Showing posts with label Thaminisha. Show all posts
Showing posts with label Thaminisha. Show all posts

Wednesday, May 15, 2013

Thaminisha.......Mr & Mrs Abdallah Kitwara

Photo Credits:  Vijimambo blog
Nawasikia(ga) tu wakisema "nyuma ya mafanikio ya mwanaume, kuna juhudi za mwanamke"
Labda ni kweli..
Lakini pia, kuna UKWELI kuwa huyo MWANAMUME yuko na huyo amuwezeshaye kwa kuwa naye amejitolea mengi kuweza kuwa naye.
Kwa hiyo, nyuma ya mafanikio ya kila mwanaume, kuna juhudi za mwanamke ambaye alichaguliwa, kukubaliwa na / ama kuendelea kuwa na mwanaume aliyenaye.
Labda....NYUMA YA MAFANIKIO YA KILA MTU, YUKO MTU.
Kwanini nimeanza na nukuu hiyo?
Ni kwa kuwa nataka ku THAMINIsha Kaka yangu Abdallah Kitwara na mkewe.
Hawa wamekuwa chachu ya maendeleo ambayo binbafsi NIMESHUHUDIA na pia NINAYAISHI.
Kabla sijatambulishwa kwake na mwenzangu katika kazi (Abou Shatry), nilipata kujua USHIRIKI wake kwenye jamii kwa kuona UDHAMINI wake kwenye timu ya Tanzania DMV
Jezi za timu zilizodhaminiwa na kampuni ya Vizion One Inc inayomilikiwa na Mr & Mrs Kitwara.
Baada ya kumuona katika hili, tuliwasiliana nao kuangalia namna ambavyo wangeweza kuwa na ushirika katika harakati zetu za kukuza mkakati wetu wa kuanza kufanya uzalishaji wa AUDIO na VIDEO kwa matukio yanayotukia hapa Washington DC na vitongoji vyake.
Tulipowasiliana nao, walikuwa wakarimu sana kutualika kwao na kisha WALITUWEZESHA KUPATA VIFAA VYA KISASA NA VYA KUTOSHA KUFANYA KAZI ZETU.
Huu ulikuwa ni zaidi ya msaada.
Hii ilikuwa zaidi ya baraka
Hili ni zaidi ya DENI LA KUSONGA MBELE
Hili walilotenda wapendwa hawa ni zaidi ya ambalo tulitegemea na baada ya kukamilisha manunuzi, tukapata (pamoja na mambo mengine) kamera ya kisasa saana
Mpiga picha mkuu wa Jamii Production Abou Shatry
Ni kwa uwezeshwaji wa wapendwa hawa, tukaweza kuanzisha JAMII PRODUCTION ambayo imejikita katika kuhakikisha inaELIMISHA, BURUDISHA na KUKOMBOA JAMII kwa mahojiano, mijadala na mambo mbalimbali
  
Ukweli ni kuwa, hapa tulipo tusingefika kwa wakati huu bila kuwezeshwa na ndugu hawa wawili.
Na si sisi pekee ambao tunajivunia nafasi yao katika jamii. Bado tumeona udhamini wao katika matukio mbalimbali ya jamii.
Mkurugenzi wa Vizion One, Abdallah Kitwara akimkabidhi Dj Luke cheki ya kusaidia matayarisho ya sherehe ya Blog ya Vijimambo itakayofanyika July 6, 2013 maeneo ya Capitol Heights, Maryland.
 Photo Credits: Vijimambo blog
Nikirejea kwenye mwanzo wa post hii, labda ni kweli kuwa mafanikio ya kila mmoja yametokana na ushirikiano wa kila mmoja wao, na kwa hakika napenda kuwaTHAMINISHA Mr & Mrs Abdallah Kitwara kwa nafasi yao katika jamii.
June 7, 2010 niliandika post hii isemayo UTAKUMBUKWA KWA DESHI YA MAISHA YAKO ambapo kati ya niliyosema ni kuwa "Maisha yana hatua tatu muhimu na mbili kati ya hizo (KUZALIWA na KUFA) hazina mjadala, na moja ambayo ndiyo tusiyoijua, ndiyo muhimu kwetu. Ndio hiyo niitayo "deshi". Na kwa kuwa kila mtu anazipitia mbili nilizozitaja, basi hakuna anayezijali wala kumkumbuka mtu kwazo. Ina maana maisha yetu yamebaki kwenye hiyo hatua iliyo kati ambayo ndiyo tunayoihangaikia..... 
......Leo hii kila aitwaye shujaa ama fisadi ama mshkiliza rekodi, ama mtakatifu ama mkatili ama mwenye cheo chochote ulimwenguni anakumbukwa kwa kile alichofanya kwa muda wake wa "deshi" ambao ni wa katikati ya kuzaliwa na kufa. 
Basi tuchuje vema maisha yetu na kuangalia na kutambua kuwa kwa kila utendalo sasa ndilo lenye kuweka historia yako mbeleni."
UKWELI NI KUWA...
Najivunia namna ambavyo Ndugu zangu hawa wamewezesha maisha ya wengi
Nami nawatakia baraka katika maisha haya ambayo punde mmesherehekea miaka kumi ya ndoa pamoja
Video hii iliyo muhtasari wa sherehe yao kuadhimisha miaka kumi ya ndoa ni kwa hisani ya IskaJoJoPhotography 


Kwangu na kwa jamii ijuayo mema, nyinyi ni HEROs
Na wimbo huu hapa chini, ni maalum kwa ajili yenu

**THAMINISHA ni kipengele kinachounganisha makala ama matoleo mbalimbali ya watu mbalimbali wanaojitolea kuboresha maisha ya wengine na hata wale wanaoona vema kuthaminisha yale waliyotendewa na wengine. Kwa matoleo zaidi BOFYA HAPA**

Sunday, February 24, 2013

Thaminisha.....ABOU SHATRY

Zaidi ya umdhaniavyo..
Mpishi wa mengi asiyepokea "tip" halali kwa kazi zake

Wengi wetu tumekuwa "walaji" wa migahawani / ama tumeshuhudia baadhi ya taratibu za walao migahawani ambapo wahudumu (Waiters / Waitresses) wamekuwa wakipokea "tips" kutokana na huduma nzuri itolewayo mahala hapo.
Na ukweli usiopingika ni kuwa, haijalishi mhudumu ametabasamu kwa kiasi gani, ama ameleta huduma kwa kiasi gani, ama amewapa meza muitakayo ama lolote linaloongeza uwezekano wa "tips" hizo, ukweli wa mambo utabaki kuwa NI LAZIMA CHAKULA MLACHO KIWE KIZURI ILI "TIP" HIYO ITOKE.
Nimeanza na mfano huu kwa kuwa naamini kuwa WAPISHI WENGI (ambao ndio chanzo halisi cha tips hizo) huwa hawaonekani na pengine hawathaminiki katika utoaji wa TIPS hizo.
Nazungumzia TIP kama kiwakilishi cha SHUKRANI na / ama SIFA ambazo watu hupata / kunyimwa kulingana na kile wafanyacho.
Na hili ni (kama vile) jambo la kawaida kwa jamii.
Kuwa na NYOTA WACHACHE japokuwa tunajua fika kuwa kazi iliyofanyika imehusisha wengi, na wakati mwingine wale walioonekana ndio waliofanya kazi zaidi.
Kwani nikikuuliza kuhusu UHURU WA TANZANIA, unajiwa na jina ama majina mangapi?
Lakini unaamini hao uwatajao ama kuwawaza ndio PEKEE waliowezesha UHURU WA TANZANIA?
La hasha..
Nikirejea kwa Kaka-Rafiki Abou Shatry, wengi hawatambui THAMANI YAKE kwa kile waonacho humu na kwingine.
Mbali ya kuwa ni bloga mahiri kupitia blog yake hii ya SWAHILIVILLA lakini pia...
Abou ni zaidi ya blogger mwenzangu.
Ni zaidi ya mshirika katika kazi. 
Zaidi ya Rafiki yangu
Zaidi ya Kaka yangu na zaidi ya mTanzania mwenzangu.
 Amekuwa mtu ambaye katika "level" ya kifamilia, tumeungana zaidi ya maelezo.
Katika "level" ya kazi, tumejuana na kushirikiana zaidi ya maelezo.
Abou amekuwa MPIGAPICHA NA MHARIRI MKUU katika takriban Video zote hizi za Jamii Production na ameshiriki katika utayarishaji mzima wa mchakato wa mahojiano.
Pamoja na "credits" zitokazo mwisho wa mahojiano bado inakuwa ngumu kwa watu kutambua THAMANI ya kazi na zaidi KIPAJI CHA UBUNIFU alichobarikiwa nacho Kaka Abou.
Niweke wazi kuwa, licha ya kupokea pongezi nyingi kwa kazi zetu, lakini MCHAKARIKAJI MKUU wa kusaka, kutekeleza na hata kuboresha kazi za USHIRIKA WETU ni Kaka Abou.
Iwe ni kutengeneza banners (kama hiyo ya Jamii Production  hapa chini ambayo bado naamini kuwa NI "NYEPESI" LAKINI YENYE KILA UZITO UNAOSTAHILI) ama iwe ni kuhariri na kurekebisha na kusambaza video za mahojiano, Abou amekuwa mstari wa mbele katika kuboresha hilo.
"Mkono" wa Abou ndani ya dakika chache za kupata wazo.
Umakini wa kazi yake, umeifanya jamii (inayoangalia videos zetu) kunufaika na kila kitendekacho.
NI MKALI KARIKA KAZI na KILICHO BORA NDILO LENGO LAKE, na mara zote anajua namna muafaka ya kukisaka.
Abou ndiye mkosoaji namba moja wa kazi zetu (weka mbali "better halves" wetu) hivyo kuepuka "lawama" zake ndiyo chachu ya maandalizi zaidi katika mahojiano.
Lakini...
Abou ni zaidi ya mwana Jamii Production.
Ni Mume, ni Baba, ni Mwanajamii na zaidi ya yote muumini mzuri ambaye kwa maisha aishiyo amekuwa mfano kwa wengi.
Ushirikiano wake katika jumuiya mbalimbali hapa DMV umemfanya awe mfano kwa wengi.
Binafsi namchukulia kama nilivyosema hapo awali......
Abou ni zaidi ya blogger mwenzangu.
Ni zaidi ya mshirika katika kazi.
Zaidi ya Rafiki yangu.
Zaidi ya Kaka yangu na zaidi ya mTanzania mwenzangu.

KATIKA KILA UFURAHIALO KWENYE VIDEO ZA JAMII PRODUCTION, TAMBUA KUWA YUPO "MPISHI" AMBAYE MARA NYINGI HAONEKANI.
Naye ni Abou...AMBAYE LEO NAMTHAMINISHA KWA YOTE MEMA ATENDAYO KWENYE JAMII YETU.

Heshima kwako Kaka Abou..Utendalo ni HAZINA KWA JAMII YETU 


**THAMINISHA ni kipengele kinachounganisha makala ama matoleo mbalimbali ya watu mbalimbali wanaojitolea kuboresha maisha ya wengine na hata wale wanaoona vema kuthaminisha yale waliyotendewa na wengine. Kwa matoleo zaidi BOFYA HAPA**

Tuesday, April 10, 2012

Let's "Party for a good cause."

Chama cha Wanawake waTanzania waishio Marekani (Tanzanian Women Association-USA) kwa mara nyingine kitaendesha ukusanyaji wa fedha katika harakati zake za kusaidia sehemu / watu ama makundi mbalimbali yenye uhitaji nchini Tanzania.
Chama hiki kinachoundwa na WANAWAKE WANAHARAKATI WA MAENDELEO kinapanga kuendesha ukusanyaji huu wa fedha kwa kushirikiana na Dj Chick and Friends siku ya Jumamosi (Aprili 14) katika ukumbi wa NECTAR LOUNGE uliopo 7926 Georgia Ave.,Silver Spring, MD 20910. Na kama "bango" hilo lionyeshavyo hapo juu, makusanyo yatapelekwa kusaidia kuboresha maisha ya kinamama na watoto nchini Tanzania.
Hii ni awamu nyingine ya harakati za TWA ambao mwaka 2008 waliendesha harambee (rejea post hii) na kufanikiwa kukusanya kiasi kilichofanikisha kununua na kukabidhi madawati 32 yaliyogharimu takriban shilingi Milioni 1.9 (kama ilivyoripotiwa hapa).
Harakati hizi zinaendana na ushauri huu aliotoa Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa nchi za Marekani na Mexico Mhe. Mwanaidi Maajar kwa wanawake.

Na sasa ni wakati wako wewe mwanaharakati na mwanajamii kuungana na HATAKATI HIZI NJEMA ZA TWA kuwezesha mkakati wa kusaidia kuboresha maisha ya wenye uhitaji.

Vyama ni vingi, JUMUIYA ni nyingi na mahitaji ni mengi, na ni sisi wenyewe tunaohitaji kusimama kidete ili kuboresha mazingira na maisha bora kwa kila mhitaji kwa kujitolea kile tuwezacho katika kufanikisha azma hii. Si lazima kiwe kikubwa, bali tukitoa kwa moyo kitafaa. Kama alivyosema Mother Theresa kuwa "I can do no great things. Only small ones with GREAT LOVE." Nasi tuungane katika kuchangia na kufanikisha kuwaondoa kinamama na watoto katika mazingira haya. Kama TUWA-USA wameweza kusimama katika MALENGO yao kama walivyoeleza HAPA, ni kipi kinachotushinda kuunga mkono harakati hizi?
Licha ya kusaidia kuboresha maisha ya wanawake na watoto nchini na pia kuinua elimu kwa watoto (hasa mabinti) nchini Tanzania, TWA-USA imekuwa ikijitahidi kufanikisha njia za kuwezesha waTanzania walio hapa kujua namna ya kupata elimu bora hapa nchini (BOFYA HAPA)
Unaweza kujua na kujifunza mengi kuhusu TUWA-USA kwa kutembelea tovuti yao HAPA

TUKUTANE NECTAR LOUNGE JUMAMOSI HII.
Let's "Party for a good cause"

Saturday, October 8, 2011

Mpigie kura Dereck Kayongo


Dereck Kayongo, mwenye mradi wa Global Soap Project ni mzawa wa Afrika Mashariki ambaye alianza kukusanya sabuni kwenye hoteli na sehemu nyingine na kisha kuzituma nyumbani Afrika. Mpaka leo hii, mradi wake umewezesha kutoa miche laki moja kwa jamii mbalimbali katika nchi tisa.
Waweza kuSOMA HABARI ZAKE NA KUMPIGIA KURA HAPA.

Sunday, August 28, 2011

Thaminisha...... Dj Luke Joe

Dj Luke Joe alipokuwa akizungumza siku ya uzinduzi wa blog ya Vijimambo.
Maisha ni mchakamchaka. Na kwa nchi za ugenini, yaonekana kuwa mchakamchaka zaidi. Ni ugenini huku ambako wengine hawapati muda wa kuwasiliana, kutembeleana, kupigiana simu na hata kufanya ibada, kwa kuwa WAMEBANWA NA KAZI NA MAISHA.
Labda kuna kweli ndani ya hili, na pengine yawezekana ni fikra zetu zinazotufanya tuamini hilo. Lakini kama wengi wanavyosema, KILE UWAZACHO KINAWEZA KUKUTABIRIA MAISHA YAKO YAJAYO. Kwa maana nyingine, kujipanga na kuamua kutekeleza kitu, unaweza kuona mafanikio ambayo hukuyaona awali. Kama nilivyosema HAPA, MAISHA NI TASWIRA.
Leo katika kipengele hiki cha THAMINISHA, nimeona ni vema kutambua mchango wa DJ Luke Joe wa Blog ya Vijimambo. Nakumbuka katika hotuba hii ya Mhe Balozi Maajar siku ya uzinduzi wa blogu ya Vijimambo alihusia matumizi ya mtandao kwa manufaa ya wanajamii walio ndani na nje ya Washington DC. Hii ilikuwa moja ya CHANGAMOTO ambazo alitoa kwa Dj Luke Joe na wote wenye blogu.
Punde baada ya uzinduzi huo, nilipokuwa katika maongezi ya kawaida na Dj Luke, alisema kuwa anahisi anaanza kupunguza jitihada zake kwenye kupiga muziki na kuwekeza zaidi katika blogu. Na sasa mwaka mmoja baadae, naamini ni wengi wanaoishi maeneo ya Washington DC na vitongoji vyake wanaweza kuamini kuwa Vijimambo imekuwa kama chanzo cha habari na matukio mengi yanayotukia ama kutarajia kutukia eneo hili. Ni kiunganishi chema na MUHAMASISHAJI mwema kwa jamii ya hapa.
Nimesema MUHAMASISHAJI (tena kwa herufi kubwa) kwa kuwa sote tuishio vitongoji vya DC tunatambua namna ambavyo chombo ambacho kilikuwa kikihusika na kutukusanya na kutuhamasisha na hata kutuhabarisha kuhusu Tanzania, uTanzania na waTanzania hapa DC kilivyo kwenye mgogoro. Na kwa kukosekana kwake, hakika ilikuwa kama kundi zima limetawanywa bila mchungaji. Na siku za karibuni, jamii yetu imepatwa na misiba mitatu iliyofuatana, na kutokana na wengi kutokuwa na ratiba inayoruhusu kuwa mahala pa msibani ama mawasiliano ya msibani, blogu ya Vijimambo ilikuwa zaidi ya "makutano" kwetu. Ni hapa tulipojua kilichotokea, kilichokuwa kikiendelea na kwa wale ambao kwa namna moja ama nyingine hawakuweza kuhudhuria, waliweza kushiriki kupitia blogu hii. Tumekuwa tukipata habari (toka msibani ambako Dj Luke amekuwa akishiriki), picha na hata video za matukio mbalimbali.
Narejea katika aya yangu ya kwanza, kwamba MAISHA YA HAPA NI MCHAKAMCHAKA, NA NI KWA UGUMU HUO, KUNA HAJA YA KUTHAMINI MUDA WA DJ LUKE ambaye licha ya kuwa na kazi kama tulivyo wengine wengi, bado anaweza kutenga muda wa ziada kufanya haya yote.
Hii imekuwa CHACHU kwangu, na naamini kwa wengine wengi.
Na ndio maana katika kipengele hiki cha THAMINISHA, tumeona tutoe (japo) TUZO HII YA KAULI kwa Dj Luke, ambaye aliyoyafanya (hasa katika kipindi hiki cha misiba) ilikuwa zaidi ya wajibu wa pamoja wa Ubalozi na Jumuiya yetu. Alikuwa kwenye misiba yote, katika matukio yote muhimu na kutuhabarisha maendeleo yote ya vifo, michango, ibada na hata maziko.
HILI SI LA KUPITA BILA KUTHAMINIWA (labda kama hujui ugumu wa aliyoyafanya).
Kwa Kaka Luke, NATHAMINI SANA MCHANGO WAKO. Najua ugumu wa ratiba za maisha ya hapa, najua ugumu wa ku-blog, na najua ugumu na gharama za kusafiri katika kona zote ulizofanya na kushiriki katika matukio yote uliyoshiriki ili kutujuza yote yanayotokea. Ni kwa kutambua ugumu huo, napenda kusema ASANTE.
Na ndio maana naona ni vema kuweka thamani yako nikianimi kuwa WASOMAO HAPA, NAO WATATHAMINISHA UWAFANYIALO
Wimbo huu hapa chini ni maalum kwa ajili ya yale mema ututendeayo. Kwangu mimi, YOU ARE A HERO.

Do you see the smiles on their faces
after you have done what you do best
do you see satisfaction on their faces
after you have blessed themw ith your gift
you don't think iit's much
but to them it means the world
they wake up in the morning and wish you were there
don't have to lie to gain their trust
you have never won a Nobel prize
they have never seen you on the TV
your little contribution makes their lives a little bit better every day

chorus
You're a hero x8

big it up, big it up for the fireman
big it up, big it upfor the street cleaners
big it up for the man aNd the woman
who take care of abandonded children
big it up, big it up for the grandmothers
who are left to take care of the children
big it up, big it up Wo!!


**THAMINISHA ni kipengele kinachounganisha makala ama matoleo mbalimbali ya watu mbalimbali wanaojitolea kuboresha maisha ya wengine na hata wale wanaoona vema kuthaminisha yale waliyotendewa na wengine. Kwa matoleo zaidi BOFYA HAPA**

Wednesday, May 26, 2010

THAMINISHA........Da Subi wa Nukta 77

Kuna wakati ambao unakosa la kusema kuhusu mtu ama kitu. Na hiyo ni kutokana na ushiriki wa mtu ama watu kwenye jambo ama mambo fulani.
NAOMBA katika kipengele hiki kipya NIMTHAMINISHE DADA SUBI.
Mmoja kati ya wale ambao wamejitolea saaana kujenga, kuboresha na kuhakikisha blog na tovuti zaendana na wakati. Amekuwa "mtoa tip" katika masuala mazima ya teknohama katika suala la NINI CHA KUFANYA na pia NINI CHA KUEPUKA.
Kila siku nimekuwa nikimwambia Dadangu huyu mpenzi kuwa NIMECHOKA KUELEZA NINAVYOTHAMINI MCHANGO WAKE na ninaloomba ni kumthaminisha hapa Mbunifu Da Subi
ASANTE SAANA DADA SUBI NA NAPENDA UJUE KUWA LICHA YA UFUPI AMA UCHACHE WA MANENO HAUMAANISHI KUTOTHAMINIKA KWA UFANYAYO.
Najua huoni tabasamu wala ridhiko nyusoni mwetu kwa yale uyafanyayo. Na pengine ni kwa kuwa watufunza ama kutushirikisha mambo kwa mafungu ama kwa uchache huoni kama ni mengi utupayo. Lakini kwangu binafsi na wale nishirikianao yale uliyonifunza, UFANYAYO NI MUHIMU NA MAKUBWA SAANA KWETU.
Na ndio maana naona ni vema kuweka thamani yako nikianimi kuwa WASOMAO HAPA, NAO WATATHAMINISHA UWAFANYIALO
Wimbo huu hapa chini ni maalum kwa ajili ya yale mema ututendeayo. Kwangu mimi, YOU ARE A HERO.

Do you see the smiles on their faces
after you have done what you do best
do you see satisfaction on their faces
after you have blessed themw ith your gift
you don't think iit's much
but to them it means the world
they wake up in the morning and wish you were there
don't have to lie to gain their trust
you have never won a Nobel prize
they have never seen you on the TV
your little contribution makes their lives a little bit better every day

chorus
You're a hero x8

big it up, big it up for the fireman
big it up, big it upfor the street cleaners
big it up for the man aNd the woman
who take care of abandonded children
big it up, big it up for the grandmothers
who are left to take care of the children
big it up, big it up Wo!!


**THAMINISHA ni kipengele kinachounganisha makala ama matoleo mbalimbali ya watu mbalimbali wanaojitolea kuboresha maisha ya wengine na hata wale wanaoona vema kuthaminisha yale waliyotendewa na wengine. Kwa matoleo zaidi BOFYA HAPA**