Monday, June 8, 2009

The Ngoma Africa Band ndani ya Masala Festival,Hannover,Ujerumani

Bendi maarufu ya mziki wa dansi barani ulaya "The Ngoma Africa Band" yenye maskani yake mjini Oldenburg,Ujerumani.wataupeleka mzimu wa dansi katika jukwaa kubwa la maonyesho la Masala Festival,mjini Hannover,Ujerumani siku ya jumapili ya 14-Juni-2009 .
Bendi hiyo yenye tabia ya kupelekana mchaka mchaka na washabiki wa mziki ughaibuni inatarajiwa kutumbuiza majira ya saa 10.00 alasiri,ambako washabiki wa nyimbo za kiswahili na mziki wa dansi wanaisubiri kwa hamu bendi hiyo, iliyofanikiwa kujizolea umaarufu kwa kutumia mdundo wa dansi wa bongo.
Kiongozi wa bendi hiyo Ebrahim Makunja aka Ras Makunja ataliongoza kundi hilo jukwaani kwa kazi moja tu nayo ni kuwadatisha akili washabiki! Wasikilize kwa kubofya www.myspace.com/thengomaafrica ama waweza kuwasiliana nao kwa barua pepe kupitia anwani ngoma4u@googlemail.com. Kujua mengi kuhusu kundi hili mahiri, bofya hapa
http://www.africa-news.eu/news/entertainment/the-ngoma-africa-band-continues-to-thrill-fans.html

Source: Msema Kweli

No comments: