Showing posts with label Afya. Show all posts
Showing posts with label Afya. Show all posts

Tuesday, February 10, 2015

Dr. Talib Ali on the TOP Doctors Interviews - Sedation Dentistry

Dr. Talib Ali, a top dentist from Avatar Dental Care in Leesburg, Virginia, discusses the benefits of Sedation Dentistry on the TOP Doctors Interviews which are seen on CNN Headline News, CNBC, FOX News and other networks. Call Avatar Dental Care Today and set your consultation with Dr. Talib Ali at 703-669-8600 or visit http://www.avatardental.com/ or his office at:
Avatar Dental Care
545 G. East Market Street
Leesburg, VA 20176

Sunday, January 11, 2015

HUYU NA YULE......Mahojiano na Dr Talib Ali

Karibu katika kipindi cha HUYU NA YULE ambapo wiki hii tumeongea na Dk Talib Ali
Yeye ni mwanzilishi wa Avatar Dental Care iliyopo Leesburg Virginia.
Ameeleza mengi kuhusu kazi zake na mikakati aliyonayo baadae Pia, ametoa punguzo la 50% kwa waTanzania watakaoenda kutibiwa kwake, pamoja na mpango wa malipo ya awamu kuwezesha watu kumudu gharama hizo
Karibu

Monday, May 20, 2013

Faida za mazoezi ya uvutaji pumzi.......Freddy Macha

Mwandishi Freddy Macha anatathmini zoezi la kichwa na uso -linaloboresha wajihi, haiba, sauti na mishipa muhimu ya fahamu.
UNGANA NAYE HAPA
 

Saturday, May 18, 2013

Unapotafutwa mstari mwembamba kati ya SAYANSI na MISINGI YA UHAI kuwezesha UHAI

Hivi karibuni kumekuwa na harakati za wanasayansi / watafiti kutafuta tiba za magonjwa mbalimbali yanayoonekana kuziathiri jamii. Ukweli ni kuwa, wanalosaka, ni kutafuta namna ya kuweza kurefusha maisha, lakini katika hilo, wanaonekana kukwaza baadhi ya wanaoamini katika DINI Haya ni matoleo ya wiki hii toka kituo cha NPR ambayo yamezungumzia "mafanikio" katika sayansi ambayo yanaonekana kuwa n"anguko" kwa wenye imani.

Wednesday, May 1, 2013

Susan G. Komen Global Race for the Cure 2013


Hello Everyone,
First, I want to thank everyone for participating in last years Global Race for the Cure. Last year we had about 30 registered team members and we raised $1500 in donations. This year the race is on May 11, 2013. Our goal for this years race is to have at least 30 team members and to raise at least $1500 in donations. 
If you want to join Team Tanzania for this years race, you can register online on our team website. The registration fee is $40 for walkers. you can access our team website by clicking or copying and pasting the link below and clicking "Join Team Tanzania":
Http://globalrace.info-komen.org/goto/TeamTanzania2013

Even if you are not able to join us for this years race, you can help us reach our fundraising goal by giving a tax-deductible donation to the team. You can donate by going to the team website and clicking "Donate to this Team."



Please feel free to e-mail me at TeamTanzania2013@gmail.com if you need further information about registering for the race or donating to the team.  

Thank you

Nelleta Kassembe
Team Captain

Saturday, December 1, 2012

Miaka 22 baada ya kifo chake, 31 baada ya kugundulika UKIMWI...

Ujumbe wake unaendelea kupuuzwa, kizazi chazidi kuteketea. Photo: MUSIC UGANDA.COM
"Today it's me tomorrow someone else
It's me and you we've got to stand up and fight
We share a light in the fight against AIDS
Let's come on out, let's stand together and fight AIDS"

Hiki ni kiitikio cha wimbo ALONE AND FRIGHTENED ambao ulibeba jina la albamu iliyozinduliwa rasmi Sept 29, 1989. Hii ilikuwa ni siku 64 kabla Philly Bongoley Lutaaya hajarejea rasmi nchini mwake Uganda (Des 2, 1989) na kufariki dunia siku 13 baadae (Des 15, 1989). Ina maana leo hii ni miaka 22, miezi 11 na siku 15 tangu amefariki, na USIA aliouimba miaka zaidi ya 21 iliyopita bado ndilo PUNGUFU KUU lililopo katika VITA DHIDI YA UKIMWI katika nchi nyingi barani Afrika.
Tuna msemo mzuuri na wa maana nchini mwetu usemao AISIFIAYE MVUA IMEMNYEA, lakini tusilokumbuka ni kuwa si kila aina ya mvua ikunyeayo hukupa nafasi ya pili ya kukauka na kuwa kama ambaye hakuguswa nayo. Kuna masimulizi ambayo huwakuta watu ambao wanatamani wasingekuwa wasimuliaji wa habari ama hali hizo na licha ya juhudi zao za hali na mali katika kuhakikisha hatupitii yale wapitiayo wao, bado twapuuza na matokeo yake ni sisi kuteketea.
Philly Lutaaya (aliyezaliwa 1951) alikuwa msanii wa kwanza mwenye umaarufu / ushawishi kuwa wazi juu ya kukumbwa na maambukizi ya virusi vya ukimwi na kisha kubadili maisha kwa kutumia kipaji alichokuwa nacho na kilichompa umashuhuri, kuweza kuielimisha jamii kuhusu JANGA LA UKIMWI na pia NAMNA ILIYO SAHIHI KWA JAMII KUPAMBANA NA MARADHI HAYO. Photo: MY HERO.COM
Tatizo la kupuuzia suluhisho halisi la matatizo kwa jamii si kitu kigeni. Tunashangazwa saana na jamii ambayo inapenda kufika 10 bila kufikiria moja na mbili. Aliloimba Philly mwaka 1989 kuwa "ni mimi na wewe tunaostahili kusimama na kupigana vita hii" lilikuwa ndilo suluhisho pekee katika kufanikisha hili.
Kwa mtazamo wa "jicho langu la ndani", naamini aliloeleza Philly ni kuwa tunahitaji kuelimishana zaidi kuhusu janga na madhara. Kuhusu ukweli wa maambukizi na namna tunavyoweza kuishi kwa upendo na kwa miaka miingi tukiwa na virusi na si UKIMWI. Kuelimishana namna ya kuwathamini na kutowatenga waathirika na kuwapa nafasi wanayostahili katika kuisaidia jamii yetu kuelimika kuhusu ugonjwa huu.
TATIZO NI SIASA ZINAPOINGIA KATIKA MAISHA YA WANANCHI.
Sasa hivi (kama alivyosema Rais mstaafu wa Marekani Ronald Regan), kila anayetetea suala la utoaji mimba ni yule ambaye mimba yake haikutolewa. Vivyo hivyo katika hili la Ukimwi. Kamati zaundwa, matumizi yapangwa na "miradi" yaanzishwa lakini waathirika wa virusi hivi wanakuwa watu wa mwisho kabisa katika mchakato mzima na wanakuwa katika upande wa kupokea maelekezo na si kupanga utekelezaji utakaowezesha kufanikisha lengo la kuzuia maambukizi.
Ni vipi tunaweza kuwa na watu wasio waathirika wakazungumzia hisia za kuwa muathirika na kupanga mikakati madhubuti ya kusaidia wengine ambao si waathirika kutofikia hisia na maisha wapitiayo wao?
Haishangazi kuwa VITA DHIDI YA UKIMWI NI MIRADI TOSHA kwani kwa asilimia kuwa yahusisha watu ambao hawana uchungu wa kweli na hawajui uhalisia wa uathirika na pia wanachukuliza vita dhidi ya ukimwi kama miradi.
Ufuatao ni ZAIDI YA WIMBO kwa kuwa ni UJUMBE TOSHA wa namna tunavyoweza kutatua tatizo la UKIMWI hapa ULIMWENGUNI.
PUMZIKA KWA AMANI PHILLY BONGOLEY LUTAAYA

Habari zaidi kuhusu Philly, bofya HAPA
SHUKRANI ZA PEKEE KWA KAKA FADHY MTANGA kwa changamoto hii
Out there somewhere
Alone and frightened
Oh the darkness
The days are long
Life in hiding
No more making new contacts
No more loving arms
Thrown around my neck

Take my hand now
I'm tired and lonely
Give me love
Give me hope
Don't desert me
Don't reject me
All I need is love
And understanding

Chorus:
Today it's me
Tomorrow someone else
It's me and you
We've got to stand up and fight
We share a light
In the fight against AIDS
Let's come on out
Let's stand together
And fight AIDS

In times of joy
In times of sorrow
Let's take a stand
And fight until the end
With open arms
Let's stand up
And speak out to the world
We'll save some lives
Save the children of the world

Let's be open
Advise the young ones
A new generation
To protect and love
Hear them singing
Playing nothing
Let's give them everything
In truth and love

Take the message
Cross the frontier
Break the barrier
We'll fight together
The doors are open
We'll lead the struggle
We won't bow down
In defeat we'll fight on

Chorus

Historia ya UKIMWI duniani

Tunapomalizia kuadhimisha SIKU YA UKIMWI DUNIANI, swali ni kwamba ni kweli tunachokiongea chajulikana kwa wengi? Na watatwezaje kutuelewa kama hawatambui Histori ya Ugonjwa huu na ama wanatambua tofauti kidogo na tutambuavyo sisi? Hebu angalia HISTORIA YA UKIMWI na kutambua mengi ambayo twahitaji kujua juu ya hilo.
Ni kutoka mtandao unaojihusisha na masuala ya matibabu wa WebMd.
a

Kutokomeza UKIMWI.....YES WE CAN!!!

Pengine yaweza kuonekana kama ndoto, na pengine yaweza kuonekana kama ni kitu kisichowezekana, lakini kwa hakika ni jambo linalowezekana. NAZUNGUMZIA KUTOKOMEZA UKIMWI NCHINI NA DUNIANI.
Japo ni kitu kiwezekanacho, lakini chahitaji jitihada za ziada.
Twahitaji malengo na pia utekelezaji wa nia.
Twahitaji kubadilika na kuacha kufanya ugonjwa huu kama mradi. Kisha kwa pamoja kuungana na walioathirika katika harakati zao za kuwa wazi. Wakiacha kunyanyapaliwa, wakapendwa, kuheshimika na kukubalika ndani ya jamii, watakuwa wazi zaidi kueleza namna tofauti walizopitia kufikia hali hiyo na kwa kufanya hivyo tutaepusha maambukizi mapya na kurefusha maisha ya wale wenye virusi hivyo. Japo idadi ya vifo vitokanavyo na ugonjwa huu vimeonekana kupungua kwa mwaka 2007 kwa mujibu wa TAKWIMU ZA W.H.O, bado tuna kazi ya ziada kuhakikisha tunawezesha namba ama takwimu hizi kufikia sifuri, yaani kuutokomeza ugonjwa huu.
Na hii ni CHANGAMOTO YETU sote.
Japokuwa kumekuwa na taarifa za awali kuonesha tumaini la kupatikana kwa KINGA na / ama TIBA ya ugonjwa huu, lakini KINGA HALISI NI KUJIEPUSHA NA USAMBAZAJI WA MAAMBUKIZI KWA KADRI YA UWEZO WETU
Kuutokomeza ugonjwa huu wa UKIMWI...... NDIO TWAWEZA
Tumwangalie dada huyu alivyoelezea namna alivyopokea matokeo ya vipimo vyake. Amekuwa muwazi juu ya hali yake, amekuwa mwelimishaji na mwanaharakati mwema kuhusu ugonjwa huu

Video yake kamilifu kuhusu biashara mbaya ya kuuza mwili pale UWANJA WA FISI waweza kuipata kwa kutembelea http://www.hyenasquare.org/
Basi tusikie wasanii nyota wa Uganda wanavyoungana kwenye mapambano haya muhimu juu ya gonjwa hili hatari.
"A little bit LOVE,
A little bit HOPE,
A little bit CAUTIONA IS ALL WE NEED.
A little bit WISER
A little bit SMARTER"


Ama twende CONGO ambako nao pia waliungana na kutoa kibao hiki kuhusu ugonjwa huu wa UKIMWI

KUTOKOMEZA UKIMWI NCHINI NA DUNIANI.....NDIO TWAWEZA

Wednesday, October 24, 2012

"You're what you eat"

Msemo huu tumekuwa tukiusikia sana.
Na pengine umekuwa kama KAWAIDA masikioni mwetu.
KWANINI?
Kwa sababu madhara ya vile tunavyokula hayaonekani ndani ya muda mfupi.
Wanaadamu tumekuwa waoga wa kile kituathiricho sasa na si siku, wiki, miezi ama miwaka kadhaa ijayo, japokuwa pale tunapopata madhara, tunajutia kila tulichotenda katika siku, wiki, miezi na miaka hiyo.
Nirejee kwenye CHAKULA.
Natambua watu wengi hufurahia aina za vyakula wanavyonunua madukani. Kuku wa "kizungu", ng'ombe wa "kisasa" na mengineyo mengi.
LAKINI JE, UNAJUA WANAKOTOKA? UNAJUA WANAVYOKUZWA, KUCHINJWA NA KUTAYARISHWA MPAKA WANAPOKUFIKIA?
Kwa wale wanaoishi maisha yasiyo na vyakula asili, HAKUNA UJANJA, lakini kwa wewe unayeamini kuwa CHA ASILI NI "USHAMBA", FIKIRIA MARA MBILI.
Karibu utazame DOCUMENTARY hii iliyokuwa ikzungumzia UTATA WA MASLAHI KATI YA AFYA NA UBEPARI.

Thursday, March 29, 2012

Inapotafutwa maana mpya ya kifo kukidhi mahitaji ya afya (II)

OKTOBA 6 2008 niliandika makala hii hapa kuhusu TAFSIRI YA KIFO KUOKOA MAISHA YA WENGINE.
Na katika makala hiyo, sehemu yake ilisema

"Madaktari wanatafuta maana mpya ya kifo ama hali ya mtu kutambulika kuwa amekufa itakayowawezesha kusaidia kuokoa maisha mengi kutokana na kutumia baadhi ya viungo muhimu vya "marehemu" hao kabla "havijafa" na kuvipandikiza kwa wagonjwa wenye uhitaji. Jarida la mambo ya afya la New England Journal of Medicine limeeleza namna ambavyo madaktari waliweza kuhamisha moyo wa mtoto ndani ya sekunde 75 tangu athibitishwe kufa kwa maradhi ya moyo.
Je! Kuna uvunjaji wowote wa misingi ya kibinadamu katika hili? Yawezekana kuna ukweli lakini (na hapa naomba kunukuu ili kuweka ujumbe halisi) "......in medicine, lines move. "Dead" means irreversibly stopped, and stoppages are increasingly reversible. And when life support ends, says one bioethicist, "not using viable organs wastes precious life-saving resources" and "costs the lives of other babies." Failure to take body parts looks like lethal negligence". Whaooooooooooooooooooooo!!!!!
Bado hawajamaliza, swali jingine ni vipi tunaweza kupata viungo muhimu vya mwilini punde baada ya mgonjwa kufariki ili kuweza kuokoa maisha ya wengine wengi? (na kwa mara nyingine naomba nisipoteze maana kwa kutafsiri) wao (wataalamu wa kupandikiza viungo) wanasema "..... By redefining death. First we coined "brain death," which let us take organs from people on ventilators. Then we proposed organ retrieval even if non-conscious brain functions persisted. Now we have "donation after cardiac death," the rule applied in Denver, which permits harvesting based on heart, rather than brain, stoppage.
But stoppage is complicated. There's no "moment" of death. Some transplant surgeons wait five minutes after the last heartbeat; others wait two. The Denver team waited 75 seconds, reasoning that no heart is known to have self-restarted after 60 seconds. Why push the envelope? Because every second counts. Mark Boucek, the doctor who led the Denver team, says that waiting even 75 seconds makes organs less useful."" Ifuate makala yote HAPA

Lakini jana tu nimesikia kuhusu HARAKATI MPYA ZA KUTAFSIRI KIFO kwa wale wanaotaka kujitolea viungo vya mwili. Katika MAKALA HAYO ndani ya KIPINDI CHA MORNING EDITION kinachozalishwa na NATIONAL PUBLIC RADIO (NPR), sehemu ya maelezo ya makala hayo yanasema "....... defining "dead" turns out to be pretty complicated. It turns out, there are two ways to declare someone dead. For decades, the main way has been "brain death."

Brain death is defined an "irreversible cessation of all the functions of the brain, including the brain stem," according to James L. Bernat, a Dartmouth Medical School neurologist who is an expert on the science and ethics of organ procurement.

These are often people who have suffered massive strokes or devastating blows to the head.

But transplant advocates have revived another definition in recent years. It's had several names, including "donation after cardiac death (DCD)" and "donation after circulatory death." It says: It's OK if donors initially may still have some brain activity. But in this case, death requires "an irreversible cessation of circulation and heartbeat and breathing and no intervention will be done to restore it," Bernat said. "So it is permanent."

In these cases, no one will perform CPR or anything else to restore circulation on the patient. A typical case might involve someone who has had a massive heart attack. Doctors and families agree there's no hope and decide it's time to discontinue life support."
SIKILIZA MWENYEWE MAKALA NZIMA HAPA AMA CHINI UONE NAMNA AMBAVYO TAFSIRI MPYA YA KIFO INAVYOWEZA KUOKOA MAISHA YA WENGINE.
Unaikubali? Unaipinga? KWANINI?

Thursday, December 1, 2011

Miaka 21 baada ya kifo chake, 30 baada ya kugundulika UKIMWI...

Ujumbe wake unaendelea kupuuzwa, kizazi chazidi kuteketea. Photo: MUSIC UGANDA.COM
"Today it's me tomorrow someone else
It's me and you we've got to stand up and fight
We share a light in the fight against AIDS
Let's come on out, let's stand together and fight AIDS"

Hiki ni kiitikio cha wimbo ALONE AND FRIGHTENED ambao ulibeba jina la albamu iliyozinduliwa rasmi Sept 29, 1989. Hii ilikuwa ni siku 64 kabla Philly Bongoley Lutaaya hajarejea rasmi nchini mwake Uganda (Des 2, 1989) na kufariki dunia siku 13 baadae (Des 15, 1989). Ina maana leo hii ni miaka 21, miezi 11 na siku 15 tangu amefariki, na USIA aliouimba miaka zaidi ya 21 iliyopita bado ndilo PUNGUFU KUU lililopo katika VITA DHIDI YA UKIMWI katika nchi nyingi barani Afrika.
Tuna msemo mzuuri na wa maana nchini mwetu usemao AISIFIAYE MVUA IMEMNYEA, lakini tusilokumbuka ni kuwa si kila aina ya mvua ikunyeayo hukupa nafasi ya pili ya kukauka na kuwa kama ambaye hakuguswa nayo. Kuna masimulizi ambayo huwakuta watu ambao wanatamani wasingekuwa wasimuliaji wa habari ama hali hizo na licha ya juhudi zao za hali na mali katika kuhakikisha hatupitii yale wapitiayo wao, bado twapuuza na matokeo yake ni sisi kuteketea.
Philly Lutaaya (aliyezaliwa 1951) alikuwa msanii wa kwanza mwenye umaarufu / ushawishi kuwa wazi juu ya kukumbwa na maambukizi ya virusi vya ukimwi na kisha kubadili maisha kwa kutumia kipaji alichokuwa nacho na kilichompa umashuhuri, kuweza kuielimisha jamii kuhusu JANGA LA UKIMWI na pia NAMNA ILIYO SAHIHI KWA JAMII KUPAMBANA NA MARADHI HAYO. Photo: MY HERO.COM
Tatizo la kupuuzia suluhisho halisi la matatizo kwa jamii si kitu kigeni. Tunashangazwa saana na jamii ambayo inapenda kufika 10 bila kufikiria moja na mbili. Aliloimba Philly mwaka 1989 kuwa "ni mimi na wewe tunaostahili kusimama na kupigana vita hii" lilikuwa ndilo suluhisho pekee katika kufanikisha hili.
Kwa mtazamo wa "jicho langu la ndani", naamini aliloeleza Philly ni kuwa tunahitaji kuelimishana zaidi kuhusu janga na madhara. Kuhusu ukweli wa maambukizi na namna tunavyoweza kuishi kwa upendo na kwa miaka miingi tukiwa na virusi na si UKIMWI. Kuelimishana namna ya kuwathamini na kutowatenga waathirika na kuwapa nafasi wanayostahili katika kuisaidia jamii yetu kuelimika kuhusu ugonjwa huu.
TATIZO NI SIASA ZINAPOINGIA KATIKA MAISHA YA WANANCHI.
Sasa hivi (kama alivyosema Rais mstaafu wa Marekani Ronald Regan), kila anayetetea suala la utoaji mimba ni yule ambaye mimba yake haikutolewa. Vivyo hivyo katika hili la Ukimwi. Kamati zaundwa, matumizi yapangwa na "miradi" yaanzishwa lakini waathirika wa virusi hivi wanakuwa watu wa mwisho kabisa katika mchakato mzima na wanakuwa katika upande wa kupokea maelekezo na si kupanga utekelezaji utakaowezesha kufanikisha lengo la kuzuia maambukizi.
Ni vipi tunaweza kuwa na watu wasio waathirika wakazungumzia hisia za kuwa muathirika na kupanga mikakati madhubuti ya kusaidia wengine ambao si waathirika kutofikia hisia na maisha wapitiayo wao?
Haishangazi kuwa VITA DHIDI YA UKIMWI NI MIRADI TOSHA kwani kwa asilimia kuwa yahusisha watu ambao hawana uchungu wa kweli na hawajui uhalisia wa uathirika na pia wanachukuliza vita dhidi ya ukimwi kama miradi.
Ufuatao ni ZAIDI YA WIMBO kwa kuwa ni UJUMBE TOSHA wa namna tunavyoweza kutatua tatizo la UKIMWI hapa ULIMWENGUNI.
PUMZIKA KWA AMANI PHILLY BONGOLEY LUTAAYA

Habari zaidi kuhusu Philly, bofya HAPA
SHUKRANI ZA PEKEE KWA KAKA FADHY MTANGA kwa changamoto hii
Out there somewhere
Alone and frightened
Oh the darkness
The days are long
Life in hiding
No more making new contacts
No more loving arms
Thrown around my neck

Take my hand now
I'm tired and lonely
Give me love
Give me hope
Don't desert me
Don't reject me
All I need is love
And understanding

Chorus:
Today it's me
Tomorrow someone else
It's me and you
We've got to stand up and fight
We share a light
In the fight against AIDS
Let's come on out
Let's stand together
And fight AIDS

In times of joy
In times of sorrow
Let's take a stand
And fight until the end
With open arms
Let's stand up
And speak out to the world
We'll save some lives
Save the children of the world

Let's be open
Advise the young ones
A new generation
To protect and love
Hear them singing
Playing nothing
Let's give them everything
In truth and love

Take the message
Cross the frontier
Break the barrier
We'll fight together
The doors are open
We'll lead the struggle
We won't bow down
In defeat we'll fight on

Chorus

Monday, August 15, 2011

Langa azungumzia utumiaji madawa ya kulevya (Audio)

Hii ni audio iliyosikika siku ya Jumapili, Agosti 14, 2011 katika kipindi cha Njia Panda na Dk. Isaac Maro akizungumza na Langa kuhusu utumiaji wa madawa ya kulevya, mapambano aliyomo sasa katika kuyaacha na mipango ya baadaye ya kupambana na matumizi ya dawa za kulevya katika harakati za kuiokoa jamii ya Tanzania.
Audio hii ni kwa hisani ya Dada Subi wa www.wavuti.com
BOFYA HAPA CHINI KUSIKILIZA...

Monday, June 13, 2011

Wednesday, December 1, 2010

Kutokomeza UKIMWI.....YES WE CAN!!!!!

Pengine yaweza kuonekana kama ndoto, na pengine yaweza kuonekana kama ni kitu kisichowezekana, lakini kwa hakika ni jambo linalowezekana. NAZUNGUMZIA KUTOKOMEZA UKIMWI NCHINI NA DUNIANI.
Japo ni kitu kiwezekanacho, lakini chahitaji jitihada za ziada.
Twahitaji malengo na pia utekelezaji wa nia.
Twahitaji kubadilika na kuacha kufanya ugonjwa huu kama mradi. Kisha kwa pamoja kuungana na walioathirika katika harakati zao za kuwa wazi. Wakiacha kunyanyapaliwa, wakapendwa, kuheshimika na kukubalika ndani ya jamii, watakuwa wazi zaidi kueleza namna tofauti walizopitia kufikia hali hiyo na kwa kufanya hivyo tutaepusha maambukizi mapya na kurefusha maisha ya wale wenye virusi hivyo. Japo idadi ya vifo vitokanavyo na ugonjwa huu vimeonekana kupungua kwa mwaka 2007 kwa mujibu wa TAKWIMU ZA W.H.O, bado tuna kazi ya ziada kuhakikisha tunawezesha namba ama takwimu hizi kufikia sifuri, yaani kuutokomeza ugonjwa huu.
Na hii ni CHANGAMOTO YETU sote.
Japokuwa kumekuwa na taarifa za awali kuonesha tumaini la kupatikana kwa KINGA na / ama TIBA ya ugonjwa huu, lakini KINGA HALISI NI KUJIEPUSHA NA USAMBAZAJI WA MAAMBUKIZI KWA KADRI YA UWEZO WETU
Kuutokomeza ugonjwa huu wa UKIMWI...... NDIO TWAWEZA
Tumwangalie dada huyu alivyoelezea namna alivyopokea matokeo ya vipimo vyake. Amekuwa muwazi juu ya hali yake, amekuwa mwelimishaji na mwanaharakati mwema kuhusu ugonjwa huu

Video yake kamilifu kuhusu biashara mbaya ya kuuza mwili pale UWANJA WA FISI waweza kuipata kwa kutembelea http://www.hyenasquare.org/
Basi tusikie wasanii nyota wa Uganda wanavyoungana kwenye mapambano haya muhimu juu ya gonjwa hili hatari.
"A little bit LOVE,
A little bit HOPE,
A little bit CAUTIONA IS ALL WE NEED.
A little bit WISER
A little bit SMARTER"


Ama twende CONGO ambako nao pia waliungana na kutoa kibao hiki kuhusu ugonjwa huu wa UKIMWI

KUTOKOMEZA UKIMWI NCHINI NA DUNIANI.....NDIO TWAWEZA

Monday, August 16, 2010

Si Malaria, si Ukimwi......NI SARATANI

Photo credit:Kick Cancer-Community Campaign
Ugonjwa wa saratani leo umetajwa kuwa unaoongoza kwa kusababisha vifo na pia kuongoza katika gharama za uchumi na hivyo kudidimiza uchumi duniani.
Katika taarifa inayotegemea kutolewa katika Mkutano wa dunia wa kudidimiza saratani utakaofanyika huko China wiki hii, imeelezwa kuwa licha ya SARATANI inagharimu maisha na gharama kuliko UKIMWI, Malaria na magonjwa mengine yaambukizwayo toka mtu mmoja hadi mwingine. Imeelezwa kuwa ugonjwa huu umegharimu takriban asilimia 1.5 ya GDP ya dunia kwa mwaka 2008, sawa na kiasi cha dola bilioni 895.
Shirika la Afya Duniani (WHO) lilitabiri kuhusu uwezekano wa ugonjwa wa saratani kuupiku ule wa moyo kwa kusababisha vifo mwaka huu. Takribani watu milioni 7.6 walikufa kwa saratani mwaka 2008 na zaidi ya watu milioni 12.4 hugundulika kuwa na maradhi hayo kila mwaka
NIWAZALO HAPA ni kuwa
Kwanini tusiwaze ni yapi yasababishayo magonjwa ya saratani?
Je! Maendeleo tunayoyakimbiza na kuyashindania, yana faida kuliko hasara?

Kwa sisi "nchi za mapokeo", tunapima vipi kila kiingiacho KUMLINDA MLAJI na athari za muda mrefu?
Je! Hatuna namna ya kuwianisha maendeleo na hasara ama madhara yatokanayo nayo?

NAWAZA KWA SAUTI TUUU
Waweza soma taarifa kamili kuhusu ripoti hiyo kuhusu saratani, bofya HAPA

Tuesday, May 25, 2010

Ili uokoaji usiwe uuaji katika ajali.....

NIMEKUWA MHANGA WA AJALI NA NIMESHUHUDIA TOKA TUKIONI NAMNA AMBAVYO UOKOAJI WA MAISHA YA MAJERUHI UNAVYOTENDEKA.
Lakini nilipokutana na makala hii ya
Dr Faustine nikaona ni vema kushirikiana nanyi kuweza kupata uelimishaji zaidi.
ENDELEA NA KILE ALICHOSEMA
DR FAUSTINE
Picha toka Maktaba ya Changamoto yetu
....... Ni muhimu sana kukumbuka kinachookoa maisha ya majeruhi si uharaka wa kukimbizwa hospitali bali ni aina ya huduma aliyopata eneo la ajali.
Mara nyingi fikra zetu ni kukimbiza majeruhi hospitali badala ya kutoa huduma ya kwanza pale pale alipo.
Pia uhamishaji/ubebaji wa majeruhi kama ilivyo kwenye picha hizi unaweza kuleta madhara zaidi kuliko kusaidia. Mifupa inaweza kuvunjika, kama mtu alipata madhara ya uti wa mgongo, mtikisiko unaweza kumfanya mtu huyu akapooza kabisa na pia ubebaji usio makini waweza kusababisha kifo.

Mambo muhimu ya kuzingatia katika eneo la ajali kama yafuatayo:

1: Kuhakikisha kuwa mazingira yanaruhusu kuokoa majeruhi. Hakikisha kuwa hakuna mafuta yanayovuja kwenye gari au hatari ya moto kulipuka.
2: Fanya uhakiki wa haraka wa walio hai na wenye kuihitaji msaada. Marehemu haitaji kuokolewa.
3: Kama majeruhi hajabanwa, jaribu sana kumsaidia pale pale alipo bila kumsogeza.
4: Kama majeruhi atahitaji kusogezwa uangalifu mkubwa utumike na kuhahakisha zile sehemu za maumivu zinalindwa vyema.
5: Hakikisha njia ya kupitisha hewa ya majeruhi iko wazi na hakuna kitu kinachoziba.
6: Hakikisha majeruhi anapumua. Kama majeruhi anapata shida kupumua inabidi asaidiwe kufanya hivyo.
7: Hakikisha majeruhi ana mzunguko mzuri wa damu na havuji damu kwa wingi. Kama majeruhi anavuja damu kwa wingi, ni muhimu kujaribu kuzuia uvujaji wa damu. Mara nyingi waweza kutumia sehemu ya vazi la majeruhi au la mwokoaji kufunga sehemu ya juu ya sehemu inayotoka damu kwa wingi au kugandamiza sehemu hiyo kama haijaathirika kwa ajali.
8: Hakikisha sehemu zilizovunjika zinakuwa "stabilised" ilikupunguza maumivu na kupunguza athari zaidi.


** Kwa kumalizia unapotaka kumsaidia majeruhi kumbuka: A: Airway; B: Breathing; C: Circulation.

Baada ya hapo ndio unaweza kufikiria kumpeleka majeruhi hospitali.

Pendekezo:
Kutokana na wingi wa ajali nchini, ni vyema vyombo vya habari vikasaidia kuelimisha jamii kuhusu hatua hizi muhimu zinazotakiwa kuchukuliwa kuwanusuru majeruhi pindi ajali inapotokea.
Majeruhi wengi wanapata madhara zaidi au kufa kutokana na uokoaji usio makini.

Wednesday, April 28, 2010

Miaka 20+ baada ya kifo chake.....

Ujumbe wake unaendelea kupuuzwa, kizazi chazidi kuteketea. Photo: MUSIC UGANDA.COM
"Today it's me tomorrow someone else
It's me and you we've got to stand up and fight
We share a light in the fight against AIDS
Let's come on out, let's stand together and fight AIDS"

Hiki ni kiitikio cha wimbo ALONE AND FRIGHTENED ambao ulibeba jina la albamu iliyozinduliwa rasmi Sept 29, 1989. Hii ilikuwa ni siku 64 kabla Philly Bongoley Lutaaya hajarejea rasmi nchini mwake Uganda (Des 2, 1989) na kufariki dunia siku 13 baadae (Des 15, 1989). Ina maana leo hii ni miaka 20, miezi 4 na siku 13 tangu amefariki na USIA aliouimba miaka zaidi ya 20 iliyopita bado ndilo PUNGUFU KUU lililopo katika VITA DHIDI YA UKIMWI katika nchi nyingi barani Afrika.
Tuna msemo mzuuri na wa maana nchini mwetu usemao AISIFIAYE MVUA IMEMNYEA, lakini tusilokumbuka ni kuwa si kila aina ya mvua ikunyeayo hukupa nafasi ya pili ya kukauka na kuwa kama ambaye hakuguswa nayo. Kuna masimulizi ambayo huwakuta watu ambao wanatamani wasingekuwa wasimuliaji wa habari ama hali hizo na licha ya juhudi zao za hali na mali katika kuhakikisha hatupitii yale wapitiayo wao, bado twapuuza na matokeo yake ni sisi kuteketea.
Philly Lutaaya (aliyezaliwa 1951) alikuwa msanii wa kwanza mwenye umaarufu / ushawishi kuwa wazi juu ya kukumbwa na maambukizi ya virusi vya ukimwi na kisha kubadili maisha kwa kutumia kipaji alichokuwa nacho na kilichompa umashuhuri, kuweza kuielimisha jamii kuhusu JANGA LA UKIMWI na pia NAMNA ILIYO SAHIHI KWA JAMII KUPAMBANA NA MARADHI HAYO. Photo: MY HERO.COM
Tatizo la kupuuzia suluhisho halisi la matatizo kwa jamii si kitu kigeni. Tunashangazwa saana na jamii ambayo inapenda kufika 10 bila kufikiria moja na mbili. Aliloimba Philly mwaka 1989 kuwa "ni mimi na wewe tunaostahili kusimama na kupigana vita hii" lilikuwa ndilo suluhisho pekee katika kufanikisha hili.
Kwa mtazamo wa "jicho langu la ndani", naamini aliloeleza Philly ni kuwa tunahitaji kuelimishana zaidi kuhusu janga na madhara. Kuhusu ukweli wa maambukizi na namna tunavyoweza kuishi kwa upendo na kwa miaka miingi tukiwa na virusi na si UKIMWI. Kuelimishana namna ya kuwathamini na kutowatenga waathirika na kuwapa nafasi wanayostahili katika kuisaidia jamii yetu kuelimika kuhusu ugonjwa huu.
TATIZO NI SIASA ZINAPOINGIA KATIKA MAISHA YA WANANCHI.
Sasa hivi (kama alivyosema Rais mstaafu wa Marekani Ronald Regan), kila anayetetea suala la utoaji mimba ni yule ambaye mimba yake haikutolewa. Vivyo hivyo katika hili la Ukimwi. Kamati zaundwa, matumizi yapangwa na "miradi" yaanzishwa lakini waathirika wa virusi hivi wanakuwa watu wa mwisho kabisa katika mchakato mzima na wanakuwa katika upande wa kupokea maelekezo na si kupanga utekelezaji utakaowezesha kufanikisha lengo la kuzuia maambukizi.
Ni vipi tunaweza kuwa na watu wasio waathirika wakazungumzia hisia za kuwa muathirika na kupanga mikakati madhubuti ya kusaidia wengine ambao si waathirika kutofikia hisia na maisha wapitiayo wao?
Haishangazi kuwa VITA DHIDI YA UKIMWI NI MIRADI TOSHA kwani kwa asilimia kuwa yahusisha watu ambao hawana uchungu wa kweli na hawajui uhalisia wa uathirika na pia wanachukuliza vita dhidi ya ukimwi kama miradi.
Ufuatao ni ZAIDI YA WIMBO kwa kuwa ni UJUMBE TOSHA wa namna tunavyoweza kutatua tatizo la UKIMWI hapa ULIMWENGUNI.
PUMZIKA KWA AMANI PHILLY BONGOLEY LUTAAYA

Habari zaidi kuhusu Philly, bofya HAPA
SHUKRANI ZA PEKEE KWA KAKA FADHY MTANGA kwa Changamoto hii
Out there somewhere
Alone and frightened
Oh the darkness
The days are long
Life in hiding
No more making new contacts
No more loving arms
Thrown around my neck

Take my hand now
I'm tired and lonely
Give me love
Give me hope
Don't desert me
Don't reject me
All I need is love
And understanding

Chorus:
Today it's me
Tomorrow someone else
It's me and you
We've got to stand up and fight
We share a light
In the fight against AIDS
Let's come on out
Let's stand together
And fight AIDS

In times of joy
In times of sorrow
Let's take a stand
And fight until the end
With open arms
Let's stand up
And speak out to the world
We'll save some lives
Save the children of the world

Let's be open
Advise the young ones
A new generation
To protect and love
Hear them singing
Playing nothing
Let's give them everything
In truth and love

Take the message
Cross the frontier
Break the barrier
We'll fight together
The doors are open
We'll lead the struggle
We won't bow down
In defeat we'll fight on

Chorus

Tuesday, December 1, 2009

Kutokomeza UKIMWI...........YES WE CAN!!!


Pengine yaweza kuonekana kama ndoto, na pengine yaweza kuonekana kama ni kitu kisichowezekana, lakini kwa hakika ni jambo linalowezekana. NAZUNGUMZIA KUTOKOMEZA UKIMWI NCHINI NA DUNIANI.
Japo ni kitu kiwezekanacho, lakini chahitaji jitihada za ziada. Twahidaji malengo na pia utekelezaji wa nia. Twahitaji kubadilika na kuacha kufanya ugonjwa huu kama mradi. Kisha kwa pamoja kuungana na walioathirika katika harakati zao za kuwa wazi. Wakiacha kunyanyapaliwa, wakapendwa, kuheshimika na kukubalika ndani ya jamii, watakuwa wazi zaidi kueleza namna tofauti walizopitia kufikia hali hiyo na kwa kufanya hivyo tutaepusha maambukizi mapya na kurefusha maisha ya wale wenye virusi hivyo. Japo idadi ya vifo vitokanavyo na ugonjwa huu vimeonekana kupungua kwa mwaka 2007 kwa mujibu wa TAKWIMU ZA W.H.O, bado tuna kazi ya ziada kuhakikisha tunawezesha namba ama takwimu hizi kufikia sifuri, yaani kuutokomeza ugonjwa huu.
Na hii ni CHANGAMOTO YETU sote.
Kuutokomeza ugonjwa huu wa UKIMWI...... NDIO TWAWEZA
Tumwangalie dada huyu alivyoelezea namna alivyopokea matokeo ya vipimo vyake. Amekuwa muwazi juu ya hali yake, amekuwa mwelimishaji na mwanaharakati mwema kuhusu ugonjwa huu



Video yake kamilifu kuhusu biashara mbaya ya kuuza mwili pale UWANJA WA FISI waweza kuipata kwa kutembelea http://www.hyenasquare.org/
Basi tusikie wasanii nyota wa Uganda wanavyoungana kwenye mapambano haya muhimu juu ya gonjwa hili hatari.
"A little bit LOVE,
A little bit HOPE
A little bit CAUTIONA IS ALL WE NEED
A little bit WISER
A little bit SMARTER"


Ama twende CONGO ambako nao pia waliungana na kutoa kibao hiki kuhusu ugonjwa huu wa UKIMWI

Wednesday, July 29, 2009

MSAADA

Nimeona OMBI HILI LA MSAADA kwenye
Blogu ya Kaka Maduhu nami nimeona niungane naye kusaidia kufikisha ujumbe huu.
Habari yote ni kutoka blog ya Maduhu kama alivyoiandika.


Sala Abdallah Matewa akiwa kitandani eneo la Mtawala Manispaa ya Morogoro wakati akiongea na blog BLOG YA MTANGAZAJI juu ya kuomba msaada kwa wasamalia wema ili kuweza kupatiwa matibabu
Fatuma Abdallah Matewa akiwa amenyanyua mguu wa mdogo wake Sala Abdallah Matewa(19)wakati akiwaonyesha jinsi ulivyoharibika na kuomba msaada kwa wasamalia wema wa kutibiwa.

BINTI Sala Abdallah, Matewa (pichani) mkazi wa eneo la Mtawala katika Manispaa ya Morogoro anaomba msaada wa kitabibu ili kuweza kupatiwa huduma ya kukatwa miguu yake yote miwili baada ya kupata ulemavu wa miguu hivyo kulala kitandani kwa miaka nane bila kufanya shughuli yoyote za uzalishaji mali na kukosa kupata elimu ya msingi.
Akizungumza na blog hii nyumbani kwao Mtawala mjini hapa wakati akijielezea juu ya historia yake ya kupatwa na ulemavu huo, Sala Matewa, alisema huku akiwa amekaa kitandani kuwa kabla ya kupatwa na hali hiyo hakuwa na ulemavu wa aina hiyo bali aliupata mara baada ya kuvunjika mguu wake wa kushoto mwaka 2002 na kupelekwa katika hospitali ya Rufaa ya mkoa wa Morogoro ambapo alitibiwa na kufungwa P.O.P na baada ya kupatiwa matibabu aliruhusiwa na kurudishwa nyumbani kujiuguza.
Sala alisema baada ya kupata matibabu hayo siku ya tatu mguu huo ulivimba sana na kwamba kutokana na hali hiyo ililazimika kurudishwa tena hospitali ya Rufaa ya mkoa huo na kulazwa katika wadi namba tatu ili ufanyiwe uchunguzi zaidi kuweza kupaini tatizo linalomsibu.
“nikiwa nimelazwa katika wadi hiyo kwa miezi mitano nilipatwa na mshangao kwa sababu nyama za mguu wangu zilianza kulika kidogo kidogo huku mifupa na mishipa ya mguu wangu huo ukianza kuonekana kama vile nimechunwa ngozi ” alisema Sala.
Aidha alisema kuwa hali ambayo iliwashangaza sana madaktari ambao walikuwa wakinitibu hospitalini hapo hata hivyo hakuweza kuwakumbuka majina yao na kwamba walilazimika kumpeleka katika chumba cha upasuaji a na walimchuna ngozi ya mguu huo kwa ajili ya uchunguzi zaidi ili kuweza kubaini chanzo cha tatizo hilo jipya la kulika kwa ngozi na nyama za mguu.
Pia Sara alisema pamoja na jitihada zote hizo za madaktari wa Hospitali hiyo ya mkoa wa Morogoro za kumpima vipimo vyote na kumfanyia uchunguzi wa kina juu ya tatizo lake lakini tatizo bado halikugundulika na hali ya mguu wake ukizidi kuwa mbaya madaktari walilazimika kushauriana na baba yake mzazi Mzee Abdalah Matewe ili mgonjwa wake arudishwe nyumbani.
Alisema baada ya kurududishwa nyumbani,alijaribu kutumia Tiba za asili ambazo hata hivyo, hazikufanikiwa, badala yake mguu mwingine wa kulia, ulivimba, baadaye ulipasuka na kumsababishia vidonda vikubwa na kwamba,tangu hali hiyo itokee, ni kipindi cha miaka Nane sasa, yuko kitandani, hajawahi kutembea wala kutoka nje kwa vile, hawezi kutembea tena kutokana na miguu yake yote miwili kupatwa na ulemavu wa kudumu.
Ukiangalia miguu yangu ilivyo panda pinda na kukonda naona kama miguu hii imekuwa ni mzigo na kero kubwa kwangu kwa vile haiwezi kurudi tena katika hali ya kawaida imeisha na imeharibika na imekufa kabisa ni heri ikatwe ili niondokane na mzigo huu kwa majonzi na katika hali ya kukata tamaa huku akionyesha miguu yake hiyo. Alisema Binti huyu.
Kutokana na uzito wa tatizo hilo dada yake mkubwa, Fatuma Matewa, akizungumzia juu ya hali ya mdogo wake alisema familia yao imekaa na kufikia maamuzi ya kuwaomba wasamalia wema ikiwemo serikali na wadau wengine kumpatia msaada wowote utakao muwezesha kupelekwa kwa wataalamu wa viungo vya binadamu ili kungalia uwezekano wa kumsaidia ndugu yao kupatiwa msaada huo wa matibabu na kama itashindikana ni heri akatwe miguu yake yote miwili na kuepukana na tatizo hilo linalomkabili kwa muda mrefu sasa.
Aidha Fatuma Matewa amewaomba viongozi wa serikali, viongozi wa vyama vya siasa na viongozi wa kidini na mtu yeyote atakayeguswa kuswa na tatizo hilo kumtembelea mahali anapoishi mtaa wa Mtawala ili kuangalia hali halisi ya uzito wa tatizo lake na mazingira anayoishi.Pia waweza kutoa mchango wa mawazo,mapendekezo ama mali kwa ajili ya kumsaidia
Waweza kuwasiliana na blog ya Mtangazaji (Ya Kaka Maduhu) kwa email ya maduhu@gmail.com ama kwa simu namba +255 713 309 314

Asante sana kwa kujali

Saturday, July 25, 2009

Ni DHAMBI, HARAMU, HATARI ama ni siasa katika hili?

 

Miaka nenda rudi tumekuwa tukisikia kila aina ya maelezo kuhusu ubaya wa matumizi ya Bangi. Lakini wakati huohuo kukawa na ubishi wa kama yasemwayo kuhusu Bangi yana ukweli ama ni siasa nyuma ya matumizi yake. Wapo wanaosema ni DHAMBI kuvuta bangi, wengine wanasema ina athari kubwa za kimatibabu na wapo waliosema kuwa ni kwa kuwa hakukuwa na mbinu nzuri za kuilipisha kodi, ndio maana ikawa inapingwa.
Sikuwahi kujiuliza undani wa hayo mpaka wa majuzi nilipoona tangazo la Tv la kuonesha kuwa kuhalalisha bangi California yaweza kuwa suluhisho la mapungufu ya pesa ambayo jimbo hilo linakabiliwa nayo. Lakini wapo wanaounga mkono kuhalalishwa kwa matumizi ya mmea huu wakieleza kuhusu utunzaji wa mazingira utakaotokana na majani yake ambayo yanaweza kuokoa maelfu ta miti kukatwa kutengeneza karatas.
Naishia kujiuliza kuwa kwanini sasa yaonekana kuna uwezekano wa kuhalalisha kile ambacho miaka yote tumeambiwa kuwa ni kibaya?
Natamani wataalamu wa afya (kama Dada Subi, Dk Faustine na wengine) wangesaidia kuelimisha hili kwani sasa yaonekana maduka ya dawa zitokanazo na bangi yanazidi kuongezeka kwa kasi na kuzidi kuwavutia wengi kuwa hakuna madhara katika kutumia hili na hadi kufikia jana ( July 24) yasemekana kumekuwa na maduka haya mengi kuliko migahawa kama Mc Donald, Seven Eleven na mingine mikubwa katika sehemu za jimbo a California.

Older Posts Home