KUMRADHI

Kutokana na kubanwa na masomo, mabandiko hayatakuwa kila siku kama awali.
NAWAPENDA



Friday, March 16, 2012

Flora Mbasha kuhudumu Washington DC Metro jumapili hii

Msanii wa muziki wa injili toka nchini Tanzania, Bi Flora Mbasha amewasili nchini Marekani na jumapili hii (March 18, 2012) atakuwa mhudumu mgeni kwa wakazi wa Washington DC na vitongoji vyake katika Kanisa la Huduma ya Injili kwa njia ya Msalaba (The Way of the Cross Gospel Ministries).
Kwa mujibu wa Mchungaji Shideko wa kanisa la The Way of the Cross Gospel Ministires, msanii huyo na wenzake watamtukuza Mungu kwa nyimbo kanisani hapo ambapo pia kundi wenyeji la Sounds of Glory Singers litahudumu.Pia Mchungaji Deogratias Lubala kutoka Tanzania atahubiriIbada hiyo inategemewa kuanza saa saba mchana na kumalizika saa tisa.
Anwani ya kanisa hilo ni:
3621 CAMPUS DR,
COLLEGE PARK. MD. 20740
NYOTE MNAKARIBISHWA

RIVERSIDE.......Culture

Hapa ndio RIVERSIDE kwangu. Ninapopatumia ku-edit Video na Picha mbalimbali, kuwasiliana na wapendwa mbalimbali, kusoma blogs na mambo mbalimbali, kusikiliza miziki mbalimbali na pia "kurusha" CHANGAMOTO mbalimbali. Umeshagundua Riverside yako?
Dunia imekumbwa na hali mbaya ya uchumi ambayo inasababisha watu kushindwa kuzikabili hasira na kupoteza ubinadamu na kutenda yasiyotendeka kwa kuwa tu uchumi umewafanya waishi waishivyo. June 12 2009 niliandika kuhusu Bw. James von Brunn, aliyekuwa na miaka 88, aliyeingia makumbusho ya Holocost hapa Washington DC na kuanza kufyatua risasi zilizoua na sababu zikiwa ni chuki za kibaguzi na pia akilalamikia kumong'onyoka kwa mafao yake ya uzeeni (Soma habari yake hapa) . Mzee huyu alipata stress na hakujua pa kuzitua. Akaishia kufanya maafa. Novemba 5 mwaka huo huo wa 2009, askari mmoja Meja Nidal Malik Hasan alifanya ufyatuaji risasi kwenye kambi moja ya jeshi na kuua askari wenzake 13 na kujeruhi wengine 30 (Soma habari yake hapa).
Matukio kama haya yameendelea kuathiri na kutokea zaidi na zaidi katika nchi mbalimbali. Na lililotokea hivi karibuni, ni la askari mmoja wa Marekani aliyeko Afghanistan ambaye aliamua kuingia mtaani na kuanza kufyatua risasi na kuua watu zaidi ya dazeni moja.
YOTE HAYA YAMEHUSISHWA NA MSONGO WA MAWAZO.
Katika taarifa hii iliyotolewa na mwanasheria John Henry Browne aliyeteuliwa kumuwakilisha, kuna chembe za ukweli kuwa mhusika wa tendo hili alikuwa amekabiliwa na mambo zaidi ya uwezo wa kichwa chake kuhimili na kujikuta aki-SNAP na kutenda aliyotenda. Lakini askari huyu ambaye alikuwa kwenye ziara ya nne ya kikazi vitani na ambaye alipata majeraha makubwa kichwa huko nyuma, hakufurahia kupelekwa tena vitani na alishaonyesha kuchukizwa ama kutoridhishwa na hatua hiyo. Mwanasheria wake anasema "He wasn't thrilled about going on another deployment," na kisha anaongeza kuwa "He was told he wasn't going back, and then he was told he was going."
Hawa ni maskari na watumiaji wa silaha ambao matukio yao yameweza kutangazika. Lakini tunao wengi kwenye jamii zetu. Ambao kwa kusongwa na mawazo wanashindwa kuonyesha upendo kwa watoto wao. Wanakuwa wakali kwa jamii zao na wanaathiri furaha miongoni mwao.Lakini yote haya huja na dalili kiasi, japo si zote huonekana mapema.
NI NANI ANAYEONA DALILI HIZI ZA WAPENDWA HAWA?
NI NANI ANAYECHUNGUZA KUONA NDUGU ZETU WANA MAHALA PA KUTUA MIZIGO YAO YA MAWAZO?
Ndilo haswa lengo la kuingia kwenye album ya TRUST ME yake Joseph Hill ama Culture ambaye humo tunakutana na wimbo RIVERSIDE.
Katika wimbo huu, Culture anazungumza umuhimu wa kwenda pembeni ya mto na kupata muda wa kutafakari uumbaji wa Mungu na kutua msongo ulio ndani mwetu. Utamsikia akizungumza "And I sat down quietly watch the fishes circle around the little stones.
Lay their burden on the riverside.
I cup my ears and I heard the little birds whistling in the tree like, so lay their burden on the riverside
Jah provides for the birds in the air and the fishes in the sea so what about me.
Lay their burden on the riverside
Look at the crow they toil not neither do they spin yet father provide far them.
Lay their burden on the riverside"
Kwa ujumla ni kuwa kila mmoja ana magumu yake, lakini kila mmoja ana mahala pa kupata unafuu.
Ni wakati wa kuisaka ilipo NAFUU yako ili kukuwezesha kuondoa msongo wa mawazo. Na kwa kufanya hivyo, utakuwa umeisaka na kuipata RIVERSIDE YAKO.
Jiunge na Culture katika kibao hiki kitaaamu cha RIVERSIDE

For I woke on Saturday morning
Feeling sticky and dirty after work
Took a walk down a riverside

I roll a little spliff
Sat down on a stone and start to cool off
With my burden down a riverside

For I check around the youths
And I try to teach the truth
Lay their burden on the riverside

I walk through every corner
Try to find someone to talk to but I have to
Lay their burden on the riverside

For I walk and I talk
And I linger and I search
Lay their burden on the riverside

And I walk, I met the youthman pocket
And I try to search around them
Lay their burden on the riverside

And I sat down quietly
Watch the fishes circle around the little stones
Lay their burden on the riverside

I cup my ears and I heard the little birds
Whistling in the tree like so
Lay their burden on the riverside

Live good among your neighbor
Like sister and brother and
Come with me a riverside

All you need is pray to Jah, quality
You see secret shall be revealed
Lay their burden on the riverside

(solo)

Jah provides for the birds in the air
And the fishes in the sea so what about me
Lay their burden on the riverside

Look at the crow they toil not neither do they spin
Yet father provide far them
Lay their burden on the riverside

Let us walk and talk
And pray quietly in search
Lay their burden on the riverside

Look at the color of those clothes, oh Jah
Make each and every one individually
Lay their burden on the riverside

Where is the love?
Where is the togetherness too?
Lay their burden on the riverside

I can't take the war and I can't take the shooting
Neither the looting, just
Lay their burden on the riverside

I tried around Rema
Even in The Jungle
To find a quiet rest

Round there in a Nannyville
My heart come to a trail
Lay their burden on the riverside

And I knock, and I search
And I whisper and I preach
Lay their burden on the riverside

Where is the quietness
And the love to be found in some corner?
Lay their burden on the riverside

Let us walk, let us search
Let us examine and let us see
Lay their burden on the riverside.


**Them, I & Them ni kipengele kikujiacho kila Ijumaa kinachoelezea kazi za wasanii (Them) kulingana na maono yangu (I) kwa ajili na manufaa ya hadhira (Them)**
Kwa nyimbo zaidi ndani ya kipengele hiki bofya hapa.
IJUMAA NJEMA

Thursday, March 15, 2012

Haki za UTU WETU na uhuru wa UANDISHI WETU


Katika maandalizi ya mkutano wa Diaspora wa mwaka 2010 nchini Uingereza, blogger Issa Michuzi alinukuliwa akisema kuwa "Kwa mahesbu ya haraka haraka hivi sasa kuna blog zinazotumia lugha ya kiswahili zipatazo 200 ambapo pia blog takriban 10 zinaanzishwa kila siku, na kuifanya Tanzania kuw nchi zinazoendelea katika tasnia ya habari kwa njia ya mtandao."
Hayo yalikuwa mahesabu ya mwaka 2010. Sasa hivi blogu ni nyingi saana. Yaani hata sisi bloggers hatujuani. Na wingi wa blogs hizi hauendani na wingi wa mafunzo (japo ya awali) kuhusiana na suala zima la uandishi na maadili yake.
Na hapa linalosemwa si kwamba kila blogger lazima awe mwandishi ama awe na elimu ya uandishi, lakini ninalomaanisha ni kuwa kuna MAADILI ya uandishi ambayo NILAZIMA tuyafuate kama tunajua kuwa kuna jamii inayotutegemea katika kuwahabarisha, kuwaelimisha na kuwakomboa kiakili.
Kwa siku za karibuni kumekuwa na matukio mengi mabaya na ya kutisha nchini Tanzania na mengine yamehusisha mauaji na matendo ya kikatili kwa wanajamii. Licha ya shukrani za dhati kwa wana-blog kwa kuweka wazi matendo hayo, bado narejesha OMBI la kuzingatia MAADILI katika kuweka picha na maelezo.
Ninaloomba ni kuzingatia UTU hata wa Marehemu na pia kuthamini HESHIMA ya marehemu na nduguze.
Kumekuwa pia na shida ya kuweka majina na / hata picha za watoto wenye umri wa chini ya miaka 18.
Ni OMBI katika kuona namna ambavyo tunaweza kuendeleza UTU WETU wakati tukiendelea kutimiza UHURU WA UANDISHI WETU.

Tukingali pamoJAH.
Tuonane NEXT IJAYO

Monday, March 12, 2012

Dr Hamza Mwamoyo katika "Ana kwa Ana ya Vijimambo Blog"

Hivi karibuni, blogger mwenzetu Luke Joe wa VIJIMAMBO alifanya mahojiano na Dr. Hamza Mwamoyo katika utaratibu wake mpya wa kutambulisha wadau mbalimbali waTanzania wanaofanya shughuli mbalimbali hapa Marekani.
Hapa anaeleza mambo mbalimbali kuanzia historia ya maisha yake kwa ufupi alikotoka mpaka hapa alipo, shughuli alizowahi kufanya, ushabiki wake katika soka na taratibu za kufuata kwa wale wanaotaka kujiunga na Idhaa ya Kiswahili ya Sauti ya Amerika (VOA).
Karibu uungane naye

Saturday, March 10, 2012

Mawazo ya sauti (I).....OMBI

Mmoja wa marafiki zangu wa Facebook alileta OMBI kuwa nikusanye yale NIWAZAYO KWA SAUTI na kutoa mkusanyo wa kijitabu. Sikuamini kama nimeshawaza vya kutosha kiasi cha kukusanya "kijitabu". Kisha akasema "basi yakusanye na kuyaweka mahala pamoja ambapo tunaweza kuyarejea kwa pamoja".
Nimeona nifanye hivyo hapa, kwani wapo WASOMAJI WANGU WAPENDWA wasio wanachama ama marafiki zangu kulee facebook.
Na haya yafuatayo ni baadhi ya MAWAZO YANGU YA SAUTI ambayo nimekuwa nikiwaza kwenye status zangu za Facebook.
KARIBU


Ndoto na UFUNUO ni matokeo ya matendo yako. Ukiota na usifuatilie ama usione kikitokea utaita ndoto. Ukiamka na kufuatilia kisha ukafanikiwa utaita UFUNUO. Yawezekana kila UFUNUO ni NDOTO ILIYOFANYIWA KAZI hivyo ushauri wangu ni kuwa UKIOTA KILICHO CHEMA, AMKA, NENDA KATENDEE KAZI. Utaifanya kuwa UFUNUO. Hahahahaaaaaaaaaaaaaaaaaaa.
Nawaza kwa sauti tuuuu!!!!

Furaha ni "akiba" ya sikitiko lijalo na vivyo hivyo ni kinyume chake. Azaliwapo mtoto furahi ukijua kuwa yeye ama wewe utakufa (hapo mtasikitika) mkiamini kuwa (kama mlitenda wema) mtakutana mbinguni (mkifurahi). Ajaye huondoka na pengine huja tena. Tenda wema ili mwisho wa "mzunguko" huu, uwe mwenye furaha.
Nawaza kwa sauti tuuuuuu!!!!

Ni kwanini twaiita BIMA YA MAISHA ilhali hatuwezi kukusanya mafao yake mpaka baada ya kufa? Ni kweli twastahili kuiita "Life insurance"? Ama ni "post-life insurane" au tuwe wazi kuiita "Death Insurance"? Aaaaah!!
Nawaza kwa sauti tuuuuuu!!!!

PARADOKSI YA JAMII YANGU....Leo hii "nyuma ya kisasa" ni ile yenye game room na gym badala ya study room. Mji wa kisasa ni ule wenye clubs na bars nyingi badala ya Maktaba..... Na bado twasema twataka kujenga jamii bora yenye kuthamini elimu.
Nawaza kwa sauti tuuuu!!!!!

UPDATE: Mpango wa kuwapiku waMarekani, Urusi, Japan na wengineo kwenye mambo ya "space" unaendelea vema. Tunapanga kwenda JUANI na tumegundua kuwa ni lazima tutue kule USIKU. Tuna-calculate take-off time ili tu-land USIKU. Kama kuna volunteer awasiliane nami...
Nawaza kwa sauti tuuuuuu!!!

PARADOKSI YA TANZANIA YANGU: Leo hii tuna wanasiasa ambao wanasema kuipiga vita rushwa ni mpaka wawe kwenye uongozi na uongozi huo hawaupati bila kutoa rushwa. Ina maana wanastahili kutoa rudhwa ili waweze kupata nafasi ya kuipinga rushwa. Swali ni kuwa WATAPINGAJE RUSHWA IKIWA NI LAZIMA WAITUMIE KUFIKA NAFASI ZA KUIPINGA?
Nawaza kwa sauti tuuuuuu!!!!!

Tatizo la kumuelimisha mtu anayedhani "ANAKUZIDI AKILI AMA WEREVU" ni kuwa kadri unapomuelimisha jinsi ulivyo sahihi, yeye anazidi kujidhihirisha kuwa hauna akili hata za kutambua kuwa ana akili kukuzidi.
Hapo sasaaa.
Hatakuelewa mpaka umuelimishe na ukimuelimisha anazidi kuona "ujinga" wako.
Gggggggggrrrrrrrrrrrrr!!!!!!!!!!!!
NAWAZA KWA SAUTI TUUUUUU

NAWAZA KUWA kazi ya mwendesha mashtaka si kusaka sababu za mshitakiwa kutenda alivyotenda, bali kumfanya mshitakiwa kuwa mwanzo na mwisho wa tendo /kosa alilotenda. Kwani wakisaka chanzo cha mtu kutenda makosa si wataishia kutomfunga wanayetaka alale jela? Na kumfunga wanayemtuhumu ni "kipimo cha ubora wa kazi zao"
Mmmmmmhhhhhhhhhhhhh!!!!!!
NAWAZA KWA SAUTI TUUU!!!!!!!!!!!!!

Hivi wajua kuwa UEREVU WA WENGINE WAONEKANA AMA KUSIFIKA KUTOKANA NA UJINGA WAO? Yaani wanaonekana kuwa na akili kwa kuwa hawana akili za kuwaza akili. Wanaonekana watiifu kwa kuwa ni wanafiki na wenye kupendwa na wakubwa wa kazi zao kwa kuwa ni wasaliti.
Labda WANA AKILI KWA KUWA HAWANA AKILI.
Ggggggrrrrrrrrrrrr!!!!!!!
Nawaza kwa sauti tuuuuu!!!!

NIMEFUNZWA kuwa HUWEZI KUMSHINDA ADUI YAKO MPAKA UMPENDE.
OK!!!!! Nililoelewa ni kuwa unastahili kumpenda adui ushindanyaye naye, na ukishampenda ina maana hatakuwa adui kwako na akishakuwa MPENDWA KWAKO, hamtashindana kwa nia mbaya, bali MTASHIRIKIANA.
NAKUBALIANA NAYO....... Wewe je?
Nawaza kwa sauti tuuuu....!!!!!!

Mtu anayetaka kuzuia maendeleo ya mwenzake ni yule anayejitahidi kumfanya mwenzie abaki ktk kiwango cha chini. Tatizo ni kuwa ukitaka abaki, itabidi umshikilie pale. Yaani nawe ubaki ambapo unataka usiyempenda abaki. Hivyo, aliyefanikiwa kuzuia maendeleo ya mwenzake ni yule ambaye naye hataendelea akijaribu kumzuia mwenzake. Ina maana afanikiwaye kumzuia mwenzake anakuwa kajizuia na mwenyewe.
Nawaza kwa sauti tuuu!!

Nimefunzwa kuwa KUONGEA NI KAMA MTIHANI. Kabla ya kuanza una maksi zote lkn uanzapo tu waanza jipunguzia ama kuzilinda. Na UJINGA ni vivyo hivyo, haupo kwa yeyote kama wote watakuwa kimya. Ukianza kuongea waonesha kiasi kilichomo ndani mwako.
Kwa maana nyingine HAKUNA MJINGA kama hakuna asemaye.
CHUNGA USEMACHO KWANI WAJIPIMISHA UJINGA / UEREVU WAKO
Nawaza kwa sauti tuuuuuuuuuuuuuuuu

KUIGA ni kama "bahati". Kwamba kuna "bahati nzuri" na "bahati mbaya". Yaani hata anayesema HAIGI, anaiga kutokuiga. Na pengine kutokufanya upende kuiga ni kuiga waliokataa kuiga. Ina maana hakuna asiyeiga japo yawezekana wapenda uigaji wako zaidi ya wa mwenzako.
Kwa kuwa sote twaiga, basi thamini "igo" lako, hakikisha haliathiri wasiolipenda na endelea KUHESHIMU WAIGAO USIYOIGA
Nawaza kwa sauti tuuuuu!!!!

ISOME, IWAZE NA HATA MAONI TOA KIMOYOMOYO.
WanaHistoria wanasema ilichukua miaka milioni kadhaa kwa nyani kugeuka mtu.
Ok!
Sasa kama miaka iliendelea kuongezeka na nyani waliendelea kuwepo, kwanini hatuoni nyani wapya wakigeuka watu kila miaka yao milioni kadhaa itimiapo tangu wawepo?
Nawaza kwa sauti tuuuuuuuuuuuu!!!!!

"Maisha huku hayafai. Nifanyie dili nije huko."
Nauliza "kisichofaa ni kipi hasa?" najibiwa "hakuna dili kabisa. Kila kitu chapanda bei. Huku sio mahala pa kuishi wala kuendesha maisha"
Nauliza "kwanini vinapanda bei?" najibiwa " wazungu na wachina wanakimbilia huku. Viwanja na nyumba za kukodi zinapanda bei? Wanafungua biashara kila mahali"
Nawaza..Kama hawa wanakuja huko, na wewe unasema hakuna dili, wamefata nini?

OK!!
"Wataalamu" wanasema addiction iliyo kuu ni watu kuwa ONLINE kwa muda mrefu. Na wana ushahidi kwa kuwa wamekuwa wakikaa online kuangalia watu wanavyokaa online na sasa wamehakikisha kuwa hilo ni tatizo. Kwanini wao wasijione ma-addicts pia? Siku hizi wezi wanapata pesa kwa kuwasaka wezi, wala rushwa wanawavumbua wala rushwa na addicts wa PC wanasema wanakaa kuchunguza addicts wa PC.
Nawaza kwa sauti tuuuuuu!!!!!

u-CHANYA wa u-HASI wao.
Atunzaye siri apendwa japo afanya hivyo kwa kuwa HAMUAMINI yeyote.
Asiye tegemezi apendwa japo afanya hivyo kwa kuwa HAAMINI kama kuna wa kumfanyia apendayo.
Aliye jasiri apendwa japo afanya hivyo kwa kuwa HAAMINI kama kuna haja ya kutegemea kwingine.
Apendaye apendwa japo afanya hivyo kwa kuwa HAAMINI kama wengine... watambua THAMANI YA UPENDO
TUPENDE U-HASI KWANI NDIO ULETAO U-CHANYA WETU
Nawaza kwa sauti tuuuuu!!!!

MASWALI MENGINE BWANAAA..
Bosi wangu ananiuliza "ni mara ngapi mawazo yako yame-concentrate 100% ktk kazi?" namwambia SIKUMBUKI.
Ati anakasirika na kuuliza KWANINI?
Namwambia "nikiwaza 100% katika kazi, sina % ya ziada kuwaza kuwa nime-concentrate 100% katika kazi. Na nikishawaza hata kwa 0.001% kuhusu concentration yangu ya kazi, ina maana sina 100% kazini."
Akacheka na kuondoka.
NIKAMUULIZA KIMOYOMOYO...UNANITEGA?

NDIO... Kuna JUU.
Na JUU yaweza kutokuwa ile JUU uliyokuwa ukiiota na kuitamani. Na pengine JUU ya "hadhi" sio ile JUU ya "kipato" ama hata ya "utekelezaji"
NA katika JUU hiyo, bado kuna "kati" na "chini".
BASI USHAURI WANGU NI KUWA....
Kama huko JUU hauko JUU, basi shuka CHINI ili uwe JUU....
Hivi naeleweka????
NAWAZA KWA SAUTI TU!!!

NAWAZA faida za "kinyumenyume"
Yaani HUJUI kuwa ulilala mpaka utakapoamka. Usipoamka....meet you in zion
Hujui USAHIHI mpaka utakapoona MAKOSA.
Huoni MAENDELEO mpaka ujue asiyeendelea ama kisichoendelea kilivyo.
Hutoitambua DHAMBI mpaka ujue upande wa pili wa kile uitacho dhambi.
Kwani unaamini HAKUNA FAIDA ya upande uuitao m'baya ambao kwa "kuukimbia" kunakufanya uonekane "mwema" na "mtakatifu"?
NAWAZA KWA SAUTI TUUUUU!!!

MAFANIKIO
Ni kitu cha ajabu na TATA kwelikweli.... Kwa sababu
-Kila mtu hukiomba japo si kila akiombaye anataka kukitumia kwa wema ama lililo jema
-UFANISI wa wengine ambao wanasema WAMEFANIKIWA ktk watendayo kwaikwaza ama kuiadhibu jamii.
-Ili UFANIKIWE kumkamata ALIYEFANIKIWA kufanya yasiyo mema, ni lazima MAFANIKIO yako yazidi MAFANIKIO yake japo wote mwafanikiwa katika mambo yanayopingana.
NAWAZA KWA SAUTI TUUUUUUU!!!

We (human beings) lives in the world of "delayed-now".There is no such a thing called THIS MOMENT because from the moment you think of it to the time you say it, it's not "THIS moment" anymore. May be "that-this moment". Hahahahahahaaaaaaaaaaa
Just THINKING OUT LOUD!!!!!!

CHOO....Labda ni jina tu kulingana na matumizi, kwani kulingana na uhitaji chaweza kuwa chumba na chumba ama sebule kuwa choo.
NAWAZA KWA SAUTI TUUUU!!!!!!

Labda UONGO ni UKWELI usio sahihi kwa wakati usemwao
NAWAZA KWA SAUTI TUUUUU!!!

Thursday, March 8, 2012

Kwenu wanawake, ASANTENI

Tribute to the Women of the World
This is a humble sampling in tribute to some of the great women throughout history ... set to the song, Hero, by Mariah Carey.

Kila mwaka wanawake na walimwengu kote ulimwenguni huadhimisha SIKU YA KIMATAIFA YA WANAWAKE DUNIANI ambayo husherehekewa tarehe 8 Machi.
Mamia ya shughuli na matukio hufanyika ndani ya mwezi mzima wa Machi kusherehekea na kuadhimisha harakati za wanawake duniani katika Uchumi, Siasa na ukombozi wa Jamii ambapo Serikali, Vikundi vya wanawake na mashirika mbalimbali huchagua kauli mbiu kuakisi masuala ya kijinsia katika jamii husika na ulimwengu kwa ujumla.
Kauli mbiu ya mwaka huu kutoka Umoja wa Mataifa ni WAWEZESHE WANAWAKE WA VIJIJI, KUOMESHA UMASKINI.
Maisha yangu yalipitia malezi ya Mama zangu wadogo na Dada zangu. Hawa nao ni sehemu kubwa ya maisha niliyo sasa. Nikiwa mhangaikaji asiyeonekana kuwa na mafanikio ya karibu maishani, waliendelea kunishauri, kunipa moyo na kunisaidia katika kile nilichoamini kuwa ni fanikio langu lijalo. Kwa asilimia kubwa najivunia uwepo wao na kwa kuwa kwa pamoja wote wamekuwa MSAADA MNYOOFU kwangu kwa kuwa na suluhisho lisilohitaji mimi kudhihirisha kitu ili kulifikia. WALIKUWA, WAMEKUWA NA NAAMINI WATAENDELEA KUWA UPANDE WANGU.
Lakini pia nina Dada wadogo ambao nao kwa nafasi waliyokuwa nayo walikuwa chachu saana ya mimi kufanikisha nitakalo. Nakumbuka nikiwa Times Fm kuna wakati ambao "feedback" pekee ambayo ningeipata ni kutoka kwa Kaka na Dada zangu wadogo ambao walijitahidi kunisikiliza kila uchao na kunipongeza ama kunicheka "nilipochemsha" jambo ambalo liliongeza ufanisi kwangu. Kwa hiyo kwa kina Dada Abeella, Byela, Atu, Juliana na wengine (ambao mmeshakuwa Mama Wadogo na mashangazi), nawashukuru, nawapenda na natambua kuwa mmekuwa sehemu kuu ya changamoto zilizonifikisha hapa nilipo.
Kuna Dada zangu wa hiari ambao kiiiila siku nawasiliana nao. Iwe ni kwa kusoma kwenye mitandao yao ama wao kusoma kwangu. Iwe ni kwa kuwasiliana kwenye facebook, messenger, msn ama aina yoyote ya mawasiliani ya kijamii. NAWAPENDA SAANA.
Mmekuwa nguzo muhimu ya kile nionacho kama mafanikio na mmefanikisha kuboreka kwa HIMAYA HII ambayo ni sehemu ya maisha yangu pia. Kwa kina mtabibu wa blog, Dada Subi, Da Yasinta wa Maisha na Mafanikio na Dada "muamshaji" Koero wa Vukani, Da Sophy wa Bambataa, Dada Agnes wa Kiduchu, Da Sarp wa Angalia Bongo, Da Faith wa "Ulimwengu Mdogo", mwanamke wa shoka Da MiJAH, Dadangu Dina wa Marios, Da Edna wa "mchakato wa maisha" (strive for life), Dada Happy Katabazi uwapaye hofu viongozi kwa kalamuyo, Dada Jackline Charles, Dada mpiganaji Judith Wambura, Dada zangu wajasiriamali Marium Yazawa na Shamim wa Zeze, Dada mwenye wito wa mitindo na mavazi Scola wa Passion4fashion, mshairi wa kutazama Upande wa Pili Da Serina, Dada Sophie wa Sophie Club, Da Mary Damian na Da mkubwa Chemi wa Swahili Time. Dada-Rafiki Makrina a.k.a Mama Paul na Da Sarafina Msuya, shukrani kwa uwepo wenu. Dada Annie wa Brizzleleo, Da Maryam, Da Maidama wa TMark, Da Jestina George, Da Jane Siame J2Wisdom, Da Susan wa Karisan Media, Da Mignonne Clara wa Nyumbani Kwetu, Da Rachel Isaac Siwa wa Swahili na Waswahili, Da Rose wa Mbeyela wa Be You na wengine wote.
Kwa kinamama nyooote mliogusa maisha yangu kwa namna yoyote ile, nawapenda na kila siku naona na kudhihirishiwa thamani yenu. Lakini leo kwa kuwa wametenga siku ya kuwaenzi hapa, NAWAOMBEA MAFANIKIO KATIKA KILA JEMA MTENDALO.
Kwa kinamama mlioonesha njia sahihi tangu awali, twawashukuru kwa mwanga mliotuwashia.
Kwa kinamama ambao mnatufunza kuhusu "upande wa pili wa dunia" nanyi pia twashukuru kuwa uwepo wenu watukumbusha kuwa dunia haijajazwa na wale watendao tupendayo tu.
Katika kuadhimisha hili, NAUNGANA NA WANAWAKE, WASICHANA NA WALIMWENGU WOTE KATIKA KUKOMESHA UKATILI DHIDI YA WANAWAKE NA WASICHANA.
Naungana na Lucky Dube pia katika kuwaombea wanawake kwa MUNGU. Nawaacha na kibao chake GOD BLESS THE WOMEN ambacho mashairi yake yako hapo chini. Sikia anavyowaombea na kuwashukuru. Akiwaita HEROES
HESHIMA KWENU KINAMAMA NYOTE

In the middle of the night I heard her pray so bitterly and so softly yeah...
She prayed for her children
She prayed for their education,
Then she prayed for the man that left her with her children.
We, praise heroes everyday
But there are those that we forget To praise
The women of this world.
They do not run from anything
They stand and fight for what's right
They do not run from anything
They stand and fight for what's right


Chorus
Oh oh oh...
God bless the women

Even when times are so hard
They are so cool, calm and collected.
They do not run from anything,
They stand and fight for what is right
They do not run from responsibilities
They stand and fight for what Is right

Chorus till fade...

Tuesday, March 6, 2012

Phanuel Ligate katika "Ana kwa ana ya Vijimambo Blog."

Hivi karibuni, blogger mwenzetu Luke Joe wa VIJIMAMBO alifanya mahojiano na Ndg Phanuel Ligate katika utaratibu wake mpya wa kutambulisha wadau mbalimbali waTanzania wanaofanya shughuli mbalimbali hapa Marekani.
Hapa anaeleza mambo mbalimbali kuanzia historia ya maisha yake mpaka shughuli zake zfanyazo hapa Marekani.
Pia ana ushauri.....
Karibu uungane naye

Mavazi ya Kiafrika. Tujivunie. Tuunge mkono...



Ladies and Gentlemen,

I would like to take this great opportunity to introduce you to my niece, Karungi Mukurasi who has a renown business in Dar for making nguo za wakina mama na mashati ya wakina baba and some very interesting stylish African suits for men.

She is the one in the photos in the attachment.

From the time she was born she showed artistic proficiency and when school was done, she embarked into this voyage which has brought her to the heights of the design of premier African dressing. She gets her materials from West Africa where the best fabrics are woven and has dress-makers to her designs both in West Africa and in Tanzania.

Her dresses have been worn by prominent women in Tanzania and some international circles, as well as some shirts which some Wabunge have found very fashionable as they mingle in public circles.

Just as the advertisement on Mwananchi Newspaper shows (photo above, click to enlarge), these are African dresses with an African style which eclipse what you may see at a Hollywood movie premier or the Oscar's red carpet runway.

Please feel free to contact her for any additional info, specially for you who are abroad and would like to show the international community that African dressing is second to none!

Her email address is: kmukurasi@hotmail.com or k_mukurasi@yahoo.com

We hope to have a website soon!

Thanks,

Ben K.

NB: Duka lipo Kinondoni Road, Kinondoni Muslim, Duka namba 37, jina la duka ni J's JOY. Namba ya simu ni +255 784 95 95 51

The greatness within you

"You may be surrounded by mud but if you are a diamond you are a diamond , you are bound to shine"-Geophrey A. Tenganamba,2011
Life is Greatest Gift of All. The world is the greatest college for a man to learn to live. This world has so many things to believe, to doubt, to confuse, to mistake, to correct, to live right and many others. It is for you to choose what to focus and believe. A Man is what he/she has accepted what to be. Even if his/her life may appear as if there is nothing great from him/her it does not mean that is what he/she was made for. There is greatness within each and every man.

Environment may lie about him/her, some external forces may even tell him/her otherwise but the truth is a man was made to be great. Not what is outside him/her but what is within him/her is a reason of his/her greatness. It is hard to believe this, because of what we have learned from external forces and what we see in our environment. Even if we don’t believe it,
the truth is THERE IS A GREATNESS IN EACH AND EVERY MAN. The way you see your world is the way you are and going to be. If you see inadequate, weakness, inferiority and incompleteness even if you are great within your world will be small, and that will be your price. Even if you are great within you will never experience greatness until y ou accept it as the truth to you.
You live in your own world, and it is optional to accept this truth as well. You are carrying your inner truth yourself, the truth of greatness and infinite possibilities it is optional to accept it as well. YOU ARE A PRODUCT OF A GREAT AND INFINITE GOD, THE ONE WHO DOES NOT CREATE GARBAGE. But if you think that you are garbage you are and if you think you are great you are also right. The world can teach you otherwise, can lie about you but it you who has a choice to tell the world who you are.

I know that many people will be surprised because of what I am doing and what I will do world wide not because I don’t have that ability like Napoleon hill , it is because they think that I am from Tanzania the underdeveloped country, but tell them the truth I am powerful beyond measure and I am the world greatest. You may be surrounded by mud but if you are a diamond you are a diamond and you are bound to shine. Let it be remembered that a diamond in the mud even if It may appear dark because of the dirty mud it is still a diamond and can still shine because it is a diamond not mud. Wherever you are, whatever you are, whoever you are you are still a diamond, there is greatness within you. Also a dirty diamond with mud will remain to be dirty if nothing is done to make it shine .

The world is the world of rules, and never deviates from its rules, whoever want to shine must pay a price of cleaning mud. Whatever you accept as truth to you, you will get results of the truth you have accepted. It is a rule. There is greatness within you and if you don’t believe this it is true for you as well. You must first accept your greatness; perceive it and live it even if you need to go against the direction of the wind. See yourself great to unleash your greatness. For you to see greatness you must first accept and believe that you are, and you must be there to where you believe you are, your heart must be there train your soul to live beyond your surroundings, to live at your greatness and then everything will follow.

You cannot be a star if you do not live there, you cannot be rich if you do not live there, you cannot own a big company if you do not live there, you cannot be executive if you live as donkey in the mud, live there where you want to be. Where you live is where you will be, where you don’t live you do not exist, live where you want to be, then your body will follow. Even if you live in the local places, offices, environment train your soul to live in greatness, in infinite possibilities. You may appear as if you are working with the local commission but you know that you don’t belong there you live beyond, you live global.

REMEMBER THAT YOU ARE A SOUL WITH PHYSICAL BEING NOT PHYSICAL BEING WITH A SOUL. THIS IS GREATNESS.Dont get too busy with mere living and forget your greatness, doing so is like being busy dying. We must be there to our greatness even if we are busy and the world is telling us opposite. To live to our greatness is to live to our true self. We were born to be great, and there is greatness in us but it is optional to prove our greatness as well.

I LOVE YOU ALL. I LOVE TO SEE YOU THERE, TO YOUR GREATNESS. HOPE WE WILL MEET

The Author of this Article is A Young Powerful Motivational Speaker In Tanzania, East Africa author of the powerful books called "Kichwa Chako ni dhahabu", "The Richest Goldmine in You" and "Nguvu ya Kujitajirisha ndani yako.
For more books about this Article and to book this speaker :gtlivemore@gmail.com, +255714477218 or
visit his blog here

The article was introduced to me by Godlisten Shayo of GSHAYO Blog

Thursday, March 1, 2012

Wewe ni ZAIDI YA WEWE

Mimi ni zaidi ya umuonaye pichani. Nawe pia. Isake "nguvu uliyo ndani mwako" utafanikiwa
Maswali ya wewe ni nani yanaweza kuleta mjadala mkubwa na pia kujiuliza kama umefikia kiwango cha juu cha u-wewe nalo laweza kuwa swali gumu. Lakini kuna ukweli kuwa "wewe ni zaidi ya wewe". Niliwahi kuandika kuwa tuko tulivyo kutokana na maisha yetu kutokana na maisha yetu yaliyopita na kwa ajili ya maisha yetu yajayo. Pia Kaka Bwaya na wachambuzi / watambuzi wengine wameandika kuhusu mada zihusianazo na hizi. Kaka Kaluse alishaandika juu changamoto za kufikiri vizuri na hofu ya kesho ilivyo dubwana la kutisha mambo ambayo kwa hakika yanatukwamisha katika kufikiri juu ya uwezekano mwingine wa kujaribu kuwa na maisha zaidi ya haya tuliyonayo.
Lakini ukweli halisi ni kwamba maisha yetu yanakwamiswa na namna tunavyochukulia mafanikio yetu na ama namna tunavyoogopa kusaka mafanikio zaidi ama tunavyoshindwa kuamua kujaribu namna nyingine za mafanikio pale kile tufanyacho kinapogoma. Kuogopa kwetu kujaribu (ambazo ni athari za hofu, fikra mbovu na zenye mtazamo hasi tunazojijengea) ndiko kunakotufanya kushindwa kujipa ama kusaka changamoto zaidi ambazo ni chachu ya ukuaji wa kila mtu. Nakumbuka msemo wa kikwetu usemao "kama hujala nje ya kwenu utaamini kuwa mamako ndiye mpishi bora ulimwenguni" ambao kwa tafsiri ya isiyo rasmi wamaanisha bila kukubali / japo kufikiri na kuangalia changamoto za maisha mengine, kwingine na kwa namna nyingine, utabaki kuamini kuwa umefikika kwenye kilele cha mafanikio yako. Kwa ujumla katika suala lolote, kuna kuona tatizo, kisha kulitambua na baada ya hapo kuangalia kama unataka kupata changamoto na kukua ama unataka kuachana nazo (nikimaanisha kuzikimbia changamoto) na hapo ndipo utakapoamua juu ya kuwa ulivyo, kuporomoka toka ulipo ama kuwa zaidi ya ulivyo.
Ndipo linapokuja suala la UTUMWA WA KIAKILI ambapo mawazo ya "nimeshapitwa na wakati" ama "hizo zi fani zangu" na hata "vina wenyewe" vinapokuja na kujikosesha nafasi muhimu na pengine adimu ya kuwa mtu wa pekee ulimwenguni. Nikimsikiliza Bob Marley anaposema "emancipate yourselves from mental slavery, none but ourselves can free our minds" napata maana halisi ya namna tunavyoweza kuwa zaidi ya sisi kama tutakuwa na fikra chanya juu ya kile tutakacho kutenda.
Kumbuka kila mwenye mafanikio alipitia maanguko mengi na kutokata tamaa ni sifa mojawapo ya shujaa hivyo hatustahili kukata tamaa maana kwa kuendeleza tuaminiyo, tupendayo na tutakayo tutafanikiwa tu. CHANGAMOTO ni sehemu ya maisha na kila uwazapo kitu na kukawa na uwezekano wa mafanikio basi ujue waweza kuwa hapo uwazapo kama utafanya hicho uwazacho kwa njia na mpangilio sahihi.
Ni muda wa kujitazama wewe kama wewe, kuangalia ulipo na kisha kutazama uwezo wako katika utendaji mambo, ndoto zako, na uwezekano wa kuwa zaidi ya ulipo na kisha ujiulize HIVI WEWE SI ZAIDI YA WEWE? Kama ndio basi "fuata ndoto zako"
Labda Luciano atukumbushe kuwa "trade winds will keeps on blowing, my life keeps on going, Jah's Love keeps on flowing. So i never give up my pride".


Jicho la ndani ni kipengele ambacho huangalia mambo kwa "undani" zaidi na kujaribu kutafuta suluhisho kutokana na tafakari ya tatizo. Kwa maandiko mengine kuhusu kipengele hiki, BOFYA HAPA