KUMRADHI

Kutokana na kubanwa na masomo, mabandiko hayatakuwa kila siku kama awali.
NAWAPENDA



Tuesday, May 21, 2013

TBC....Oneeni huruma kodi zetu basi!!!

Yaani hata mnapoambiwa mara tatu na zaidi bado ham'badili tovuti yenu tuuuuuuu!!!
Ina maana makusanyo yote hayo mpatayo hamuwezi kuwa na mtu wa IT?
Ukisoma utaona maelezo kwenye ukurasa huu nilioubandika hapa chini yanasema Taji Liundi ni mkuu wa Idhaa japo alikaririwa akisema kuwa alishatoka TBC
Maelezo hayohayo yanasema watazindua kituo 2009 japo ukurasa ulikuwa updated 2010
Ngoja niwanukuu nisipoteze uhondo "It is proposed that the official launch of TBC International to be January 1 2009. 
COMING SOON 
Last Updated ( Friday, 05 November 2010 03:35 ) "
NAWAPENDAJE TBC??????

Kijiwe cha Ughaibuni.....VIJIMAMBO.

Karibu katika kipindi kingine cha Kijiwe cha Ughaibuni kinacholetwa kwenu na Blog ya Vijimambo.
Katika kipindi hiki kinachojadili mambo mbalimbali, leo wanaanza na masuala ya mahusiano na zaidi, wameshirikisha kinamama wawili kuleta usawa.
Karibu uungane nao

Monday, May 20, 2013

Ana kwa ana ya Mr. Abdallah Kitwara na VIJIMAMBO

Hii ni sehemu ya kwanza ya mahojiano kati ya blog ya Vijimambo na Rais wa VIZION ONE Inc. Bwn. Abdallah Kitwara
Katika mahojiano haya, Bwn. Kitwara anaeleza historia yake kwa ufupi, shule alizosoma na kilichomshawishi kufungua kampuni hiyo ya Vizion One Inc.
Pia, anaeleza ni sababu gani zilizosababisha kutumia jina VIZION yenye "Z" badala ya "S"
Mbali na Vizion One, Inc. ana kampuni gani nyingine hapa Marekani na Tanzania?
Nini siri ya mafanikio ya kampuni yake?
Anauchambua vipi "UTUMWA WA KISASA" hapa Marekani?
UNGANA NAO
 

Ana kwa Ana ya Bwn. William Chiume na Swahili Tv

Makamu mwenyekiti wa Klabu ya Gymkhana Bwn. William Chiume akihojiwa na SWAHILI TV.

Faida za mazoezi ya uvutaji pumzi.......Freddy Macha

Mwandishi Freddy Macha anatathmini zoezi la kichwa na uso -linaloboresha wajihi, haiba, sauti na mishipa muhimu ya fahamu.
UNGANA NAYE HAPA
 

Sunday, May 19, 2013

Usiku wa kinadada wa kiTanzania...Juni Mosi '13

Zimebaki siku chache kabla ya tukio hili la kipekee kwa kinadada.
Na ticket ndiyo zinayoyoma.  
Hivyo......Jipatie ticket yako sasa. 
Tiketi ni $65 nayo inajumuisha..
- Dinner and dance
- Open Premium bar
- Free Parking (Parking zipo za bure hotelini)
- Live performances
- Fashion shows
- and more
To buy ticket online (with your credit card or PayPal) CLICK HERE 
- you will be charged $2.00 processing fee (P'se call us after paying with PayPal)
Kwa ufafanuzi zaidi angalia video hii mpya ya TANO Ladies

Saturday, May 18, 2013

Unapotafutwa mstari mwembamba kati ya SAYANSI na MISINGI YA UHAI kuwezesha UHAI

Hivi karibuni kumekuwa na harakati za wanasayansi / watafiti kutafuta tiba za magonjwa mbalimbali yanayoonekana kuziathiri jamii. Ukweli ni kuwa, wanalosaka, ni kutafuta namna ya kuweza kurefusha maisha, lakini katika hilo, wanaonekana kukwaza baadhi ya wanaoamini katika DINI Haya ni matoleo ya wiki hii toka kituo cha NPR ambayo yamezungumzia "mafanikio" katika sayansi ambayo yanaonekana kuwa n"anguko" kwa wenye imani.

Wednesday, May 15, 2013

Thaminisha.......Mr & Mrs Abdallah Kitwara

Photo Credits:  Vijimambo blog
Nawasikia(ga) tu wakisema "nyuma ya mafanikio ya mwanaume, kuna juhudi za mwanamke"
Labda ni kweli..
Lakini pia, kuna UKWELI kuwa huyo MWANAMUME yuko na huyo amuwezeshaye kwa kuwa naye amejitolea mengi kuweza kuwa naye.
Kwa hiyo, nyuma ya mafanikio ya kila mwanaume, kuna juhudi za mwanamke ambaye alichaguliwa, kukubaliwa na / ama kuendelea kuwa na mwanaume aliyenaye.
Labda....NYUMA YA MAFANIKIO YA KILA MTU, YUKO MTU.
Kwanini nimeanza na nukuu hiyo?
Ni kwa kuwa nataka ku THAMINIsha Kaka yangu Abdallah Kitwara na mkewe.
Hawa wamekuwa chachu ya maendeleo ambayo binbafsi NIMESHUHUDIA na pia NINAYAISHI.
Kabla sijatambulishwa kwake na mwenzangu katika kazi (Abou Shatry), nilipata kujua USHIRIKI wake kwenye jamii kwa kuona UDHAMINI wake kwenye timu ya Tanzania DMV
Jezi za timu zilizodhaminiwa na kampuni ya Vizion One Inc inayomilikiwa na Mr & Mrs Kitwara.
Baada ya kumuona katika hili, tuliwasiliana nao kuangalia namna ambavyo wangeweza kuwa na ushirika katika harakati zetu za kukuza mkakati wetu wa kuanza kufanya uzalishaji wa AUDIO na VIDEO kwa matukio yanayotukia hapa Washington DC na vitongoji vyake.
Tulipowasiliana nao, walikuwa wakarimu sana kutualika kwao na kisha WALITUWEZESHA KUPATA VIFAA VYA KISASA NA VYA KUTOSHA KUFANYA KAZI ZETU.
Huu ulikuwa ni zaidi ya msaada.
Hii ilikuwa zaidi ya baraka
Hili ni zaidi ya DENI LA KUSONGA MBELE
Hili walilotenda wapendwa hawa ni zaidi ya ambalo tulitegemea na baada ya kukamilisha manunuzi, tukapata (pamoja na mambo mengine) kamera ya kisasa saana
Mpiga picha mkuu wa Jamii Production Abou Shatry
Ni kwa uwezeshwaji wa wapendwa hawa, tukaweza kuanzisha JAMII PRODUCTION ambayo imejikita katika kuhakikisha inaELIMISHA, BURUDISHA na KUKOMBOA JAMII kwa mahojiano, mijadala na mambo mbalimbali
  
Ukweli ni kuwa, hapa tulipo tusingefika kwa wakati huu bila kuwezeshwa na ndugu hawa wawili.
Na si sisi pekee ambao tunajivunia nafasi yao katika jamii. Bado tumeona udhamini wao katika matukio mbalimbali ya jamii.
Mkurugenzi wa Vizion One, Abdallah Kitwara akimkabidhi Dj Luke cheki ya kusaidia matayarisho ya sherehe ya Blog ya Vijimambo itakayofanyika July 6, 2013 maeneo ya Capitol Heights, Maryland.
 Photo Credits: Vijimambo blog
Nikirejea kwenye mwanzo wa post hii, labda ni kweli kuwa mafanikio ya kila mmoja yametokana na ushirikiano wa kila mmoja wao, na kwa hakika napenda kuwaTHAMINISHA Mr & Mrs Abdallah Kitwara kwa nafasi yao katika jamii.
June 7, 2010 niliandika post hii isemayo UTAKUMBUKWA KWA DESHI YA MAISHA YAKO ambapo kati ya niliyosema ni kuwa "Maisha yana hatua tatu muhimu na mbili kati ya hizo (KUZALIWA na KUFA) hazina mjadala, na moja ambayo ndiyo tusiyoijua, ndiyo muhimu kwetu. Ndio hiyo niitayo "deshi". Na kwa kuwa kila mtu anazipitia mbili nilizozitaja, basi hakuna anayezijali wala kumkumbuka mtu kwazo. Ina maana maisha yetu yamebaki kwenye hiyo hatua iliyo kati ambayo ndiyo tunayoihangaikia..... 
......Leo hii kila aitwaye shujaa ama fisadi ama mshkiliza rekodi, ama mtakatifu ama mkatili ama mwenye cheo chochote ulimwenguni anakumbukwa kwa kile alichofanya kwa muda wake wa "deshi" ambao ni wa katikati ya kuzaliwa na kufa. 
Basi tuchuje vema maisha yetu na kuangalia na kutambua kuwa kwa kila utendalo sasa ndilo lenye kuweka historia yako mbeleni."
UKWELI NI KUWA...
Najivunia namna ambavyo Ndugu zangu hawa wamewezesha maisha ya wengi
Nami nawatakia baraka katika maisha haya ambayo punde mmesherehekea miaka kumi ya ndoa pamoja
Video hii iliyo muhtasari wa sherehe yao kuadhimisha miaka kumi ya ndoa ni kwa hisani ya IskaJoJoPhotography 


Kwangu na kwa jamii ijuayo mema, nyinyi ni HEROs
Na wimbo huu hapa chini, ni maalum kwa ajili yenu

**THAMINISHA ni kipengele kinachounganisha makala ama matoleo mbalimbali ya watu mbalimbali wanaojitolea kuboresha maisha ya wengine na hata wale wanaoona vema kuthaminisha yale waliyotendewa na wengine. Kwa matoleo zaidi BOFYA HAPA**

Tuesday, May 14, 2013

Hongera na Karibu Balozi Mulamula

Photo Credits: Sunday Shomari blog
Katika taarifa yake ya leo, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Jakaya Mrisho Kikwete ametangaza kujaza nafasi za mabalozi wa Tanzania katika nchi za Marekani na Falme za kiarabu.
Mmoja wao
Rais Jakaya Kikwete ameteua mabalozi ili kujaza nafasi zilizo wazi nchini Marekani na Umoja wa Falme za Kiarabu.
Kwa mujibu wa taarifa ya Katibu Mkuu katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, John Haule, Rais Kikwete amemteua Balozi Bi. Liberata Rutageruka Mulamula (pichani juu) kuwa balozi wa Tanzania nchini Marekani (Washington D.C.) kujaza nafasi iliyoachwa wazi na Mhe Balozi Mwanaidi Maajar aliyemaliza muda wake.
Balozi Mulamula, ambaye anakuwa Balozi wa pili wa kike nchini Marekani ni Msaidizi wa Rais Mwandamizi katika masuala ya kidiplomasia na aliwahi kuwa Katibu Mtendaji wa kwanza kuiongoza Sekretarieti ya Nchi za Maziwa Makuu kwa kipindi cha miaka minne kuanzia Januari, 2007 hadi Desemba, 2010.
Pia, Rais Kikwete amemteua Balozi Bw. Mbarouk Nassor Mbarouk kuwa Balozi wa Tanzania katika nchi ya Umoja wa Falme za Kiarabu. Hadi uteuzi huu unafanyika, Bw. Mbarouk alikuwa Afisa Mwandamizi katika ubalozi wa Tanzania nchini Urusi (Moscow).


 Chonde Chonde Mhe. Makalla...Kabla hujawaketisha Ruge na Jay Dee

Photo Credits: Vijimambo Blog
 Moja kati ya habari ambazo zimesambaa wiki iliyopita, ni HII ya Naibu Waziri wa Habari Michezo Vijana na Utamaduni Amos Makalaambaye amenukuliwa "kutangaza hadharani kulivalia njuga suala la mzozo kati ya Mkurugenzi wa wa Kampuni ya Clouds Media Group Ruge Mutahaba na msanii nyota wa kike wa Bongo Fleva Judith ‘Wambura Lady Jaydee"
  Hili ni JAMBO JEMA na la kupongezwa kwa kuwa hakuna ambaye anapenda kuona MZOZO HUU ambao kwa hakika wengi wanauona USIO WA MAANA KWA JAMII YETU ukiendelea kutawala vyombo vya habari na kuweka kando masuala muhimu ambayo yangeweza kuanzisha mijadala chanya kwenye jamii yetu.
Lakini...
Pamoja na PONGEZI zangu katika kuondoa hili, napenda kuleta OMBI / TAHADHARI kwa Naibu Waziri kuhakikisha kuwa ANATATUA CHANZO CHA TATIZO HILI PAMOJA NA YALE YAFANANAYO NA HILI badala ya kujikita kwa RUGE na LADY JAY DEE.
Ninalomaanisha ni kuwa aangalie kinachosababisha watu wamuunge mkono Lady Jay Dee na wengine wamuunge mkono Ruge japo wote wanapingana na ni katika KAZI MOJA (muziki)
CHONDE CHONDE Mhe Makalla, kabla hujakutana na WAPENDWA HAWA (wachukianao), naomba ufanye uchunguzi kujua kile ambacho kiko nyuma ya kinachosikika na kusomeka kwenye mitandao.
Kwa yeyote mwenye akili timamu, atatambua kuwa KINACHOLALAMIKIWA NI ZAIDI YA KINACHOSEMWA.
Kumekua na matatizo katika fani nzima ya muziki nchini Tanzania. Na sehemu ya matatizo haya inatokana na serikali yetu.
Oktoba 12, 2008 niliandika hapa kuhusu Wasanii kama "chombo cha starehe" cha serikali na kati ya niliyoeleza ni kuwa
"Pengine kubwa na lenye kuonesha "kuthamini burudani" ya wasanii wa nyumbani ni pale wanapoalikwa kwenda kuwatumbuiza waheshimiwa wabunge ambao kwa miaka nenda rudi wameshindwa kuweka sheria ambazo zingelinda haki na mapato yao.
Najua Waheshimiwa wabunge na wenye mamlaka wana-enjoy saana sanaa ioneshwayo na wasanii wetu, lakini kama wanaishia kuwalipa pesa ya onesho (kama hayo ya bungeni) ama kuwapigia makofi na pesa ya onesho la airport, ama kama ni suala la mkataba wa kupiga kampeni na ama propaganda za wasanii, basi napenda watambue kuwa "kwa mujibu wa tafsiri niliyopewa na mwalimu wangu ninayemuamini, nao wanawatumia wasanii kama chombo cha starehe".
Hivi si wakati wa kuweka sheria kali kwa wale wanaosambaza kazi za wasanii? Si wakati wa kupitia vyema hakimiliki na unyonyaji ufanywao kwa wasanii na watu wachache kujinufaisha kwa jasho la wasanii? Ni kweli kuwa viongozi serikalini hawayaoni haya ama hayana "sound" ya kisiasa? Nachukia kila ninapoona "politrix" inaingilia uhalisia wa maisha na kuweka pembeni suluhisho linaloweza kumnyanyua msanii, familia na taifa kwa ujumla.
Lakini pia lawama hizi ama haya yote yatokeayo yana mkono wa wasanii wenyewe. Kutokuwa na umoja miongoni mwao, kuendekeza njaa na majungu baina ya baadhi yao na kutokuwa na elimu na utawala wa KAZI YA SANAA kunawafanya wagawanywe na kutumika bila wao kujijua. Kutokuwa na hesabu kamili na halisi za namna ya kugharimisha muda na kazi zao kulingana na hali ya maisha ya sasa ukizingatia kuwa ndio kazi yao wategemeayo kwa maisha ya sasa na uwekezaji wa maisha yajayo...."

 Na ukweli wa hili la UMOJA na KUENDEKEZA NJAA linadhihirika zaidi sasa ambapo katika MGAWANYIKO uliopo sasa, hakuna wanaojitokeza wazi kuunga ama kupinga kinachosemwa na yeyote kati ya Ruge na JayDee.
UKWELI NI KUWA.....

Kati ya hawa washutumianao (hasa katika hili la kazi za muziki), mmoja kati yao alistahili kuwa "MKWELI KWA KILA MSANII" ambaye (kulingana na msimamo na mahusiano yake kikazi) anauona UKWELI toka upande wake wa maisha.
Lakini mpaka sasa tumesikia WACHACHE sana wakizungumzia hili, kama vile lizungumzwalo haliathiri kazi na / ama fani yao.
Ina maana TATIZO LAWEZA KUWA KWANINI HAWAJASEMA NA WAKISEMA NI NINI KITAWAKUTA?
CHONDE CHONDE Mhe MAKALLA.....KABLA HUJAWAKETISHA RUGE NA JAY DEE, tafuta sababu za ukimya uliopo sasa juu ya hili linaloathiri maisha ya wasanii wengi.
Kama ni kweli kuwa asemalo Lady Jay Dee ni "uzushi", basi tuangalie namna ambavyo wasanii wanaweza kutambua wajibu wao katika jamii na kisha kuwajibishwa kwa kusema kisicho sahihi.
Kama ni kweli kuwa asemalo Ruge ni "uzushi", basi tuangalie namna ambavyo vyombo binafsi vya habari ambavyo pia ni wadau wakuu wa ajira za wasanii vinaweza kuwajibishwa pale vinapotenda yasiyo haki kwenye kazi za wasanii.

Na huu ni MTAZAMO wangu kwa namna ninavyoona tatizo.
Labda....namna nionavyo tatizo ndio tatizo

Thursday, May 9, 2013

Ana kwa Ana ya Ebou Shatry na Swahili TV

Ebou Shatry akiwa katika kipindi cha Maisha Ughaibuni moja kwa moja kutoka Maryland, USA.
SIKILIZA SEHEMU HII YA KWANZA

Na katika sehemu hii ya pili, Ebou Shatry Chief wa Swahilivilla blog, anaawasa watanzania wakubaliane na changamoto. Waache kulalamika "Watu wananizibia riziki".
Zaidi anawaomba watanzania wawe kitu kimoja, wapendane na kushirikiana, kama zilivyo jamii za mataifa mengine Ughaibuni.

Kijiwe cha Ughaibuni......Mwanaume...UMEOA ama UMEOLEWA?


Karibu katika sehemu nyingine ya KIJIWE CHA UGHAIBUNI ambayo inajadili suala la ndoa
Sikiliza, Uburudike, Uelimike