Showing posts with label Music. Show all posts
Showing posts with label Music. Show all posts

Saturday, August 7, 2010

Mdundiko.... Ngoma yenye timbwilitimbwili nyingiiii

Photo:Busaramusic.org
Photo: Angalia Bongo
Kwa sisi tuliokulia "kijijini" Dar Es Salaam tunalitambua hili. Mdundiko. Ngoma ambayo kwa hakika ilitufanya wengi kukumbana na mengi.
Mdundiko ulikuwa ukikusanya watu wengi na tukienda mwendo mrefu na katikati ukikusanya watu ambao kwa kuwa wanaongezeka "nje" ya ulipo wewe, unajikuta uko katikati na kama ndio mtoto basi hata namna ya kujisogeza pembeni huwezi.
Na humo katikati unasuguliwa na majasho na vikwapa vya watu na mpaka ngoma inazimwa, unarejea nyumbani (kama hutapotea) ukiwa una harufu itayomfanya mzazi atake maelezo ya kina juu ya utokako. Maana unakuwa unanuka kama zizi. Watu mamia, vikwapa vina "kwalite" tofauti ya kuachia harufu na wengine kuoga ni aleji kwao. Yaani ni mshikemshike tu
Kibaya zaidi ni kuwa TULISHAKATAZWA kuufuata maana watoto wanapotea saana lakini mara zote tukiuona tunajiaminisha kuwa tutaucheza kwa dk chache then tutarudi. Ukija shituka, unafika home wakati wanakula dinner.
Na sheria ya nyumbani ni kuwa kama giza limelazimisha taa ziwashwe, ina maana hustahili kuwa nje
SI BAKORA HIZOOOOOOOOOO
Na kwa wengine hii ikasababisha mengine mengi. Wapo wanaopata wanaowataka (wapenzi wapya) na wapo wanaoachwa kwa kufuata yasiyotakwa.
Kibaya zaidi, wapo waliokuwa wanatelekeza nyumba zao na matokeo yake kundi jingine "linalojiajiri" kuufuata mdundiko dakika chache "wanasafisha" nyumba za watu bila kipingamizi. Maana Mama na wana wote wamekimbilia ngomani
Msikilize George Kanuti Njogopa akikupa uhondo wa kinachoendelea katika mdundiko kwa kubofya hapa chini

Alaaaaaaaaaaaaaaaaa!! Kumbe hakumalizia? Basi fuatilia habari kamili na maelezo katika makala hii tamu na ya kusisimua kwa ku BOFYA HAPA

Wednesday, March 3, 2010

Production or "forgeaction"? Bongo Flava "production" in scandal again..

Hey wats up everybody!! I thought the Producers in Tanzania have improved a lot but i guess i was wrong!!, 2 and Half years ago i made a beat and named it Block Running, I sold it to one of the Label called Koch Entertainment of New York for the agreement of wherever this beat goes my name gotta be there as a beat maker of this beat, 2 days ago i was shocked when one of my friends from Tanzania sent me a song with the same beat i made 2 and half yrs ago!!, and I didnt hear my name on the track all i heard is Marco Chali, So i called Koch entertainment to ask wats going on, Koch entertainment management were so surprised to hear that news so they told me to send the song to them and I did, They asked me if i ever sent the beat to MJ Records of Dar es Salaam, Tanzania. I told em i never did but i put the beat on I tunes so people can buy and use for promotions and not for any type of business but Mj records used the beat without permission from Koch Entertainment and also they didnt follow the agreement we signed that wherever this beat goes my name gotta be there as a beat maker. I dont have any rights of complaining this issue to MJ Records that why my name wasnt on the song as a beat maker all ill do is to take Koch Entertainment to court and they will deal with the MJ Records. The only thing im gonna deal with,if MJ records bought this beat from itunes,and if they did why they used it for the Business!!?.
I put the song which Producer Marco Chali of MJ Records produced last year and my beat i made 2 and half years ago so you guys can compare and tell me if this beat is the same or not the same.

Thanks.
Stiggo Ibrahim,
S&S Records-NY

Thursday, February 18, 2010

Natamani kuona ........

Nikiwa mpenzi mkubwa wa muziki wa kiTanzania, NATAMANI KUONA kitu ambacho kitakuwa kikitoa mjumuisho wa muziki huo na KUENZI KAZI NA WASANII wa muziki wa Dansi nchini.
Natamani kuona SIKU YA DANSI NCHINI ambayo bendi zitajumuika kuimba nyimbo za wasanii mbalimbali waliochangia kwa kiasi kikuuubwa kuufanya muziki wa Tanzania kuheshimika. Waliotumika kuelimisha, kuburudisha na pia kukamilisha harakati mbalimbali katika jamii.
Natamani kuona tamasha litakalowaenzi nyota wengi wanaoendelea kutuelimisha kwa miaka nenda rudi na pia waliotangulia mbele ya haki kama kina Marijani Rajabu, M'baraka Mwinshehe, Hemed Maneti, Lovy Longomba, Eddy Sheggy, Kalala Mbwembwe, Agrey Ndumbalo, Fred Benjamin, Adam Bakari, Jerry Nashon, Kyanga Songa, Moshi William, Seleman Mbwembwe, Othman Momba, Joseph Maina, Abel Baltazar, Seleman Mwanyiro na wengine wengi.
Najua ni wengi nawe msomaji waweza kumbusha ambao ungependa kuona wakienziwa kwa kazi zao wawe hai ama wametangulia mbele ya haki.
Natamani kuona TAMASHA LA KILA MWAKA likionesha thamani halisi kwa wale ambao hawakuendekeza URAHISI WA KAZI bali umuhimu na ubora wake.

Natamani kuona......natamani saaaaana
Kwa wale mliotangulia mbele ya haki, mpumzike vema huko mlipo. Kazi zenu zingali zaelimisha na kuburudisha

Saturday, October 10, 2009

Nimeipenda hii... Kisha nikajiuliza ni lini ntaona waTz Pamoja?

Sipendi kuiona "waTanzania Pamoja" kwa kuwa waKenya wametoa, bali kwa kuwa ni kitu cha maana na manufaa kufanya. Si kwa manufaa ya wanamuziki tu (ambao wanapata mengi si kwa kufanya kazi ya pamoja bali kwa kuonesha ushirikiano) lakini kwa jamii nzima ambayo itathamini zaidi UMOJA NA USHIRIKIANO WA WASANII. Nimependa zaidi intro ya mtoto aliposema "People should LOVE EACH OTHER because we were created in GOD's OWN IMAGE and we should RESPECT EACH OTHER all times.....EVERYONE IS IMPORTANT. TUPENDANE ILI TUISHI"

Lakini pia niwasikilizishe hii ya Waganda kuhusu Africa na kisha tuone kama hii yaweza kuwa CHANGAMOTO kwa waTanzania kufanya hili

TUPENDANE

JUMAMOSI NJEMA

Saturday, August 15, 2009

FFU wa Ngoma Africa katika Makamuzi ya hatari! AFRILU Festival!

FFU wa Ngoma Africa band! wakiwa katika makamuzi ya hatari hatari! kwenye onyesho la AFRILU Festival mijin Ludwigshafen,Ujerumani, ambako onyesho hilo la ijumaa ,liliwatia kiwewe washabiki na kukubali kuwa "Bongo Dansi" la FFU wa Ngoma Africa ni virungu vya kimataifa
Wasikilize hapa http://www.myspace.com/thengomaafrica

Habari na picha kwa hisani ya Msemakweli.

Thursday, July 30, 2009

Luciano na Tanzania

Jana nimemsoma Da'Yasinta na uTANZANIA wake anaojivunia (msome hapa) . Nikafurahia saana. Katika maoni kama kawaida nikamsoma Kaka Kamala aliyeleta CHANGAMOTO nyingine akiuliza "tanzania nini na mtanzania ni nani?" na hilo likanifanya nirejeshe mawazo kwa wale ambao wanajua wanatokea Afrika lakini hawana hakika na watokeako. Hivi wana pa kupenda ama wataipenda Afrika kwa ujumla wake? Lakini kuna mengi ndani ya Afrika ya kumfanya mtu asiyelazimika kuipenda aipende? Vita, Ubadhirifu, Ufisadi ama? Tarehe 7 Aprili nilikumbuka saana nyumbani kisha nikaandika kuhusu siku nitakayorejea nyumbani (Bofya hapa kuisoma post hiyo). Nilijiuliza kuhusu nyumbani kisha "nikasindikiza" toleo hilo na wimbo wake Luciano uitwao When Will I Be Home (Bofya hapa kuusikiliza) ambao pia (kwa mshangao wangu nilipousikia mara ya kwanza) unaitaja TANZANIA kama nchi anayojiuliza kama ndiko iliko asili yake ama la.
Nakumbuka mwanzo wa miaka ya 2000, Kaka-Rafiki Gotta Irie aliniandikia mail kunieleza kuwa alikuwa na mpango wa kumualika Luciano kwenda kufanya onesho nyumbani. Nilifurahi kusikia hivyo kwa kuwa mimi ni msikilizaji na mpenzi wa muziki wa Luciano, na aliporejea toka huko (katika onesho ambalo niliambiwa kuwa lilifana licha ya mahudhurio kuingiliana na matukio ya kidini), lakini hata aliporejea toka huko, Luciano ameendelea kuizungumzia Tanzani ana anasema katika kukaa nchini na kutembea alijifunza mengi na kisha akaandika wimbo wa Remember When ambao kama aelezavyo kwenye mahojiano haya yajayo, alipata wazo hili akiwa Tanzania. Nikajiuliza MAPENZI aliyonayo kwa nchi ambayo inazidi kumong'onywa na wabadhirifu na namna anavyojitahidi kuielimisha jamii juu ya uzuri wa Tanzania nikaguswa saaaana. Luciano ni msanii nimpendaye (wacha nikiri) na haipiti siku bila kumsikia.
Msikilize hapa katika mahojiano (ANZA DAKIKA YA 2 NA SEKUNDE 31) umsikie hisia zake kuhusu Tanzania na Africa kwa ujumla


Blessings

Wednesday, July 15, 2009

Ndiko yalikoanzia?????

Nilipoandika kuhusu kifo cha Michael Jackson, Kaka Kamala aliniomba kama ningeweza kupata habari kuhusu kujibadili kwake na kushirikiana nanyi.
Pamoja na kusubiri matokeo ya mwisho ya vipimo vya kitaalamu kuhusu kifo cha Michael Jackson, bado kifo chake kinahusishwa zaidi na madawa ya kupunguza maumivu ambayo alionekana kuyatumia kwa muda mrefu na kuwa addicted nayo. Ni hakika kuwa sasa wapo wanaoamini kuwa uchunguzi unaoendelea sasa ni kujua nani alimpa madawa hayo, alistahili kupewa madawa hayo na ni kwa kiwango na usimamizi gani alikuwa akiyatumia kwani wapo wanaosema kuwa walionya juu ya matumizi ya madawa hayo.
Lakini pia zipo habari kuhusu mwanzo wa matumizi ya madawa hayo na hata kichocheo kingine cha kubadilika kwa ngozi yake. Na hiyo inasemekana ilitokana na kuungua wakati akitengeneza tangazo la Pepsi kama inavyooneshwa katika video hii iliyotoka punde.
Yasemekana baada ya kuungua alianza kutumia madawa makali ya kupunguza maumivu na pengine ndio mwanzo wa matumizi mabaya ya madawa hayo. Na wapo wahusishao hili na mabadiliko yake ya muonekano wa ngozi. Tukio lenyewe la kuungua ni hili hapa kama lilivyotolewa na US Weekly

Saturday, July 11, 2009

Ngoma Africa band kukiwasha cha moto ! Fest Afrika, Finland 18 Julai 2009

The Ngoma Africa Band aka FFU ! watatumbiza mjini Tampere,Finland katika onyesho la aina yake Fest-Afrika! litakalo fanyika siku Jumamosi 18 Julai 2009,katika sehemu ijulikayo kama Klub, mjini Tampere,Finland.
Kiongozi wa bendi Ebrahim Makunja aka Ras Makunja atakiongoza kikosi chake kuelekea mjini Tampere,Ufini kwa ajiri ya kuwapa burudani ya asiye na mwana abebe jiwe! washabiki wa Ufini,ambao ngoma africa imewapa cheo washabiki hao kuwa ndio wahajili wao huko ufini!.
Bendi hiyo mashuhuri kwa kuwatia kiwewe washabiki barani ulaya imeshawahi kutumbuiza huko ufini mwanzoni mwa februari mwaka huu 2009 nyakati za msimu wa baridi na kutoana jasho na washabiki! wameitwa tena kwa kazi moja tu ya kutoa burudani ya kukata na mundu.
Wadau wa Ufini na scandinavia kwa ujumla chereko chereko na mwenye mwana!
watumishi wenu The Ngoma Africa Band wanakuja kuwapa burudani
wasikilize hapa www.myspace.com/thengomaafrica ukiwataka ngoma4u@googlemail.com

Monday, July 6, 2009

Kibao kumuenzi M.J

Wasanii The Game, Chris Brown, Diddy, Wayna Morris wa Boyz II Men na Polow Da Don wameungana kwa pamoja kutoa kibao kumuenzi Mfalme wa Pop duniani Michael Jackson ambacho wamekiita "Better On The Other Side." Wimbo ulirekodiwa na "kuachiwa" tarehe 26 ya mwezi uliopita ikiwa ni siku moja tangu kufariki kwa Michael.
Tazama kibao hicho hapa chini

Wednesday, July 1, 2009

Wasanii wetu wanajipoteza katika harakati za kujitafuta

Adolph Mbinga, Sister V (Much Respect to you Sis) Mimi na Rogert Hegga baada ya mahojiano 100.5 Times Fm 2002
Labda tafsiri ya mafanikio ndio kizingiti cha kuwepo kwa makubaliano ya nani anafanya nini ili kiwe nini.
Yaani wakati fulani mtu anafanya afanyalo na kuonekana anazidi kujipoteza, lakini kwa mtazamo wake, kile atendacho na mahala alipo ama anapoelekea vyaweza kuwa tafsiri njema ya mafanikio.
Kwa muziki wa nyumbani Tanzania tumeshuhudia HAMAHAMA za wasanii ambazo zinawafanya kuwika katika wiki ama miezi ya mwanzo ya bendi zao mpya wakiwa na nyimbo mpya (ambazo mara nyingi ni vijembe vya walikotoka) na kisha wakikaa muda mchache wanafifia. Na hakuna ambaye ameendelea kuhamahama na kuendelea kukua kimuziki. Asilimia kubwa ya wasanii hawa (kwa namna nionavyo mimi) wanazidi kujipoteza katika kutafuta ilipo sehemu yao.
Lakini pia mbali na kuhama bendi, wasanii hawa wanajipoteza wanapokimbia kueleza ukweli wa maisha ama visa vilivyo katika jamii na kuendekeza majungu na kuimbana ambapo baada ya muda nyimbo zao huwa hazina mvuto kwa kuwa (pengine) kisa kilichoimbwa hakivuti hisia za watu.
Hakuna ubishi kuwa kuhamahama kwa wasanii kama Mwinjuma Muumini, Ali Choki, Banza Stone, Hussein Jumbe, Waziri Sonyo, Mhina Panduka, Amina Ngaluma, Badi Bakule na wengine niliowasahau waliokuwa wakitamba miaka kadhaa iliyopita kumewashushia uwezo kwa kuwa kila waendapo wanakutana na umiliki mpya, uongozi mpya, mazingira na masharti mapya na kazi mpya.
Pengine wakitulia na kutuliza vichwa kutunga yahusuyo jamii zaidi kutakuwa na manufaa kwa jamii husika badala ya kuendeleza mabishano na majungu ambayo "yanaua" uwezo wao kikazi.
Mfano halisi ni wasanii kama Mwinjuma Muumini "Kocha wa Dunia" aliyetamba na vibao kama Mgumba I & II, Kilio cha Yatima, Maisha Kitendawili, ama Rogert Hegga "Katapila" aliyetunga Fadhila kwa Wazazi I & II, ama Adolph Mbinga na hata Banzastone ambao baadhi ya vibao vyao vilizungumzia maisha halisi ya jamii (hata kama uandishi wao ulitokana na matukio yaliyowakumba wao) na tukashuhudia wakiijingiza kwenye vijembe na mabishano yanayowapa umaarufu wa wiki kadhaa kisha wanapotea. Hakuna ubishi kuwa kati ya nyota wote niliowataja hapo, hakuna anayetamba tena baada ya kubadili mtazamo wa tungo zao na kufuata washabiki badala ya WITO wao kwa jamii. Wanasahau lililosemwa na Cyril Connolly aliyesema "Better to write for yourself and have no public, than to write for the public and have no self."
Sikiliza nyimbo hizi FADHILA KWA WAZAZI toka kwao Mchinga Sound na MGUMBA II toka kwa Double M Sound uone ubunifu na uadilifu uliotumika katika tungo upangiliaji wa ala za muziki na viitikio, vitu ambavyo sasa vimepotea licha ya washiriki karibu wote katika nyimbo hizi kuendelea na muziki.
Ni mtazamo tu katika muziki

Sunday, June 28, 2009

Ngoma Afrika Band kutumbuiza AFRIKA FESTIVAL,Goeppingen City,Germany

The Ngoma Africa Band aka FFU!na mdundo wao wa "Bongo Dansi" wanatarajiwa kutingisha jukwaa lingine katika onyesho kubwa la Afrika Festival litakalo fanyika mjini Goeppingen,Ujerumani siku ya jumamosi ya 4 Julai 2009 saa 2.00 Usiku.
Bendi hiyo maarufu na dansi lake linalowatia kiwewe washabiki huko ughaibuni, wanasubiliwa kwa hamu na washabiki katika onyesho hilo.
Wasikilize hapa www.myspace.com/thengomaafrica pia unaweza kuwasiliana kwa kupitia.
ngoma4u@googlemail.com

Thursday, June 25, 2009

Sasa ni taarifa rasmi.

MICHAEL JACKSON kafariki
Hatimaye imekuwa rasmi kuwa yule gwiji wa muziki wa Pop ulimwenguni MICHAEL JACKSON amefariki dunia saa tisa na robo kwa saa za Marekani ya magharibi.
Aliripotiwa kuwa na tatizo la moyo kusimama kufanya kazi (Cardiac Arrest) na kisha kupelekwa hospitali. Hata hivyo afya yake imekuwa ikiripotiwa kuzorota miezi ya karibuni na yasemekana alikuwa na uzito mdogo kuliko umbo lake (takribani 100lbs) na pia kukabiliana na msongo wa mawazo (Stress) kutokana na matatizo yake ya kisheria, kimapato na kifamilia na wapo wanaoamini kuwa kifo chake kimechangiwa na matatizo haya.
Mpaka anafariki, Michael Jackson alikuwa akishikilia rekodi ya kuuza nakala nyingi zaidi katika wimbo Thriller ambao video yake ilivuma kote ulimwenguni.
Mwaka 1985, Michael Jackson akishirikiana na Lionel Richie, waliandika wimbo wa WE ARE THE WORLD ulioimbwa na kundi la UNITED SUPPORT OF ARTIST FOR AFRICA (U.S.A for Africa). Tazama video yake ukifuatilia mashairi yake pia

There comes a time when we heed a certain call (Lionel Richie)
When the world must come together as one (Lionel Richie & Stevie Wonder)
There are people dying (Stevie Wonder)
Oh, and it's time to lend a hand to life (Paul Simon)
The greatest gift of all (Paul Simon/Kenny Rogers)

We can't go on pretending day by day (Kenny Rogers)
That someone, somewhere will soon make a change (James Ingram)
We're all a part of God's great big family (Tina Turner)
And the truth (Billy Joel)
You know love is all we need (Tina Turner/Billy Joel)

(CHORUS)
We are the world, we are the children
We are the ones who make a brighter day so let's start giving (Michael Jackson)
There's a choice we're making we're saving our own lives (Diana Ross)
It's true we'll make a better day just you and me (Michael Jackson/Diana Ross)

Well, send 'em you your heart so they know that someone cares (Dionne Warwick)
And their lives will be stronger and free (Dionne Warwick/Willie Nelson)
As God has shown us by turning stone to bread (Willie Nelson)
And so we all must lend a helping hand (Al Jarreau)

(REPEAT CHORUS)
We are the world, we are the children (Bruce Springsteen)
We are the ones who make a brighter day so let's start giving (Kenny Loggins)
Oh There's a choice we're making we're saving our own lives (Steve Perry)
It's true we'll make a better day just you and me (Daryl Hall)

When you're down and out there seems no hope at all (Michael Jackson)
But if you just believe there's no way we can fall (Huey Lewis)
Well, well, well, let's realize that a change can only come (Cyndi Lauper)
When we (Kim Carnes)
stand together as one (Kim Carnes/Cyndi Lauper/Huey Lewis)

(REPEAT CHORUS AND FADE) (Everyone)


Moja ya picha inayosemekana kuwa kati ya picha za mwisho kabisa zikimuonesha Michael Jackson akikimbizwa hospitali yapatikana HAPA

Tuesday, June 9, 2009

Ali Kiba ndani ya DC Metro

Leo nilikuwa napitia habari mbalimbali pamoja na sehemu za maonesho ya burudani ambako mara nyingi huwa napata ratiba za wanamuziki wa Reggae watembeleao miji ya karibu na DC na ambao mara nyingi huwa wanaanza kujipanga kwa maonesho nyakati hizi. Katika pitapita yangu nikakutana na tangazo la onesho lake Ali Kiba ambalo litafanyika ukumbi wa Zanzibar On The Waterfront

Nilifarijika saana kuona msanii huyu ameweza kufikia hatua ya kuandaliwa onesho mahala hapo ambapo pia wasanii wengi wenye kuheshimika hasa katika muziki wa kiafrika hufanya maonesho yao hapo. Nakumbuka onesho la mwisho mimi kuhudhuria hapo lilikuwa ni lake Oliver "Tuku" Mtukudzi ambaye sihitaji kumuwekea maelezo.
Nikaona ni vema kuwakumbusha wale wapenzi wa Ali Kiba kuwa atakuwa katika ukumbi mkubwa zaidi ya zile ambazo kina "anonymous" wamekuwa wakiziita kumbi za Birthday.
Lakini pia nikawiwa kuwakumbusha wahudhuriaji kuwa hawaendi kumuona Ali Kiba akitumbuiza na wao kumtolea macho, wajitahidi kushirikiana naye katika kucheza. Mimi kama msanii (japo wa "level" ya chini) najisikia vibaya nionapo msanii anatumbuiza na ni yeye pekee anayewajibika ilhali wengine wamemtumbulia macho.
Tazama onesho la Ali Kiba lililofanyika hapa DC ambalo asilimia kubwa ya wahudhuriaji wahudhuriaji walikuwa wakimuangalia kama hawamjui ama hawam-feel ama hawaelewi kiimbwacho wakati naamini wimbo ulioimbwa ni kati ya nyimbo zake maarufu.

Jamani JICHANGANYENI NA MCHEZE NAYE BASIII MKIENDA HAPO Zanzibar O.T.W

Monday, June 8, 2009

The Ngoma Africa Band ndani ya Masala Festival,Hannover,Ujerumani

Bendi maarufu ya mziki wa dansi barani ulaya "The Ngoma Africa Band" yenye maskani yake mjini Oldenburg,Ujerumani.wataupeleka mzimu wa dansi katika jukwaa kubwa la maonyesho la Masala Festival,mjini Hannover,Ujerumani siku ya jumapili ya 14-Juni-2009 .
Bendi hiyo yenye tabia ya kupelekana mchaka mchaka na washabiki wa mziki ughaibuni inatarajiwa kutumbuiza majira ya saa 10.00 alasiri,ambako washabiki wa nyimbo za kiswahili na mziki wa dansi wanaisubiri kwa hamu bendi hiyo, iliyofanikiwa kujizolea umaarufu kwa kutumia mdundo wa dansi wa bongo.
Kiongozi wa bendi hiyo Ebrahim Makunja aka Ras Makunja ataliongoza kundi hilo jukwaani kwa kazi moja tu nayo ni kuwadatisha akili washabiki! Wasikilize kwa kubofya www.myspace.com/thengomaafrica ama waweza kuwasiliana nao kwa barua pepe kupitia anwani ngoma4u@googlemail.com. Kujua mengi kuhusu kundi hili mahiri, bofya hapa
http://www.africa-news.eu/news/entertainment/the-ngoma-africa-band-continues-to-thrill-fans.html

Source: Msema Kweli

Saturday, January 3, 2009

CHANGAMOTO YETU SANAANI

Kundi zima la Tuku lilikuwa ni mpiga ngoma, mpiga tumba + chekeche, mpiga gitaa la besi, yeye na gitaa kiongozi, mpiga marimba na marimba nyingine (kama ya kigogo hivi). Muziki wao... bofya hapo chini usikie.

Kwa muda sasa nimekuwa nikizungumzia na kuandika juu ya sanaa yetu na hususani Muziki. Na mara zote nimekuwa nikizungumzia muziki ambao utatutambulisha hata nje ya nchi. Muziki ambao hata kama mtu hatajua unatoka Tanzania lakini akiambiwa hatosita kuelewa hivyo. Ni hilo ambalo linapotea sasa. Tunapoteza dira na muelekeo kwenye muziki kwa kile kinachoonekana kama utandawazi. "Tunatayarisha" miziki kwa gharama na uwezo mdogo kuliko maelezo. SABABU? Niliwahi kuwauliza baadhi ya wasanii sababu wanazodhani zakwamisha ukuaji wa muziki wetu (wakati nikishiriki vipindi vya sanaa pale 100.5 Times Fm) na baadhi yao bila aibu wakanijibu kuwa ni Lugha (wakimaanisha Kiswahili kinatukwamisha). Nikajiuliza majina ya wasanii wa Afrika wenye heshima ya sanaa hii Ulimwenguni nikakuta wengi wao hawatumii Kiingereza. Hapa sitaacha kumtaja nguli Oliver Mtukudzi ambaye napenda kazi zake na nilishangazwa na kikosi chake anachotumia kutoa burudani hiyo. ni wachache na zana zao ni za kiasili zaidi.
Inasikitisha saana unapoona sifa na uwezo wa baadhi ya ma-producer wa muziki wa "kizazi kipya" nyumbani. Yaani ukijua kupiga kinanda na gitaa kisha ukajua matumizi ya softwares, basi ushakuwa producer. Well!! hilo pekee si tatizo, ila kutojua nani wa kumshirikisha katika muziki gani ili aweke ala gani ilete ladha gani ndio tatizo kuu hapa. Kuna wasanii wengi saana wanaofanya vema kwenye miziki ya asili na ambao kama wangeshirikishwa wangeweza kuupa muziki wetu mtazamo mpya, lakini kwa "u-mimi" uliopo katika "productions" zetu nahisi tunatafuta maendeleo kwa kujichimbia chini zaidi.
Nilijifunza mengi saana kuhusu uchanganyaji wa muziki wa asili na huu "mpya" kwa muda niliokuwa najihusisha na muziki wa ki-Afrika na ulionifanya niwe natembelea studio za Njenje pale Ilala ambapo kwa msaada wa watayarishaji Kepi, Samwel, na wengine nilijifunza mengi na kuanzia hapo niliuona upungufu wa muziki wetu kwa "jicho la ziada" na naamini hii itakuwa changamoto kwa "watayarishaji" wengi wa nyumbani kuangalia watakalo kufanya kabla hawajatamani kuwa kwenye orodha ya wamiliki wa studios. Ni mwaka mpya na changamoto mpya kwenu ni kuukuza muziki badala ya kutegemea muziki kuwakuza. Studio nyingi lakini ubora uko chini kuliko maelezo. Na bado kila siku "waimbaji" wajiitao wasanii wanasema "wamekuja kutushika na kutaka kuteka soko la kimataifa" kwa miziki isiyo na ubora.
Tukitaka na kuamua tutaweza na hii ni Changamoto Yetu sanaani

Msikilize TUKU katika moja ya nyimbo zinazompa heshima saana Ulimwenguni. Kaimba kikwao na katumia zana halisi za kikwao. Wimbo unaitwa Ndakuvara

Naomba niongeze huu Tapindwa Nei kuonesha muziki wa asili uliotulia unogavyo. Muziki mwanana, tempo ya kufikirisha, maandalizi mazuri na unaweza kuuhisi ndani mwako

Sunday, December 7, 2008

Ras Nas ndani ya Dokkhuset, Trondheim, Norway

Ras Nas
Mwanamuziki mkongwe wa miondoko ya muziki wa Dansi na Reggae, Nasibu a.k.a Ras Nas, yuko tayari kufanya vitu vyake katika jiji la Trondheim, Norway, usiku wa Ijumaa tarehe 12 Desemba. Kwa mujibu wa Ashley ambaye ni Meneja Uhusiano wa Kongoi Productions, katika onesho hilo linalotazamiwa kuwa ONESHO LA MWAKA, Ras Nas ametayarisha kikosi kikali chenye wanamuziki toka Congo Brazzaville, Ivory Coast na Sweden. Kwa tahadhari, asiye na mwana itabidi aelekee jiwe! Shoo itaanza saa nne na nusu usiku. Kabla ya hapo DJ Roar Lund atakuwepo uwanjani kufyeka msitu.

Kwa maelezo zaidi Bofya Hapa (kiinglish)
NYOTE MWAKARIBISHWA

Thursday, November 13, 2008

ISHIKE Radio part 10 from Dona Productions


ISHIKE Radio part 10 is uploaded and it has tons of New TZ/KE music.
Click the link http://www.djdona.com/mp3/DJ%20Dona%20ISHIKE%20RADIO%20Part%2010%20(YES%20WE%20CAN%20EDITION).mp3

Tracklisting
1. Intro
2. AY Feat P Square - Freeze
3. STL (Stella Mwangi) - Dreamer
4. Wahu feat Bobby Wine - Little things you do
5. Nonini Feat lady Bee- Kumbuka
6. K-Nel Feat Ben - ISHIKE RADIO Freestyle
7. Ngwair - Nipe Deal
8. Mejja, Mad Traxx, Jimwat - Mezesha
9. Chid Benz- King Kong
10. Big Pin feat Collo - Kadem
11. Bebe Cool Feat Gasuza- Sexy Thing
12. Mwasiti and Chid Benz - Haoo
13. Mad Traxx Feat Wyre- Serious
14. Fid Q Feat AY - Shimo Limetema
15. Kleptomaniax- Magnetic
16. Langa Feat Chidi Benz - Ninaposimama
17. Kaya - Fire Fire
18. Cloud Tissa Feat Nameless - Physically Fit
19. J Sha 4 - Play
20. Afande Sele- Heshima
21. Inspector Harun - Ndoa Haina Doa
22. Shena Feat Z-Anto - Fursa
23. Black Rhyno - Black Chata
24. Bombaa Clan - Does U R Mother Know
25. Blu 3 - Together
26. Kleptomaniacs Feat Ulopa - Psycho
27. Skool Fizz - Huku Majuu
28. Prezzo Feat Taz - Tupendane
29. Matonya feat FID Q - Taxi Babu
30. Ray C Ft Chidi Benz-Nihurumie
31. UB Feat Mr Lenny - Pesa
32. P-Square - Game Over
33. Grace - Anfuukula
34. Noorah - Mapenzi Sinema
35. Hydro - Swing That Back
36. Jua Cali featuring Mejja, Alahola, Rady, Ru, K-Solja and Linda
37. Alfayo - Physical
38. Bella - Faasi
39. G-Flow - Pepeta
40. Outro

Wednesday, November 12, 2008

Hatuwathamini kwa kuwa hatuwajui. Kwanini?

"Everyman must know their past, so we can stand firm in the future" Na haya yalisemwa na Morgan Heritage walipoimba juu ya KNOW YOUR PAST katika albamu yao ya More Teaching. Ni haya tunayokosa katika kujitambua ambayo "yanapelekea" kutotambua mlingano wa tulipo na tutokako. Na huu ni ukweli.
Hivi sasa inapofika Ijumaa, mimi na wenzangu wapenda "za kale" ama wengine wanaziita "zilipendwa" tunajimwaga ukurasa huu wa BONGO CELEBRITY kupata burudani hiyo. Ukiingia kwenye sehemu ya maoni utaona watu wanauliza hivi aliyeimba huo ni nani? Aliwahi kupigia bendi gani na wengine kutoa majina na miaka isiyo na hakika. Inasikitisha kuwa wasanii wetu NGULI ambao wamesaidia kuielimisha jamii, kuiburudisha na hata kutimiza matakwa ya viongozi kwa kuwakusanyia hadhira wanapojiandaa kuhutubia ama kukamilisha azma zao kama za Gezaulole wanasahaulika kwa kuwa tu wahusika hawafanyi wanalotakiwa. MASWALI NILIYONAYO
HIVI CHAMA CHA MUZIKI WA DANSI TANZANIA (CHAMUDATA) wako wapi kushindwa kuandaa, kutunza na kuenzi taarifa za wanamuziki wa Dansi nchini?
Kweli leo hii watu wanakosa habari, historia na hata kazi za wasanii walioiweka Tanzania kwenye ramani ya muziki barani kwetu? Leo hii tunakosa kuwajua kina Marijani Rajabu, Balisidya, Mbaraka Mwinshehe, Moshi William, Eddie Sheggy, Adam Bakari, Hemdi Maneti, Ndala Kasheba, Selemani Mwanyiro, Abeli Baltazar na wengine kwa kuwa tu hakuna pa kupata kumbukumbu zao?
Kweli kazi na maisha ya hawa wasanii mahiri yanapauka na kupotea kwa kuwa tu hakuna pa kupata kumbukumbu zao?
Kwanini Chamudata wasiwe na tovuti ya kueleza maisha ya wasanii WOTE wenye uanachama?
Nitasema ukweli kuwa wasanii waliojenga msingi wa sanaa nchini hawaheshimiki na kujulikana kwa kuwa wahusika hawafanyi wanalotakiwa kufanya.
Ni jambo la kusikitisha kuona wasanii wetu wamefanya kazi kuubwa sana wakati wa maisha na wapo wanoendelea kufanya hivyo, lakini HATUWATHAMINI KWA KUWA HATUWAJUI. Na swali ni Kwenini?
Huu ni MTAZAMO WA CHANGAMOTO YETU KWETU na ndivyo namna nionavyo tatizo. Labda ndilo tatizo.

Saturday, October 18, 2008

Remembering Philips Lucky Dube.


Lucky katika onesho lake la Aug 25, 2007 Crossroads Entertainment Complex Bladensburg MD
Lucky na Back Up singers tar 25 Aug 2007 Crossroads Complex

Nilipomaliza kuangalia show yake usiku wa tarehe 25 Agosti 2007, niliwaeleza rafiki zangu kuwa sitakosa show ya Lucky Dube bila sababu ya msingi. Sababu ya kusema hivyo ni namna nilivyojivunia na kuvutiwa na onesho zima la Lucky. Kuanzia matumizi ya muda, ala, jukwaa (akiwa pamoja na back up singers wake) na hata uvaaji wao na namna alivyoiimbisha hadhira na kuifanya kuwa kitu kimoja japo ulikuwa ni mchanganyiko wa watu wa asili na imani tofauti.
Lakini wiki 7 baadae nikiwa bado nina kumbukumbu ya show ile nikapata habari za kuuawa kwake. Ilikuwa ngumu kuamini lakini ulikuwa ukweli kuwa mtu aliyetumia muda wake mwingi kupigania haki na usawa na upendo miongoni mwa jamii na kukemea maovu kama uporaji na mauaji, anajikuta akiwa mhanga wa yale aliyojaribu kuisaidia jamii kuondokana nayo.
Lucky alikuwa ASKARI anayepigania haki za kinamama na watoto, akipinga ubaguzi na ukandamizaji, akisimamia imani, kuelimisha kuhusu mfumo wa maisha upumbazao wengi, kutetea misingi ya muziki wa Reggae, Mapenzi, kuburudisha kwa hadithi za kusadikika ambazo ukweli wake upo katika jamii zetu na pia alikuwa mume kwa Zanele na baba kwa watoto wake 7. Ukisikiliza nyimbo zake nyingi, Lucky alikuwa ni msanii anayeelezea hadithi halisi tangu mwanzo wa nyimbo na unapomaliza kusikiliza wimbo unatambua alichokuwa akikisisitiza ama kukanya, ama kuelimisha. Ukisikiliza PRISON anaanza kwa kusema "somebody told me about this when i was still a little boy. He said to me crime does not pay, education is the key. As a little boy i thought i know what i was doing. But today here i am. I'm a Prisoner". Sikiliza wimbo wake wowote utaweza kuona mpangilio wa mashairi katika kueleza atakacho na hicho kilimtofautisha saana na wasanii wengine.
Sikiliza pia uhusiano wa midundo na ujumbe katika nyimbo zake utatambua kuwa alikuwa na uwezo wa kuiweka hadhira katika utayari wa kupokea ujumbe kwa mirindimo iendanayo na ujumbe katika wimbo
Lucky Dube katika miaka 25 aliyoshiriki katika sanaa hii ya muziki aliweza kutoa jumla ya albamu 23 ambazo 6 kati yazo alitoa katika mahadhi ya Mbaqanga, 1 katika mahadhi ya Afrikaans na 16 katika mahadhi ya Reggae. Ni mahadhi ya Reggae yaliyompa nafasi ya kutambulika, kuheshimika na kuelimisha jamii kwa upana wake ambako katika albamu hizo ameimba kuhusu mambo mengi yanayoathiri maisha yetu ya kila siku miongoni mwao ikiwa ni pamoja na Haki za wanawake na watoto (Hold On, Little Heros, God Bless the women), Mahusiano na Mapenzi (Romeo, Never Leave You, I've got you babe, Big Boys Dont cry, Lovers in a dangerous time, How will i know, Release Me) , Siasa (Political Games, Monster, Is This Freedom, Guns and Roses, The Way It Is, Together as one,) Maisha ya kufikirika (My World, Divorce Party,), Ubaguzi (Together as One, Trinity), Maovu (Crime and Corruptions, War and Crime, Crazy World, mfumo wa maisha upumbazao watu (Other side, Shut Up, Affirmative action, Love Me the way i am), ya kale na ya sasa (Changing world, Money Money), Imani (Take it to Jah, Shembe, Rastas,) na hata muziki ( Reggae is strong, Back to my roots, We Love It, Seriouss Reggae Bussiness).
Lucky Dube aliuawa na watu wanaodhaniwa kutaka kupora gari lake mbele ya nyumba ya nduguye alipotoka kuwapeleka wanawe usiku wa tarehe 18 Oktoba 2007. Ni kama alivyoimba katika wimbo wake wa CRIME AND CORRUPTON kuwa "do you ever worry about leaving and coming back in a coffin, with bullets in your head" ndivyo haswa ilivyokuwa hatima ya maisha yake. Kama alivyoimba katika Reggae Is Strong kuwa "Nobody can stop reggae" ndivyo kazi zake zinavyoendelea kuielimisha jamii kila kuikicha licha ya maisha yake kusimamishwa.
Kazi zake zitaendela kuburudisha, kuelimisha na kuikomboa jamii kutoka utumwa wa kiakili bila kikomo.

REST IN PEACE LUCKY