTORY"
Blog hii ilibahatika kushiriki katika matukio ya kusaidia kutunisha mfuko ili kiweza kufanikisha jambo hili (kama ilivyoliripoti HAPA)na ilijionea CHANGAMOTO mbazo kinamama hawa wanakabiliana nazo katika kusonga mbele, na leo NAWIWA furaha kubwa kuleta shukrani kwa wanachama wote kwa kusimama imara katika azma yao na kuifanikisha jambo hili ambalo ni ZAWADI KWA JAMII NZIMA YA KITANZANIA. Mwl Albert Juakali wa Shule ya Msingi Iboma wilayani Chunya mkoani Mbeya akifundisha wanafunzi wa darasa la kwanza chini ya m'buyu.
Vyama ni vingi, JUMUIYA ni nyingi na mahitaji ni mengi, na ni sisi wenyewe tunaohitaji kusimama kidete kuweza kufanikisha tatizo hili na kuboresha mazingira na maisha bora kwa kila mwanafunzi kwa kujitolea kile tuwezacho katika kufanikisha azma hii. Si lazima kiwe kikubwa, bali tukitoa kwa moyo kitafaa. Kama alivyosema Mother Theresa kuwa "I can do no great things. Only small ones with GREAT LOVE." Nasi tuungane katika kuchangia na kufanikisha kuwaondoa watoto katika mazingira haya. Kama TUWA-USA wameweza kusimama katika MALENGO yao kama walivyoeleza HAPA, ni kwanini vyama na jumuiy anyingine zisiweze??
Licha ya kusaidia kuinua elimu kwa watoto (hasa mabinti) nchini anzania, TUWA-USA imekuwa ikijitahodo kufanikisha njia za kuwezesha waTanzania walio hapa kujua namna ya kupata elimu bora hapa nchini (BOFYA HAPA)
Unaweza kujua na kujifunza mengi kuhusu TUWA-USA kwa kutembelea tovuti yao HAPA
Kwa Dada zangu wa TUWA-USA.
ASANTENI SAANA.
TWAWATHAMINI, TWAWAPENDA, TWAWAOMBEA NA KUWATAKIA HERI KATIKA KILA JEMA MPANGALO KUFANYA KWENU NA KWA JAMII YETU
Kwa blog ya Changamoto Yetu, ninyi ni
HEROES
Wimbo huu ni maalum kwenu wana-TUWA-USA
BLESSINGS
Picha toka Blogs za Kaka Issa & Ahmad Michuzi