Showing posts with label Politics fix. Show all posts
Showing posts with label Politics fix. Show all posts

Thursday, August 22, 2013

MJADALA WA MAONI YA KATIBA MPYA KWA WAKAZI WA DMV


Ndugu watanzania wa Washington DC na vitongoji vyake.
Tunapenda kuwakaribisha katika mjadala wa Katiba mpya ya Tanzania utakaofanyika siku ya Jumamosi (24/8/13) kuanzia saa tisa kamili alasiri mpaka saa kumi na mbili jioni.
Mjadala huu utakaorekodiwa kwenye video utasambazwa kwenye vyombo mbalimbali vya habari pamoja na ofisi husika.
WAHUSIKA WANAOTARAJIWA KUSHIRIKI NI:
1: Wawakilishi wa matawi ya vyama vya siasa (CCM, CUF, CHADEMA)
2: Wawakilishi wa Jumuiya na Taasisi za waTanzania 
3: Wananchi wote watakaohudhuria kuchangia na kuuliza maswali.
 Anwani ni
3621 Campus Drive
College Park, MD 20740


Tafadhali....JIANDAE na Usikose kuhudhuria na kutoa mchango wako ili kufanikisha kupata katiba itakayotufaa sote.

Wednesday, May 8, 2013

Ya Lwakatare na "kesi ya ugaidi"....kuna la kujifunza

Leo tumepata habari za kufutwa mashitaka ya uGAIDI yaliyokuwa yakimkabili kiongozi mwandamizi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo Bwn Wilfred Lwakatare.

Lakini hili (la kushutumiwa kwa kesi kubwa kisha ikaishia "hewani" bila maelezo kamili ya kwanini ilianza na / ama imeishia ilivyoisha) halijaanza kwenye kesi hii ya Bwn Lwakatare pekee.
Tulishaiona kwenyebaadhi ya kesi zilizovuma nchini Tanzania
Kesi kama ya Babu Seya, ya Zombe, ya Balozi Mahalu nk
TATIZO ninaloliona ni kuwa, hakuna anayewajibiswa kwa MAKOSA YA KESI HIZI.
Kinachotokea ni kuwa KESI INAJENGWA KWA (kile nilichofafanuliwa kama) PROBABLE CAUSES kisha inashindiliwa kwa mmoja na huyo AKICHOMOKA basi kesi imekwisha (at least machoni mwa waTanzania waliofanywa kuifuatilia).
Ama kinyume chake huwa sahihi..
Kwamba KESI INAJENGWA KWA (hichohicho nilichotambulishwa kama) PROBABLE CAUSES kisha inashindiliwa kwa mmoja ambaye "hachomoki".
Kama kuna mamilioni yaliibiwa ubalozini kwenye kesi ya Balozi Mahalu, kama kuna uuaji ulifanyika kwenye kesi ya kina Zombe, kama kuna UGAIDI kama ulioelezwa na M'bunge aliyeonyesha karatasi ya ushahidi mahakamani (0:59)

NA BADO WASHUTUMIWA WAKASHINDWA KUTIWA HATIANI......HII INA MAANA WALIOTENDA MAKOSA HAYA WAKINGALI WANAPETA
Lakini pia.....
Vipi kuhusu wale ambao wanasota jela wakiomba DNA itumike na haitumiki ili TUWAHUKUMU KUKAA HUKO ama TUWAPOKEE MTAANI na kila upande uridhike?
Maswali haya si mapya kwangu hapa kibarazani...
Januari 2, 2010 niliandika...
"...Lakini ni kwanini tusifanye kitu kwa usahii kwa mara ya kwanza? Na kama kuna ambao ni watu huru huko magerezani (na kwa habari nilizokuwa nasikia kuhusu kubambikiziana keshi nina hakika wapo), ni kwa muda gani tutaendelea kuwashikilia? Na siku wakija kugundulika kuwa walifungwa kimakosa ni nania wa kubeba gharama za kuwafidia? James Bain sasa atalipwa $50,000 kwa kila mwaka aliokaa gerezani. Ina maana Jimbo la Florida litamlipa takribani dola milioni 1.75 muda mfupi ujao. Na hiyo ni kwa kuwa waendesha mashtaka walifanya makosa. Kama ulimwengu wetu wa Tanzania utabadilika (na naamini umeanza) na kupata watu watakaotetea haki za walio gerezani bila hatia, ni nani wa kulaumiwa? Ni vipi tupate mabilioni ya kukarabati nyumba za watendakazi wa serikali na tukose vifaa kama hivyo kuamua kesi muhimu kama hizo? Ni maisha mangapi yanawekwa pasipostahili kwa kuwa tu wenye dhamana hawajali HAKI NA USAWA wa wananchi wao?...."
REJEA HAPA KWA ARTICLE KAMILI
Bado tatizo la uwajibishaji linakuja hapa ambapo tunashindwa kujua kuwa IWAPO KOSA LIMETENDEKA, KWANINI ASIPATIKANE WA KUWAJIBIKA NALO?
KUNA LA KUJIFUNZA

Friday, April 19, 2013

Ana kwa Ana na Nape Nnauye....Mwaka mmoja baadae


Mwishoni mwa mwaka 2011, nilibahatika kupata fursa fupi ya kuketi na kuhojiana na Katibu Itikadi na Uenezi wa Chama Cha Mapinduzi Ndg Nape Nnauye. Alikuwa nchini kwa ziara fupi ya kikazi na pia alikutana na wanachama wa matawi ya CCM hapa nchiniTulijadili mambo machache tofauti kuhusu chama anachoongoza na migogoro iliyomo ndani mwake.
MWAKA MMOJA TANGU TUHOJIANE...UNAONA MABADILIKO?
Karibu kusikiliza mahojiano yetu hapa chini

Sunday, March 31, 2013

MJADALA: Mustakabali wa Jumuiya za waTanzania baada ya ujio wa matawi ya vyama vya siasa

Karibu katika mjadala kuhusu mustakabali wa Jumuiya mbalimbali za waTanzania katika DIASPORA baada ya kufunguliwa kwa matawi ya vyama mbalimbali vya siasa katika nchi husika.
Katika mjadala huu uliohusisha wakazi wa Washington DC na vitongoji vyake (DMV), washiriki wanajaribu kujadili namna tulivyofika hapa na pia namna ya kuweza kujinasua toka katika hii dhana ama hali halisi ya TATIZO la mgawanyiko unaoanza kujitokeza kutokana na ITIKADI miongoni mwa waTanzania.
Karibu uungane nasi
 

Thursday, March 14, 2013

Ya Lwakatare na VIDEO YAKE........MSHINDI AWE MTANZANIA

Hivi karibuni kumetolewa VIDEO HII HAPA (na chini) ambayo kwa hakika imezua tafrani kwa jamii nzima.
Katika mijadala mingi iliyoibuka kuhusiana na video hiyo, yaonekana watu wamesahau kuhusu TANZANIA na mjadala umehamia kwenye mchuano kati ya wafuasi waaminiyo SERIKALI YA CCM NA UPINZANI.
Lakini watu hawa wamesahau kuwa haijalishi kilichotokea mpaka sisi kuiona video hiyo,VIDEO HIYO NI HATARI KWA USALAMA WA TAIFA (katika hali iwayo yote)

Iwe imeghushiwa ama ni halisi, video hii INADHIHIRISHA TISHIO KATIKA USALAMA WA TAIFA
1: Kama imeghushiwa, ina maana taifa letu liko kwenye "ncha" ya machafuko toka kwa watu wenye vipaji vya kutengeneza video zilizo karibu na ukweli.
2: Kama ni ya kweli, basi taifa letu liko kwenye "ncha" ya kuingia katika IMANI ISIYO SAHIHI kuhusu yanayotokea na yanavyotokea.
Kinachonishangaza ni kuwa, badala ya kuweka MASLAHI YA TAIFA NA WANATAIFA MBELE, na kupambanua CHANZO CHA VIDEO HII ili kutumika kutoa ushahidi wa moja kati ya mambo mawili niliyozungumza, naona ITIKADI INATAWALA mijadala hii jambo ambalo si la manufaa hata kidogo.
Jamani...
Tuwe waTanzania kwanza.
Tujadili namna ya kupata suluhisho la TISHIO HILI LINALOTUKABILI.
Natumai tutaanza kuona ITIKADI ZIKIWEKWA KANDO NA KUANZA KUJADILI HATARI INAYOAMBATANA NA VIDEO HII.
Na kwa kufanya hivyo, MSHINDI ATAKUWA MTANZANIA na sio itikadi kwani tutakuwa tumepata CHANZO NA NIA YA VIDEO HII, NA HILO LITAEPUSHA HATARI INAYOLIKABILI TAIFA

Na huu ni MTAZAMO WANGU kwa namna nionavyo tatizo.
Labda namna nionavyo tatizo ndio tatizo.


"POLITICS FIX" ni kipengele kinachozungumzia mambo ambayo blogu hii inaamini yanastahili kuwekwa vema katika siasa za nyumbani Tanzania, ama zinazoathiri Tanzania. Kusoma matoleo yaliyopita katika kipengele hiki BOFYA HAPA

Sunday, August 26, 2012

Matawi ya vyama vya siasa DIASPORA….DALILI NZURI, “MADENI” ZAIDI

Hatimaye ufunguzi wa tawi la CCM hapa Washington DC umefanyika Jumamosi ya Agosti 25 mwaka huu ikiwa ni siku 100 kamili tangu kufunguliwa kwa tawi la CHADEMA hapa.
Na kama ilivyoonekana kwenye taswira za ufunguzi wa matawi yote, IDADI YA WANACHAMA NI KUBWA.
Hiviii......Unaona UMATI MNENE kwenye uzinduzi wa tawi la CCM-DMV?
Photo Credits: Vijimambo Blog 
Na Je!!!...Uliona UMATI MNENE kwenye uzinduzi wa tawi la CHADEMA-DMV?
Photo Credits: Swahili Villa Blog 
Hii ni dalili nzuri sana.
Kwamba kuna namna nyingine ya kiITIKADI katika kuwaunganisha waTanzania wa jamii ya hapa Washington DC na vitongoji vyake. Na dalili iliyo nzuri zaidi, ni kuwa HAKUNA UHASAMA kati ya watu wa itikadi mbili hizi.
HONGERENI KWA HILO .
Na sasa tumeshuhudia uzinduzi wa matawi haya (kwa hapa DC na kwingineko) na kwa hakika tumeona IDADI ya kuridhisha kwa waliohudhuria uzinduzi wa vyama vyote, linalofuata (ama niseme LINALOTAKIWA KUFUATA) ndilo ninaloita DENI.
TANZANIA ina mahitaji mengi sana ambayo yanahitaji ushirikiano (hasa wa kimawazo) toka kwa watu wa “upande wa pili”. Ninaloamini ni kuwa IWAPO WATU WOTE HAWA KWENYE MIKUTANO YOTE HII WATAUNGANISHA NGUVU (HATA ZA MAWAZO) kusaidia matatizo ya Tanzania, TUTAFIKA MBALI.
Na hilo ndilo DENI KUU kwetu. Na ndio DENI KUU kwa viongozi wa matawi haya…KUUNGANISHA WANACHAMA WAO KUWEZA KUIJENGA TANZANIA YETU.
Nawatakia kila la kheri WANACHAMA NA VIONGOZI WOTE wa matawi ya vyama vya siasa katika DIASPORA.
Lakini nawakumbusha kuwa CHANGAMOTO YETU si kuwa na matawi mengi, ama wanachama wengi, bali kuwa sehemu ya suluhisho la matatizo yaliyoko nyumbani Tanzania na kwa kufanya hivyo, tutaona UMUHIMU WA MATAWI HAYA KATIKA DIASPORA.

Nawaza kwa sauti tuuuuuuuu!!!!!!!!! 

"POLITICS FIX" ni kipengele kinachozungumzia mambo ambayo blogu hii inaamini yanastahili kuwekwa vema katika siasa za nyumbani Tanzania, ama zinazoathiri Tanzania. Kusoma matoleo yaliyopita katika kipengele hiki BOFYA HAPA

Tuesday, January 3, 2012

Kabla Magufuli hajaomba radhi, ...........

Waziri wa Ujenzi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. John Magufuli
Moja kati ya habari zilizotawala mwanzo wa mwaka huu ni kupanda kwa nauli za vivuko na hasa cha Kigamboni. Hili limeonekana kupata msukumo wa upinzani toka sehemu mbalimbali na zaidi toka kwa WABUNGE walioonyesha nia ya kumfanya Waziri Magufuli awaombe radhi wananchi na pia kufuta kauli yake. Kauli inayozungumziwa hapa ni ile aliyonukuliwa akisema "Na
atakayeshindwa kulipa nauli mpya Dar- Kigamboni na apige mbizi au azunguke
Kongowe" Hii IMEWAKERA WENGI (miongoni mwa wachache waliolalamika)
Kwanza niwapongeze wabunge wa KULIVALIA NJUGA HILI.
Lakini pia niwapongeze kwa uwezo wao kuwahadaa wananchi wao juu ya hili.
Suala la kupanda kwa nauli linaonekana kutokea na kupata nafasi kubwa kwenye vyombo vya habari kwa sababuni kweli kuwa WANANCHI HAWANA UWEZO WA KULIPIA KIVUKO (hata kabla ya nyongeza ilikuwa taabu)
Lakini lazima sote tukubali kuwa kuna ulazima wa kuongeza bei ya kuvuka kwa kuwa GHARAMA ZA KUENDESHA KIVUKO ZIMEPANDA.
Sasa hapa kuna namna ya kushughulika na haya. NAMNA AMBAYO WABUNGE WANGU (walio wabunifu wa kukwepa vyanzo vya matatizo) wanaepuka. Tunatakiwa kuangalia chanzo cha tatizo kuliko mvuto wa kuendekeza "UVIVU WA FIKRA" ambao unatuaminisha katika kila tunacholishwa na hawa wanajaribu kupata "UTENDAJI KAZI" kwa mambo ambayo si suluhisho la matatizo ya wananchi.
Na hili (la kutatua chanzo cha tatizo) ndilo la muhimu kuangalia kwa kuwa ndilo litakalotatua tatizo na pia limo ndani ya uwezo wetu.
Gharama za kuendesha kivuko si kitu ambacho tunaweza kushughulikia kwa urahisi. Lakini tunaweza kujadili na kutatua suala la uwezo wa wananchi kulipia kivuko hicho.
Majuzi niliona WARAKA WA KAKA MBUNGE WA KIGAMBONI kuhusu kupinga ongezeko. Na nukuu ya walionakiliwa. Nami palepale (kwenye facebook) nikampongeza na kumueleza "Hii ni safi sana. Naamini wananchi wa Jimbo lako wataanza kufuarahia MPANGO WAKO MPYA wa kuwawakilisha na kutuwekea hapa. Sijawa na takwimu halisi, lakini nilisikia "pingamizi kubwa" la wananchi wa Kigamboni kuhusu POSHO ZENU WABUNGE. Unaweza kuliandikia na hilo pia? Ama ni mimi niliyekosa barua yako kuhusu hili? HERI YA MWAKA MPYA" na yeye akanijibu akisema "Mubelwa acha fujo. Msimamo wangu ni kwamba mfumo mzima wa malipo kwa watumishi wa umma unapaswa kuangaliwa upya na usilenge wabunge peke yao."
Haikuniingia akilini kuona HOJA YANGU INATAFSIRIWA KAMA FUJO, na ndio maana nikamjibu kuwa "FUJO? Kaka. Nadhani unatania. Na kama la, basi nitalazimika kuanza kukushangaa. Ni kipi nilichosema ambacho ni cha fujo? Je! Kwa huo msimamo wako kuwa "malipo kwa watumishi wa umma unapaswa kuangaliwa upya na usilenge wabunge peke yao" ULIUANDIKIA BARUA KAMA HII? Kama ndivyo, pongezi. Kama sivyo, kwanini? Na hii pia inakuwa fujo?
Nahisi unanirejesha kulekule kwa Ndg Lazaro Nyalandu aliyelalamika kuwa sisi tuulizao hili na lile TUNA UBUNIFU WA KULALAMIKA. Sina hakika kama hili ni suala lililopo "mjengoni" ama la. Lakini kama nilivyoweka bayana MSIMAMO WANGU KWA NDG. NYALANDU HAPA, sitasita kuweka bayana kwa yeyote atakayeonyesha ubunifu wa kulalamikia walalamishi wasio wabunifu. "

Swali ni kuwa KWANINI WANANCHI WASHINDWE KULIPA? Na je! Magufuli akiomba radhi itasaidia vipi kubadili maisha ya wananchi?
Niliwahi kutoa mfano mmoja wakati nimekwenda Karagwe mwaka 2003. Wakati huo, rais wa awamu ya tatu alikuwa ametoa msamaha wa kodi ya wananchi. Watu wakapongeza. Lakini nilipokwenda kijijini Karagwe nikagundua kuwa WATU HAWAKUHITAJI MSAMAHA WA KODI KWANI HAUKUWA UKIWASAIDIA KUTATUA TATIZO LAO LA UCHUMI. Wakati huo, nilifika gulioni na kukuta watu wameleta mikungu ya ndizi ambayo walikuwa tayari kubadilishana nayo kwa PAKITI YA CHUMVI YA SHILINGI HAMSINI. NA HAWAKUPATA MTU WA KUBADILISHANA NAO. Wakaziacha hapo kwa kuwa hata nyumbani zipo zinazoivia shambani. Wakati huo huo, mkungu huo wa ndizi ulikuwa ukiuza kwa maelfu ya shilingi jijini Dar. TATIZO LILIKUWA NI BARABARA. Kama barabara ingekuwa nzuri, basi magari yanayofuata ndizi yangefika kule, na pengine wangeuza kwa shilingi elfu moja ama mbili, yule muuzaji angeuza mwanza kwa elfu kama tano na wale wa Dar wangeipata kwa bei zaidi.
Ina maana kama mtu huyu angeuza mikungu mitatu, angepata shilingi elfu tano za kulipa kodi. Kwa maana nyingine, mwananchi angelipa kodi, mwananchi angebaki na pesa mfukoni na serikali ingekusanya mapato zaidi na pengine mlaji wa Dar angepata ndizi kwa bei nafuu zaidi kwa kuwa usafiri usingekuwa na gharama kubwa sana.
Ni hilo linalonifanya niiwaze Kigamboni.
Wananchi hawana maisha mabaya kwa kuwa Magufuli kaongeza nauli, bali kwa kuwa WANANCHI HAWANA KAZI, HAWANA BIASHARA NA / AMA VYANZO VYA MAPATO.
Na hili ndilo liletayo yote haya. Na HILI HALITOKANI NA KAULI AMA HATUA YA MAGUFULI KUPANDISHA NAULI.
Hawa wabunge niliosikia wamemtaka Waziri Magufuli aombe radhi, wangeanza kwa kutueleza wao wamewafanyia nini wananchi wao kuweza kuwakwamua katika uwezo mdogo wa kulipa nauli? HILI NDILO TATIZO KUU.
Kama wananchi wangekuwa na kipato mara mbili ya walicho nacho, wasingejali kuongezewa hizo gharama, hasa kwa kuwa zimetajwa kuongezwa kwa NIA ILIYO SAHIHI. Suala la kauli ya Magufuli, ni moja, lakini haliendani na CHANZO CHA TATIZO.
Narejea kusema kuwa JAPO DALILI ZA KUKOSEKANA KWA MAJI KWENYE MTI HUONEKANA KWENYE MAJANI, WAKATI WA KUMWAGILIA, TUNAMWAGILIA MIZIZI NA SI MAJANI. Wabunge wajiulize kwanini wananchi hawataweza kulipa hicho kiwango kipya badala ya kung'ang'ania kuwa kauli ya Magufuli ni mbaya.
By the way, wangeshughulikia na kurejesha pesa zilizofujwa, wakagoma kupokea posho zao na kuacha ku-extend vikao kwa mambo yasiyo na tija kwa wananchi, ningeweza amini kuwa wana "uchungu na wananchi wao". Na pengine pesa hizo zingetosha kujenga daraja.
Nimeona wakilalamika kuliko ambavyo nilisikia wakiWAKILISHA MAONI YA WANANCHI KUHUSU POSHO ZAO, KUHUSU UMEME, KUHUSU MENGINE MENGI.

KABLA MAGUFULI HAJAOMBA RADHI....WABUNGE MTUELEZE MMEFANYA NINI KUWAWEZESHA WANANCHI KUMUDU (JAPO) NAULI YA ZAMANI, YA SASA (ILIYO NA ULAZIMA) NA PIA KUTIMIZA AHADI ZENU. Mtueleze MMEWAWAJIBISHA VIPI MAFISADI, na MNAONA UWIANO GANI KATI YA PESA MNAZOLIPWA, KAZI MNAYOFANYA NA WANANCHI WA MAJIMBONI MWENU!

Sunday, November 6, 2011

Chonde chonde "waheshimiwa". Kabla hamjasema tena ya Cameron.......

Picha kwa hisani ya Mawasiliano Ikulu Blog
Moja kati ya habari zilizotikisa anga la TAARIFA nchini Tanzania ni suala la serikali ya Uingereza kutoa kauli kuhusiana na haki za mashoga na misaada kwa wale waipingao.
Punde baada ya kauli hiyo tukasikia kauli mbalimbali za viongozi mbalimbali wa Tanzania kuhusiana na hili hasa kwa kuwa lilihusisha SERA na MISAADA kwa nchi zetu. Kauli rasmi ya kwanza ilitolewa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Mhe Bernard Membe ambaye amenukuliwa akisema “Tanzania ni nchi maskini lakini hatutakubali kuruhusu upuuzi huo eti kwa sababu ya misaada yake na fedha zao, lakini ushoga si utamaduni wetu, hata sheria zetu zinakataa,”
Na kama hukubahatika kusikia kauli ya Mhe Membe basi kuna kitu unakosa katika maandishi haya, msisitizo wa kimatamshi ama niseme "TONE".
Kwa namna alivyotamka, kwa hakika ungetambua kuwa alikuwa akipinga taarifa na kauli hizo za Mhe Waziri Mkuu wa Uingereza. Siku hiyohiyo tukaona "tweet" toka kwenye akaunti itumiayo jina la Jakaya Kikwete (na naamini ni ya mhe Rais kwani kama imekuwepo kwa muda mrefu wangeshaitoa iwapo isingekuwa yake) nayo ilieleza kama unavyoona hapa chiniOK.....WAHESHIMIWA WAMESEMA.
Nirejee nyuma kidogo. Mpaka kwenye post yangu hii ya Februari 24 2010 iliyokuwa na kichwa kisomekacho Wanasiasa wetu na sakata la Ushoga / Usagaji.
Hili bandiko lilikiwa maalum kueleza MTAZAMO WANGU kutokana na kauli ya Mbunge wa chama tawala cha NRM Mhe. David Bahati aliyewasilisha mswada katika Bunge la nchini UGANDA ambao kama ungepitishwa (wakati huo) basi ungewaadhibu MASHOGA NA WASAGAJI walio nchini Uganda na wenye asili ya Uganda kwa adhabu mbalimbali kuanzia kifungo mpaka kifo.
 Katika bandiko hil nilieleza mambo lakini mwanzo nilieleza kuwa ni lazima tujiangalie na kutambua kuwa MASHOGA NA WASAGAJI wamezaliwa katika familia ambazo nyingi ni za watu wasio mashoga wala wasagaji. Kwa hiyo kama wamezaliwa katika familia zilizo tofauti na walivyo wao, NI LAZIMA TUJIULIZE kuwa NI WAPI TULIPOJITENGA NAO NA KUWAFANYA / KUWAACHA WABADILIKE NA KUWA WALIVYO?
Sisi kama JAMII TUNA SEHEMU YA LAWAMA kwa kuwa ama hatuwasaidii kutokuwa walivyo, au tunachochea kuwa walivyo hata kama twatenda haya bila sisi kujua.
HAPA NDIPO NINAPOKUJA KWA WAHESHIMIWA HAWA WAWILI WALIOTOA KAULI.
WAHESHIMIWA...
Kama suala la mashoga na wasagaji linawakera kama ambavyo mmeonyesha kwenye kauli zenu, ni yapi ambayo mmeyafanya kulipunguza ama kuliondoa?
Mimi na ninyi na wasomaji wangu tunajua kuwa kama tungekuwa na mashoga sifuri, basi tusingehofu kuhusu hili. Lakini kwa kuwa idadi yao ni kubwa NA INAONGEZEKA KWA UHURU KILA UCHAO, mnaona athari zake. Lakini kabla hamjasema tena juu ya kauli ya Cameron, mtusaidie kutueleza ni yapi mmefanya kupunguza ama kuondoa ushoga Tanzania?
Tena nimesikia Mhe Membe akisema SHERIA INASEMA WANAWEZA KUFUNGWA MPAKA MIAKA 30 JELA.
Sina hakika ni wangapi walikuwa wakilijua hili, na sina hakika takwimu za Waziri na Rais zaonyesha ni wangapi wameshafungwa kwa hili?
Kama nilivyosema katika post yangu ya mwaka jana, hakuna kiongozi anayetaka kujishughulisha na chanzo cha tatizo. Wanakurupuka kwa namna za KUAHIRISHA tatizo na kisha kutumia uhahirisho huo kujipatia kura za kurejea madarakani. Kisha tatizo larejea.
Wakati nasikia habari za kile nilichokuja kung'amua kama matendo ya kishoga na usagaji nilikuwa mdogo, na nina imani kuwa walikuwepo mashoga na wasagaji wachache saana ukilinganisha na sasa lakini kile wanachokiita "mila za kiAfrika" ziliwazuia wazazi, walezi na viongozi kujadili ATHARI za kujikita kwenye tabia mbaya kama hizo na matokeo yake ndio tuonayo sasa ambapo tatizo hili LIMEOTA MIZIZI na twasikia harakati za KUWAFUNGA MIAKA 30. Kisha baada ya hapo?
Hivi waheshimiwa mmeshawahi kwenda magereza na kuona hali ilivyo?
Magereza zetu hazina zinachofanya kubadili tabia za wafungwa. Niliwahi kuuliza haya katika post hii ya maswali yangu kumi kwa Rais Kikwete, kisha nikauliza hapa KWANI KAZI ZA JELA ZETU NI ZIPI???, na kabla ya hapo niliuliza hapa kuwa UBORA WA JELA NI UPI NA ZETU NI NAMBA NGAPI?, na hata kuhusu "mibambiko" ya jela kama hii hapa, kuhusu Magereza zetu, lakini nani alijishughulisha kujibu? Kwa taarifa yenu, Magereza zetu zasemekana kuwa kama "maskani" za mashoga na / ama vyanzo vya ushoga. Sasa wapelekeni tuhalalishe magereza yetu kuwa "RAINBOW HEADQUARTERS".
Kama ni kweli waheshimiwa wote mmkereka na kauli ya Mhe Cameron, tuambieni mmeshafanya nini, mnafanya nini na mtafanya nini kuondoa suala la ushoga na usagaji ambalo MMEONYESHA kuwa mnalipinga kwa nguvu, ari na kasi MPYA.
Nasio Fontaine aliwahi kuonya katika wimbo wake DANGEROUS kuwa "don't worry about the pretty things you hear them say" na katika ubeti wa kwanza anaanza akisema "I heard your speeches, man and your empty promises. But now that i know, YOUR WORDS ARE DANGEROUS" Hebu msikilize kwa UKAMILIFU

Tuwekeni POLI-TRICKS pembeni na kujaribu kuisaidia TANZANIA YANGU kutoka kwenye MATATIZO yanayotatulika.

Wednesday, May 4, 2011

Hesabu za siasa na ki-sisasa

Mara zote ni kinyume; wengi ndio wachache na wachache ndio wengi

Hivi ulibahatika kusoma toleo la Kaka Kamala alilosema MOJA JUMLISHA MOJA SAWA NA MOJA? (BOFYA HAPA KAMA ILIKUPITA). Je maoni ya waliochangia akiwemo Ndugu Born Again Pagan?
Kuna ukweli wa hesabu za wenzetu hawa wanasiasa ambazo kwa namna moja ama nyingine zimekuwa kinyume na zile tulizozoea kwenye masomo na elimu yetu ya kawaida. Wiki hii tumeanza na habari za kuuawa kwa Osama bin Laden. Watu wakasherehekea na kurukaruka wakisema WAMEMPATA MTU ALIYEKUWA AKITISHIA USALAMA. Lakini punde baada ya MTU huyo kuuawa, hali ya usalama ikaimarishwa duniani kote. Swali nililojiuliza na ninajiuliza ni kuwa "iweje mtu anayeonekana kuwa hatari auawe na kisha hali ya usalama iwe mashakani kuliko ilivyokuwa wakati yuko hai?" Unadhani unaambiwa ukweli kuhusu HATA ya mtu huyu? Ndugu yangu mmoja aliandika kwenye ukurasa wangu wa Facebook kwamba kama Osama alikuwa MTU HATARI, basi wamepata kimoja kati ya viwili. Wamempata MTU lakini hawajazuia HATARI. Lakini katika HESABU ZA KISIASA (ambazo naona zinakwenda kinyume na hesabu zetu wananchi), ni USHINDI. KWANINI?
Kwa HESABU ZAO, ni kama vile "wengi wanakuwa wachache na wachache wanakuwa wengi." Hakuna kujali kile wanachoimba na kuahidi kukitetea wakati wa kampeni zao. Hawawajali wananchi na kwao ubinafsi ni maana nyingine ya "manufaa kwa umma"
Labda tuangalie UMOJA WA MATAIFA ambao una wanachama lukuki na unaonekana "kutawala" dunia kimaamuzi lakini bado maamuzi ya mataifa matano yenye kura ya turufu ndiyo yanayoamua dunia iende wapi, iadibike na / kuadibishwa vipi, nani awe rafiki wa nani na nani awe adui wa nani hata kama hawana jibu la kwanini iwe hivyo. Na mataifa mengine yanatulia na kuendelea kutafsiri hiyo kama DEMOKRASIA.
Tukirejea kwenye ngazi ya nchi, tunaona kuwa maslahi ya wananchi pengine ndio kitu cha mwisho kufikiriwa akilini mwa "waheshimiwa" hawa. Wanatanguliza u-mimi na hata maamuzi yao hayaonekani kuwajali wengi ambao ndio waliowachagua. Hawawajibiki, hawaonekani kuwathamini na hawako katika nyadhifa zao kushughulikia lolote lihitajiwalo nao. Kwao, kulinda heshima yao ni jambo la muhimu kuliko kujali wananchi. Wanasikia matatizo, wanayaona na kisha WANAYAPUUZA
Nasema mahesabu yao yako kinyume maana kwao wananchi ndio "minority." Kwao wanaona kama wanahitajika kumaliza mahitaji yao kwanza ndio njia sahihi na ndio maana kwangu mimi ni WATAWALA kuliko viongozi.
Sasa kwanini tunawaamini? Kwanini tunawapigia kura wakati hatuna nafasi kwao kwani jamii nzima kwao ni "minority."
Wasikilize Morgan Heritage katika kibao chao hiki, POLITICIAN hasa wanaposema "why should we trust politicians, why should we vote every election? When there's no place for we, you and me, in the secret society they call us minority."

Tuesday, March 15, 2011

Lazima tupande ndio tuvune. Yaani tuwekeze ndio tunufaike.

Photo Credit: Qwota.com
"Everyone wants to go in heaven; but nobody wants to die" Ni mameno ya Winston Hubert McIntosh ama Peter Tosh alipoimba kwenye wimbo wa Equal Rights. Kwa ufupi naona kama linalohimizwa hapa ni suala la kutaka kuweka bayana kuwa kama unahitaji chochote lazima kuwekeza gharama zitakiwazo.
Natazama "mfumo" wa serikali uliopo na najiuliza kama unatoa changamoto kwa watendaji kusaidia walio na uhitaji. Yaani kama Rais na wabunge wote wanachaguliwa kwa wakti mmoja ina maana ikitokea wabunge wakawa wengi kutoka katika chama cha Rais basi hata wasipotekeleza ilani za uchaguzi hakuna wa kuhoji kwa nguvu bungeni. Lakini pia najiuliza kama serikali ni kwa ajili ya wananchi si ina maana wanatakiwa wafanye kila lililo ndani ya uwezo wao kuwezesha wananchi kufanikiwa? Unadhani itawezekana kama kufanya kila liwezekanalo itamaanisha serikali kuhatarisha nguvu zake za kiutawala? Kimsingi tutasema NDIO lakini kiitifaki itakuwa HAPANA.
Lakini bado najiuliza kama tungekuwa na chaguzi tofauti, kwa maana Marais na wakuu wa mikoa wakachaguliwa miaka miwili na nusu kabla ya wabunge na madiwani si ingekuwa safi? Kwamba kwa nusu muhula tunawaangalia na kuwasoma viongozi waliopo madarakani na kama hawatekelezi lolote "tunawamwagia upupu" kwa kujaza wapinzani wao kwenye uchaguzi ujao. Ndhani hii ingeamsha UTEKELEZAJI wa ilani za uchaguzi na pia ingewasaidia wananchi kupata kile wanachohitaji kutoka kwa wawakilishi na viongozi wao.
Najua watasema ni gharama, lakini kama ndizo zitakazowasaidia wananchi kutoka kwenye umaskini na ujinga kwanini zisitumike? Kuna gharama gani zaidi ya kuwa na taifa lenye uhitaji mkubwa leo kama ambavyo ilikuwa miaka 50 iliyopita?
Gharama lazima zitumike kuokoa taifa maana NI LAZIMA TUPANDE NDIO TUVUNE, YAANI TUWEKEZE NDIPO TUNUFAIKE

Saturday, February 19, 2011

MAKE A CHANGE......Bushman

"If we don't change our values and re-arrange our systems, we'll always gonna be another victims......"

"contradicting themselves in their every illustration, and make me believe in their world of confusions" "treating our people like they're gabage, and through lost of vanity we never seem to aknowledge......now it's time for us to re-enforce ourselves. Who's gonna do it for US? NONE BUT OURSELVES"
Hawa juu ni kina sisi wakiondoka "eneo la tukio"

Na huyu juu ni "yeye" alipotoka "eneo la tukio"

Kutambua watoto waliopotea / kupotezana na wazazi wao

Labda hakuna wa kulaumu kwa kuwa wa kulaumiwa ndiye mlaumu.
Labda HAKUNA ATAKAYEWAJIBIKA kwa kuwa NI DESTURI YAO.
Na sasa tumsikilize BUSHMAN katika wimbo MAKE A CHANGE

Photo Credits: Michuzi Blog, Full Shangwe Blog, Global Publishers Web.

Saturday, January 1, 2011

Mhe Rais, kabla hatujazungumzia katiba mpya, tufafanulie hili...

"NI VIPI WIZARA YA KATIBA IMETUMIA PESA ZA WANANCHI BILA KUTIMIZA HILI NA SASA UNAHITAJI KULIWEKEA TUME MAALUM?
Ni kweli tume hii itafanya kazi nzuri kuliko WIZARA? Na kama ndivyo, utaendelea kuwa na Wizara ya Katiba isiyojishughulisha na katiba kwa kuwa suala la katiba litashughulikiwa na tume utakayounda? Na pesa je? Kutakuwa na peza za WIZARA YA KATIBA na TUME YA KATIBA? "
Photo Credits: Dimitrios Kambouris via
Josephat Lukaza Blog
Usiku wa kuamkia leo, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Jakaya Mrisho Kikwete amehutubia Taifa katika salamu zake za mwaka mpya. Hotuba yake hiyo ya karibu robo tatu ya saa iligusia mambo mengi sana ikiwemo Hali ya Usalama nchini, Demokrasia, Uwajibikaji wa mawaziri, Nidhamu katika matumizi ya mali za serikali, Hali ya Uchumi, Hifadhi za chakula, Kilimo, Matatizo ya Umeme, Mahusiano ya kimataifa, Michezo na kisha akagusia MAADHIMISHO YA MIAKA 50 YA UHURU wa Tanganyika (ameita Tanzania Bara).
Na katika kugusia hilo, Mheshimiwa Rais wangu amezungumzia mambo makuu manne ambayo yanapangwa kufanyika mwakani. "Kwanza, nautangaza mwaka 2011 kuwa ni Mwaka wa Maadhimisho ya Miaka Hamsini ya Uhuru wa Tanzania Bara....Pili, tufanye tathmini ya kina ya mafanikio tuliyoyapata, katika juhudi zetu za kujiletea maendeleo katika miaka hamsini hii. Kila Wizara, idara na taasisi za Serikali na hata sekta binafsi zifanye tathmini ya eneo lake. Tathmini hizo ziandikwe katika vitabu ili kuhifadhi kumbukumbu hizo muhimu kwetu na kwa vizazi vijavyo. Vitabu na nyaraka hizo vitakuwa kumbukumbu zenye manufaa makubwa kwa wenzetu watakaokuwepo mwaka 2061 wakati wa kusherehekea miaka 100 ya Uhuru wa Tanzania Bara. Itarahisisha kazi yao ya kufanya tathmini wakati huo......Tatu, kwamba yafanyike maonyesho maalum katika Uwanja wa Maonyesho wa Julius Nyerere hapa Dar es Salaam na kote mikoani kwenye viwanja vya maonyesho, kuelezea mafanikio yaliyopatikana katika nyanja mbalimbali katika miaka 50 tangu Uhuru wa Tanzania Bara..." Hili nilishaligusia HAPA na nitalizungumzia kadri muda utakavyoruhusu. Kwa leo niendelee na mada kuu ambayo jambo la nne ambapo Mhe Rais amesema...
"Ndugu wananchi.
Jambo la nne ambalo tulilokubaliana kufanya ni kuanzisha mchakato wa kuitazama upya Katiba ya Nchi yetu kwa lengo la kuihuisha ili hatimaye tuwe na Katiba inayoendana na taifa lenye umri wa nusu karne. Katiba yetu ya sasa tuliyoachiwa na waasisi wa taifa letu, imeifanyia nchi yetu mambo mengi mazuri na kuifikisha Tanzania na Watanzania hapa tulipo. Tunayo nchi moja huru, ya kidemokrasia na inayoendesha mambo yake kwa kuzingatia utawala wa sheria, kuheshimu haki za binadamu na mgawanyo wa madaraka miongoni mwa mihimili mikuu ya dola. Nchi yenye amani, utulivu na watu wake ni wamoja, wanaopendana na kushirikiana na maendeleo yanazidi kupatikana.
Pamoja na hayo, mwaka 2011, nchi yetu inatimiza miaka 50 ya Uhuru wa Tanzania Bara, miaka 47 ya Mapinduzi matukufu ya Zanzibar na miaka 47 ya Muungano wa nchi zetu mbili. Yapo mabadiliko mengi yaliyotokea katika nyanja mbalimbali za maisha ya nchi yetu na watu wake katika kipindi hiki. Kwa ajili hiyo ni vyema kuwa na Katiba inayoendana na mabadiliko na matakwa na hali ya sasa. Katiba ambayo italipeleka taifa letu miaka 50 ijayo kwa salama, amani, umoja na kuwepo maendeleo makubwa zaidi.
Ndugu Wananchi;
Ndiyo maana tukaamua kuanzisha mchakato huu na kwa ajili hiyo, nimeamua kuunda Tume maalum ya Katiba, yaani Constitutional Review Commission. Tume hiyo itakayoongozwa na Mwanasheria aliyebobea, itakuwa na wajumbe wanaowakilisha makundi mbalimbali katika jamii yetu kutoka pande zetu mbili za Muungano. Jukumu la msingi la Tume hiyo litakuwa ni kuongoza na kuratibu mchakato utakaowashirikisha wananchi wote bila kubagua, vyama vya siasa, wanasiasa, wafanyabiashara, asasi za kiraia, mashirika ya dini, wanataaluma na makundi mbalimbali ya watu wa nchi yetu kote nchini, katika kutoa maoni yao juu ya wayatakayo kuhusu Katiba ya nchi yao.
Baada ya kukamilisha kukusanya maoni,Tume itatoa mapendekezo yake yatakayofikishwa kwenye vyombo stahiki vya Kikatiba kwa kufanyiwa maamuzi.Baada ya makubaliano kufikiwa, taifa letu litapata Katiba mpya kwa siku itakayoamuliwa ianze kutumika.
Ndugu Wananchi;
Ni matumaini yangu kuwa mchakato huo utaendeshwa vizuri, kwa amani na utulivu kama ilivyo sifa ya nchi yetu na mazoea yetu ya kujadiliana bila kugombana. Wananchi watapewa fursa ya kutosha ya kutoa maoni yao kwa uhuru na pawepo kuvumiliana kwa hali ya juu pale watu wanapotufautiana kwa mawazo. Pasiwepo kutukanana, kudharauliana, kushutumiana, kubezana, kuzomeana wala kushinikizana. Naomba washiriki waongozwe kwa hoja badala ya jazba. Tukiwa na jazba, hasira na kushinikizana kamwe hatutaweza kutengeneza jambo jema. Na inapohusu Katiba ya Nchi itakuwa hasara tupu. Haitakuwa endelevu na kulazimika kufanyiwa marekebisho mengi mwanzoni tu baada ya kutungwa.
Nawaomba Watanzania wenzangu wenye maoni yao wajiandae kushiriki kwa ukamilifu katika mchakato huu. Katoeni maoni yenu mazuri yatakayowezesha nchi yetu kuwa na Katiba itakayokidhi matakwa yetu ya sasa na ya miaka 50 ijayo."

Mheshimwa Rais. Kwanza nikupongeze kwa mikakati yote uliyoieleza. Umeonekana kutoa ufafanuzi katika mambo mengi. Lakini kuna moja ambalo NINAOMBA UTUFAFANULIE (hata kupitia msaidizi wako) KABLA HATUJAANZA MCHAKATO WA KATIBA MPYA. Katika Baraza lako la mawaziri ulilotangaza Nov 24 mwaka jana ulitaja WIZARA YA KATIBA NA SHERIA ambayo sasa ipo chini ya Mhe Selina Kombani. Waziri wa Sheria na Katiba Mhe Celina Kombani
Ninalowaza ni kuwa Wizara hii kamili yenye bajeti na watendakazi kamili ilikuwa ikifanya nini katika awamu yako ya kwanza? Natambua uwepo wake kama ilivyoonekana HAPA kwenye baraza lako la kwana ambapo ilikuwa chini ya Mhe Mary Nagu. Je! Kuna loloe ambalo tunaweza kuelezwa kuwa Wizara hiyo ilifanya katika miaka mitano ya awali katika suala la Katiba?
Ni kweli kuwa kuna UELIMISHAJI WOWOTE KUHUSU KATIBA uliofanywa na Wizara hii? Ama (kama mlijua kuwa Tanganyika itatimiza miaka 50 ya uhuru na 47 ya Tanzania) hamkukumbuka kutumia Wizara hii kuanza kufanya tathmini ya kujua nini kingehitajika mwaka 2011? Je!! Tutakosea kusema kuwa HUU NI MCHAKATO WA ZIMAMOTO?
Umesema (na hapa nakunukuu) "Baada ya kukamilisha kukusanya maoni,Tume itatoa mapendekezo yake yatakayofikishwa kwenye vyombo stahiki vya Kikatiba kwa kufanyiwa maamuzi.Baada ya makubaliano kufikiwa, taifa letu litapata Katiba mpya kwa siku itakayoamuliwa ianze kutumika."
SWALI LANGU NINALOOMBA UFAFANUZI ni kuwa, NI VIPI WIZARA IMETUMIA PESA ZA WANANCHI (na umenukuliwa ukisema matumizi ya serikali yameongezeka) BILA KUTIMIZA HILI NA SASA UNAHITAJI KULIWEKEA TUME MAALUM?
Ni kweli kuwa tume hii itafanya kazi nzuri kuliko ambayo ingefanywa na WIZARA? Na kama ndivyo, utaendelea kuwa na Wizara ya Katiba isiyojishughulisha na katiba kwa kuwa suala la katiba litashughulikiwa na tume utakayounda? Na pesa je? Kutakuwa na peza za WIZARA YA KATIBA na TUME YA KATIBA?
Ama watendaji wa Tume ya utakayounda watakuwa ni wafanyakazi wa Wizara ya Katiba? Kama ndivyo, natumai TUME HII HAITAKUWA MATUMIZI YA ZIADA bali sehemu ya shughuli za WIZARA ambao kwa kuwa zilistahili kuwa zimefanyika ama zifanyike kama wajibu wa kawaida na si "ofa" kwa waTanzania.
MUNGU IBARIKI TANZANIA, MUNGU IBARIKI AFRIKA.

Tuesday, December 21, 2010

Mhe. Nyalandu na ubunifu wa kulalamikia "walalamikaji wasio wabunifu"

Photo Credit: Lazarosnyalandu.com
Mtandao wa gazeti la Mwananchi toleo la jumapili ya Desemba 12, uliweka habari iliyomkariri Naibu Waziri wa Viwanda, Biashara na Masoko Mheshimiwa Lazaro Nyalandu akisema "Watanzania wanaoishi nje ya nchi, wamekua walalamikaji tu kuhusu taratibu za uwekezaji, lakini hawachukui hatua."
Aliyasema haya alipokuwa akifanya mazungumzo na gazeti hilo baada ya kuzindua Kampuni ya Ndege ya Bold Air katika uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwl JK Nyerere jijini Dar.
Kampuni hiyo inamilikiwa na Ndg John Ndunguru, mTanzania anayeishi Marekani.
Kisha Mhe. Naibu Waziri akaongeza kuwa “Kitendo cha kulalamika bila ya kuchukua hatua ni ishara kwamba wengi wao sio wabunifu. Nampongeza ndugu yangu John Nduguru, kwa kutumia fursa hiyo na kuanzisha kampuni hii,”
NAIBU WAZIRI ANAKOSOA ULALAMIKAJI NA UBUNIFU ilhali mwenyewe anakiri kuwa hali ya uwekezaji si njema na kuwa serikali ya awamu ya nne inapanga "kuwaandalia Watanzania mazingira bora ya uwekezaji kama ambavyo imekuwa ikifanya, ili kila Mtanzania aliyeko nje na mwenye uwezo wa kuwekeza, aje kufanya hivyo."
Baada ya kusoma makala haya na kuyatafakari (na kuombea fikra changanuzi) nimeishia kusikitishwa na UBUNIFU ALIONAO NAIBU WAZIRI KATIKA KULALAMIKIA WALALAMIKAJI.
LABDA KATIKA KUWEKANA SAWA NA MHESHIMIWA NAIBU WAZIRI.
KWANZA, binafsi nilitegemea Mhe Naibu Waziri "achukue hatua" (aliyosema sisi hatuchukui) kuwajibu na kuwaelimisha waTanzania "walalamikaji" walio nje ya nchi kupitia hizo blogu asomazo badala ya kwenda "kulalamika" kwenye gazeti. Ama angefanya vema zaidi kwa kuwa "mbunifu" na kuanzisha tovuti ama blogu ya Wizara yake itakayoeleza kwa ufasaha mambo mbalimbali kuhusiana na nafasi za uwekezaji zilizopo nchini.
PILI, tunatambua kuwa Tanzania kuna blogs nyiingi sana. Na kuna ambazo zipo makini kwenye kuandika matatizo mbalimbali na kisha kuona umuhimu wa kuweka suluhisho. Na hufanya hivyo.
Kisha zipo blogu za taswira ambazo huweka picha na "taarifa rejeo" ambazo zinabandikwa kama zilivyo na mara nyingi hakuna suluhisho linalotolewa. Kibaya zaidi ni kuwa wachangiaji wengi huwa ni "anonymous" ambao husema lolote watakalo hata kama haliifai jamii. NINAZIDI KUAMINI KUWA MHESHIMIWA WAZIRI ANASOMA HIZI. Na anadhani ndizo ziwakilishazo blogu za waTanzania. NA HILI LINASIKITISHA
Lakini MARADHI haya ya KUTOPENDA KUSOMA si ya sasa na ni kitu kibaya kuona kuwa yanamung'unya mpaka wanaotakiwa kutufanyia maamuzi yatakayojadili na kutabiri mustakabali wetu.
Naibu Waziri AMEDHIHIRISHA kuwa kwa mtazamo wake, kusaidia si kuelimisha, bali ni kutoa pesa. Yaani anaona sisi tunaoelimisha jamii ili iweze kujikomboa na kujitegemea TUNALALAMIKA NA HATUFANYI LA MAANA zaidi ya wale wanaotoa ajira za muda mfupi (na wakati mwingine za kudhalilisha). Labda wawekezaji ni wale wajao nyumbani wakafanya harusi za mamilioni na kualika vikundi vya ngoma kucheza na kuwalipa (japo kwa usiku mmoja).
Kama Naibu Waziri anasoma blogu za picha, maoni ya ma-anon na kudhani kila aandikaye "Mdau-US" ama "Mdau-UK" ni mtu aliye nje ya nchi, namshauri afanye uchunguzi kabla hajasema.
LAKINI HAKUNA LA KUSHANGAZA. Kwani analofanya Naibu Waziri ni kukwepa umuhimu wa utekelezaji wa majukumu yake. Wengi twajua kuwa kwa wanasiasa, mambo mengi hutafsiriwa tofauti. Kwa hiyo "kulalamika" anakokuzungumzia kwaweza kuwa kwa namna nyingi na kwa kuwa anataka kukimbia ukweli kuhusu mahitaji na suluhisho la matatizo linaloelezwa na wananchi, sitashangaa kusema nasi twalalamika.
MIFANO.
LAWAMA za wananchi mbele ya watawala wetu, ni ukweli wa uhitaji wa wananchi
Wananchi "wamelalamika"
juu ya uwezo wa mTanzania (anayestahili kuwa wa kawaida) kufanya harusi ya mamilioni ya pesa ilhali shule (za mahala atokako na anapoeleza kupajali) hazina hata madawati na zenye madawati hazina lolote la kuwafanya wanafunzi"watamani" kwenda, kuwepo ama hata kuifikiria shule. Mazingira ni hafifu na hatari.
Wananchi wamelalamika na hata blogu hii "imelalamika" na kuandika kuhusu huduma mbaya za afya hasa kwa kinamama na watoto
Wananchi wamelalamika na blogu hii "ikalalamika" kuhusu maji yenye sumu yanayomwagwa kwenye vyanzo vywa maji ya kunywa kama haya yaliyoonekana kutiririka katika Mto Mzinga huko Mbagala
Wananchi wamelalamika na blogu hii "ikalalamika" kuhusu hali mbaya ya uchumi Wananchi wamelalamika na blogu hii "ikalalamika" kuhusu mgao wa umeme
Wananchi wamelalamika na blogu hii "ikalalamika" kuhusu nyongeza ya mishahara ya wabunge Wananchi wamelalamika na blogu hii "ikalalamika" kuhusu wazee wa Jumuiya ya Afrika Mashariki kutolipwa pesa zao kwa miaka 33, ilhali bunge lilivunjwa Julai na mamilioni ya pesa yakawa kwenye akaunti Agosti. Labda mambo ambayo Mhe Naibu Waziri amesahau ni kuwa ALITAKIWA KUANZA KAZI KWA KUTUELEZA ATAFANYA NINI, VIPI, LINI NA MATOKEO YATAKUWA NINI. Huo ni kati ya UBUNIFU ambao tulitaraji toka kwake
Tulitaraji Mhe Naibu Waziri asiwe mbunifu katika kulalamikia walalamikaji wasio wabunifu, bali atueleze (kama Naibu Waziri wa Seriali ya Muungano)
-Ni vipi atafufua viwanda vinavyokufa nchini.
-Ni vipi bidhaa zinazozalishwa na VIWANDA VYA TANZANIA vitaweza kukidhi UBORA WA KIMATAIFA na kukabilianba na GHARAMA ZA UENDESHAJI iwapo gharama za umeme ndio hizo zinapaa kwa zaidi ya asilimia 10?
-Ni vipi atahakikisha uhakika wa "rasilimali" kwa viwanda na biashara za nyumbani?
-Ni vipi wale waishio karibu na viwanda vikubwa watanufaika na uwekezaji wa mabepari hao
-Ni vipi atahakikisha vibarua wa awali katika viwanda na biashara ni wale ambao wanaishi mazingira ya kuzunguka viwanda na Biashara hizo
-Ni vipi wanaoishi karibu na mazingira ya viwanda na biashara wataboreshewa makazi yao badala ya kumwagiwa sumu toka viwandani
-Ni vipi rasilimali muhimu kama maji adimu kwa wananchi hazitatumika kupoza mitambo ya viwanda na kuwafanya wananchi wakose maji

Licha ya yote, na tofauti na yeye, bado twaendelea kupongeza, kufarijika na kushawishika na mchakato wa Mhe Naibu Waziri katika kuboresha maisha ya wakaazi wa jimbo lake la Singida Kaskazini kwa kampeni yake aliyoanzisha ya OPERESHENI ONDOA TEMBE.

Photo Credit: Mpoki Bukuku.
Labda nimalizie kwa kukumbusha yale ambayo nilishaandika kwenye bandiko langu la UJINGA WA KUKIMBIA MIDAHALO, ambapo nilimnukuu Lucky Dube akisema "We are the soldiers for righteousness. And we are not sent here by the politicians you drink with. We' re sent by the poor. We' re sent by the suffering. We' re sent by the oppressed"
Ni ukweli huo ambao twauona na kuusimamia sasa. Ni ukweli huo tutakaoutumia kuwawajibisha waheshimiwa mliongia madarakani na naamini hakuna ubishi kuwa KWA KILA JEMA MTAKALOTENDA TUTAWAPONGEZA NA KWA KILA BAYA MTAKALOTENDA TUTAWAKOSOA. Nasema KUKOSOA na sio KULALAMIKA.
Na naamini kukosoa kwa kutoa sehemu ya suluhisho NI UBUNIFU

Tuesday, November 30, 2010

Kosa la kwanza la Rais Kikwete......

ONYO: Usisome kama nia yako ni kusoma sio KUELEWA. Rais Jakaya Kikwete akihutubia taifa punde baada ya kuapishwa kuongoza nchi kwa awamu ya pili. Photo credit: Chingasite
Ni kweli kuwa UCHAGUZI UMEMALIZIKA na sasa ni harakati mpya za kuanza KUIJENGA Tanzania yetu katika muhula wa mwisho wa awamu ya nne ya uongozi wa Taifa.
MOSI nirejee ambayo nilishasema awali, NAWAPONGEZA woote walioshiriki katika mchakato wa kumsaka "kiongozi bora" atakayeleta mabadiliko yenye manufaa kwa wananchi.
Shukrani kwa
1: Walioshinda kushinda,
2: Walioshinda kushindwa (ambao wamefanya "juu chini" kutangazwa washindi)
3: Walioshindwa kushinda
Haijalishi "umeangukia" katika kundi gani hapo juu, lakini utakuwa umepata changamoto nzuri ama katika kutekeleza utakiwayo kutekeleza sasa kwa wananchi waliokuchagua, ama katika kujipanga upya kwa uchaguzi ujao kwa wanaopanga kugombea tena.

PILI, nieleze kuwa kumekuwa na MATUMAINI YA MAFANIKIO katika muhula huu. Na matumaini haya yameonekana kuwa makubwa sana. Watu wengi wametabiri UTENDAJI katika awamu hii kwa kuwa wamewekewa watu ambao hawakuwemo katika mfumo wa uongozi uliopita. Kwa maana nyingine, BUNGE LA SASA LINA MABADILIKO KIDOGO na hasa mabadiliko yaliyohusisha "kuanguka kwa vigogo" kadhaa wa chama tawala ambao hakuna aliyetaraji wangeng'olewa kirahisi na watu wa upinzani. Ilishangaza wengi kuona wagombea wa chama tawala licha ya kuwa na "viwezeshwa" vya hali, mali na "mfumo", bado waliweza kukosa nafasi walizozipigania kwa nguvu. Lakini TAFSIRI YAKE SI NGUMU.... WATU WAMECHOSHWA NA VIONGOZI WASIOWAJALI.
Lakini kwa wale ambao wanadhani "ndugu hawa" walioenguliwa ama kunyimwa ridhaa ya kwenda bungeni ndio wamekwisha kisiasa, wanastahili kufikiria mara ya pili.
Tumeanza kuona harakati za Raisi kutumia HAKI YAKE YA KIKATIBA kuteua wasaidizi wake katika nyanja mbalimbali ili kutekeleza kazi zake. Tumeshaona uteuzi wa BARAZA LA MAWAZIRI ambalo kwa heshima na taadhima niliwaomba MAWAZIRI WAORODHESHE WATATENDA NINI, VIPI NA KUFIKIA LINI? (Irejee hapa). Sijajua VIGEZO vya uteuzi huo, na wala sina hakika kama katika vyeo vya kuteuliwa kuna ambacho kina "udogo" wa utendaji ukilinganisha na ubunge. Najua wakuu wa mikoa (ambao kama nilivyosema hapa nawaona kama MZIGO KWA SERIKALI NA WANANCHI na CHANZO CHA KUDIDIMIA KWA MAENDELEO NCHINI), na pia kuna wakuu wa wilaya, kuna makatibu wa wizara, wabunge wa kuteuliwa, mabalozi n.k. Na pia tumeona ambavyo Mhe Raisi ameanza kwa kuteua wabunge ambao mmoja wa wateuliwa AMEZUA GUMZO (hapa) kutokana na kuhusishwa na tuhuma ambazo bado hazijathibitishwa kwa wananchi.
Lakini bado nawaza kama Waheshimiwa wastaafu kama Mhe. Lawrence Masha, Mhe Monica Mbega, Mhe Phillip Marmo, Mhe Getrude Mwongela, Mhe Batilda Buriani na wengine wengi hawatanyakua nafasi za kuteuliwa. Ninawaza pia kuwa kama niko sahihi (kwamba hakuna cheo cha kuteuliwa chenye udogo wa shughuli kuliko ubunge), ni kipi kitamfanya Mhe Raisi ateue watu ambao wameshindwa kuwatumikia wananchi wao ilhali wanajua fika kuwa watakuja kuwaomba kura miaka 5 ikiisha? Kama watu hawa walipuuza NGUVU YA KURA YA WANANCHI mpaka yalipowakuta ya kuwakuta, ni vipi watawajibika ilhali wanajua atakayewateua hawatamuomba kura na hataenda tena kwa wananchi kuomba kura kwa kuwa muhula wake umeisha?
SINA HAKIKA KAMA RAISI ATATEUA YEYOTE KATI YA "WALIOSHINDWA KUSHINDA" UCHAGUZI lakini pia sitashangazwa na hili japo nitasikitika sana.

Na katika kumalizia sentenzi iliyo kichwa cha habari hii, nasema.......
KOSA LA KWANZA LA RAISI KIKWETE LITAKUWA NI KUPUUZA NGUVU NA MAONI YA WANANCHI YA KUTAKA MABADILIKO IKIWA ATAWATEUA WATU WALIOSHINDWA KATIKA UCHAGUZI ULIOMALIZIKA.
Hili litakuwa kosa kama atateua yeyote kati ya walioshindwa na halitakuwa kosa mpaka atakapotekeleza kile ninachoona kina uwezekano wa kutendeka.
Mpaka wakati huo, naendelea KUFUNGA NA KUOMBA kwamba Mheshimiwa Raisi aheshimu matakwa, nia na haja ya mabadiliko iliyooneshwa na wananchi.

Na hivi ndivyo nionavyo tatizo lijalo na natunza haki ya kukosea na kukosolewa. Labda namna nionavyo tatizo ndilo tatizo.

Tuonane "NEXT IJAYO"

Thursday, November 25, 2010

Nionavyo mimi....MAWAZIRI WAORODHESHE WATATENDA NINI, VIPI NA KUFIKIA LINI?


Hakuna ambaye hajasikia BARAZA JIPYA LA MAWAZIRI lililotangazwa jana na Mhe Raisi Kikwete. Maoni juu ya baraza hilo ni mchanganyiko na wapo walioonekana "kulikubali" na pia waliolipinga ama kutoridhishwa nalo.
Wengi wa waliolikubali wameonekana kukubali zaidi uteuzi wa Mhe John Magufuli na Mhe Anna Tibaijuka katika wizara zao. Ni jambo la kufurahisha kuona BARAZA LINAUNGWA MKONO na wananchi. Kuna imani ama matarajio kwamba KUTAKUWA NA MAFANIKIO kutokana na kuungwa mkono kwa baraza hili. Hizi ni dalili njema.
LAKINI pia kuna walio na shaka. Wanaosema "wengi ni walewale" na wanahisi "ushikaji" umetawala uteuzi huu..
Wacha nami nianze kuweka yale nilonayo moyoni.
KWANZA niwapongeze wanaomuunga mkono Raisi (kwani hata bila kumuunga mkono baraza "litasonga"). Na pia wale wanaopongeza uteuzi wa Mama Tibaijuka niungane nao, lakini pia NIONYE AMA KUTAHADHARISHA kuwa Mama Tibaijuka ANAINGIA KWENYE MFUMO (pengine uliomomonyoka) AMBAO UNAWEZA KUWA KIGINGI KATIKA UTENDAJI WAKE. Bado naamini kuwa utendaji wa Umoja wa Mataifa ulikuwa na mazingira mazuri ya kazi yasiyo na mchanganyo na mkanganyo wa siasa kama ilivyo Tanzania yangu. Natumai watu watakaokuja kuangalia uongozi wake wataliweka hili katika fikra.
Ni hapa ninaporejea kwenye mada kamili kuwa
KABLA HAWAJAJITAMBULISHA KWETU KAMA MAWAZIRI, NINAPENDA WAJIPANGE NA KUANGALIA NI NINI WATATIMIZA KATIKA MIAKA MITANO IJAYO NA NI VIPI WATATIMIZA HAYO KWA KUFUATA ILANI YA CCM.
MAWAZIRI hawa wanalazimika kuwa na mipango kamili. Ninachukia kuona kila miaka mitano iishapo, tunalinganisha utendaji kazi wa mtu kwa kitu tusichokijua. Sasa watueleze ni nini tutarajie miaka mitano ijayo na kisha watupe mgawanyiko wa namna watakavyotimiza hayo kwa kufuata ilani za CCM. Wananchi WANA HAKI ya kujua utekelezaji wa AHADI HIZI ZA RAISI KIKWETE.
TOVUTI ZA WIZARA KUFAFANUA KAZI ZAO...Mhe. RAISI...ATI UMESEMA WIZARA YA MAHUSIANO NA URATIBU? Labda TOVUTI ZA WIZARA zitafafanua ni nini wizara inafanya ama inastahili kufanya. Hii Wizara ya Mahusiano na Uratibu ningependa kujua inahusika kuhusianisha na kuratibu nini? Pia "Mchanyato" wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo unatuelekeza wapi? Na katika TAARIFA YA MAREKEBISHO YA WIZARA KUTOKA MWANDISHI MSAIDIZI WA RAISI imesema "wizara ya vijana imehamishwa kutoka wizara ya kazi na kuihamishia wizara ya habari kwa sababu kuu mbili. Kwanza ni kushahabiana na michezo na utamaduni,...." NINAWAZA KUHUSU MSHAHABIANO HUU. Ni kweli kuwa katika yote yawafaayo na kuwahusu vijana, Ikulu imeona mshahabiano wao na Michezo na Utamaduni tu? Si Elimu, si Sayansi na Teknolojia, si Afya, Si Uwekezaji, Si Maendeleo ya Jamii, si Utawala Bora, si Uchumi, si Utalii, si Madini, si mafunzo ya jamii si, si, si ........?
Ningependa zaidi kujua zaidi kuhusu hili
AJALI ZA BARABARANI. Ni nani atakayechukua jukumu la kushughulikia kuzuia ajali na kuratibu usalama wa wananchi? Je! Ni Wizara ya Ujenzi (Barabara na Uwanja wa Ndege), Wizara ya Uchukuzi (Reli, Bandari, Usafiri Majini) ama Wizara ya Usalama wa Raia (ambayo hata sijui imekuwa "faded" ndani ya wizara ipi? Ama ni wizara gani?
WIZARA YA UCHUMI??? Nilipowasiliana Kaka Jeff Msangi na awaza kama wizara ya fedha ndiyo ishughulikayo na masuala ya uchumi. Ama mchakato wa uchumi ama uharibifu kutokana na madini utasimamiwa na Wizara ya Fedha, wizara ya Madini ama Wizara ya Mazingira?
Kuna mengi ya kuwaza na kuchangia kuhusu baraza hili ACHILIA MBALI KUWA NA WANAWAKE 9KATI YA BARAZA LA WATU 50.

"Wacha niachie" hapa, naamini nawe utaona la kuongeza katika kuisaidia TANZANIA YANGU ISONGE MBELE
Tuonane "Next Ijayo"

Wednesday, November 24, 2010

Kwenu wapinzani. Ms'ojua ushindani na kukalia ukinzani uwageuzao "washindwani"

Photo Credit: Alternatives-Economiques Blog
Nilisikia msemo kuwa the moment you discover the "cool", is the same moment the "cool" thing loses it's "cool". Nikaambiwa haya hutokea zaidi katika biashara. Kwamba unapodhani umegundua kile ambacho hakijagunduliwa, kisichopatikana na kilicho "cha pekee", ni wakati huohuo ambao unafungua milango kwa "waigilizaji" walio wengi kukimbilia hapo na matokeo yake ule mfumo wa "supply vs demand" unafanya kazi yake.
Labda suala hapa ni lile lile kuwa HAKUNA NAMNA YA KUDHIHIRISHA KUWA UNAWEZA KUTUNZA SIRI, KWANI NI LAZIMA UISEME ILI MTU AJUE NI IPI ILIYOKUWA SIRI NA UKISHAISEMA UMESHAPOTEZA KILICHOKUFANYA UJIVUNIE...U-SIRI.
Bahati mbaya ni kwamba mifano hii ya kibiashara inaonekana kuwafikia hata "wafanyabiashara wa siasa" nchini Tanzania.
Yaani punde baada ya waTanzania kuamini kuwa WAMEWEKA UPINZANI HALISI BUNGENI, wale "wengine" wenye kuendekeza maslahi zaidi ya wananchi wamerejea kwenye upande ambao unawafanya wananchi wazidi kukubaliana na tafsiri ya Da Subi ya siasa kuwa "siasa si-hasa, bali visa na mikasa".
Tulianza kuyaona mapeeema baada ya uchaguzi pale tulipokubaliana kuwa yawezekana "Ni kweli Dk Shein kashinda..lakiniii..... labda Maalim Seif hajashindwa pia" (irejee hapa) na kikubwa tulichowaza hapo ni kama "kukubali" huku kuliendana na mahitaji ya wananchi ama mahitaji binafsi ya Maalim Seif ambayo hayakutimizwa katika chaguzi tatu zilizopita. Kisha likaja suala la kutangazwa uongozi wa upinzani Bungeni (hapa) ambapo tuliambiwa bayana kuwa "Vyama vingine vya upinzani vyenye wawakilishi Bungeni, TLP, CUF na NCCR-Mageuzi vimekataa kujunda ushirikiano na CHADEMA na badala yake, vinatarajiwa kutangaza safu yao baada ya makubaliano."
Hatujatulia, tukasikia kuhusu wapinzani kutaka kupelekana mahakamani kwa sababu za kampeni ya Kawe na sasa twaona vita ya "demokrasia" inaendelea.
SUALA HAPA SI NANI ANAFANYA NINI, BALI NI NANI NA NANI WANAPINGANA NA KUPIGANIA NINI?
Ni maadui wangapi ambao upinzani wanao na ni wangapi ambao wanaweza kuwa na namna mija ya kuwaondoa? Kama ni MARADHI, UJINGA, MALAZI NA MAISHA DUNI YA WANANCHI, ni kwanini WAKINZANI hawa hawaungani kuwateketeza?
Kama wote ni waenguka wa chama tawala na wanataka kufanya kile kinachozembewa kufanywa na chama tawala, ni kwanini wanashindwa kutafuta palipo na msimamo wa pamoja, wakaungana na kisha wakaweza kumng'oa huyo wapangaye kumng'oa?
Sasa yaonekana "vita dhidi ya matatizo ya wananchi" (ambayo ilistahili kuanza) ndio imekwisha (mpaka mwezi Juni 2015) na sasa ni "vita" ya kusaka umaarufu kwa migongo ya wenzao.
Hivi ni kweli "umoja" unatakiwa kuwepo wakati kila mmoja anasaka UTAWALA?

Sasa na huu ni ujumbe "Kwenu wapinzani. Ms'ojua ushindani na kukalia ukinzani ufanyao 'washindwani'", watu wanataka mabadiliko. Mkanganyiko wa nani anafanya nini kwa manufaa ya fulani na si wachagua si mwema. Hauzifai jamii zilizowaweka madarakani huko bungeni, wala hauifai nchi yetu kwa ujumla. Ni lazima mkumbuke kuwa nyote mwafanya harakati za kusaka maendeleo, lakini cha kusikitisha ni kuwa MWASAKA MAENDELEO KWA KUDIDIMIA UENDELEZI. Yaleyale NILIYOANDIKA HAPA
Kama ulikosa kilichoimbwa, sikiliza na kufuatilia mashairi yake chini.

"Listen people to a story that was written long ago,
Bout a kingdom on a mountain and the valley folks below
On the mountain sit a treasure, buried deep beneath the stone
And the valley people thought they'd have it for their very own.

Chorus
Go ahead and hate your neighbor, go ahead and cheat a friend
Do it in the name of heaven, you'll be justified it in the end
There won't be any trumpets blowing On the judgment day
On the bloody morning after one tin soldier rides away.

So the people of the valley sent a message up the hill
Asking for the buried treasure, tons of gold for which they'd kill
Came an answer from the mountain, "with our brothers we will share
All the secrets of our mountain, all the riches buried there."

Now the mountain cried with anger, "Mount your horses, draw your swords"
And they killed the valley people, so they won their just rewards
Now they stood beside the treasure, on the mountain, dark and red
Turned the stone and looked beneath it, "Peace on earth" that all it said.

Chorus
Go ahead and hate your neighbor, go ahead and cheat a friend
Do it in the name of heaven, you'll be justified it in the end
There won't be any trumpets blowing, On the judgment day
On the bloody morning after, one tin soldier rides away.".... x2

Kama huoni player BOFYA HAPA

Saturday, November 20, 2010

WALIOGOMEA MIDAHALO....Wengi wao ama wana UJINGA, ama wamejawa DHARAU

ONYO: USISOME HAPA KAMA
1: WAKASIRIKA KABLA YA KUFIKIRI
2: UNAAMUA KISHA UNAFIKIRIA ATHARI
3: HUPENDI KUJUA UKWELI HATA KAMA UKWELI NDIO UPENDO

"Speak the truth and speak it over. Love God and leave, is my only destination." NASIO
Tafsiri ya UJINGA niliyonayo ama niliyoambiwa (na ambayo naisimamia) ni ile isemayo kuwa mjinga ni MTU ASIYEJUA, NA ANAJUA KUWA HAJUI. Kwa tafsiri hii, ina maana UJINGA ni hatua moja bora kutoka UPUMBAVU na iliyo rahisi kuirekebisha kwani aliye mjinga anaweza kurekebishika akiamua kuufanyia kazi ujinga wake.
Ina maana kwa tafsiri hii ya Ujinga, naamini kuwa wabunge wa CCM (ambao waligomea midahalo) walitambua wazi kuwa walitakiwa kueleza sera zao kwa wananchi na kuzipambanisha ili kuweza kuwapa nafasi wananchi kutambua aliye bora kwao. Lakini KWA AMRI TOKA LUMUMBA (makaoni mwa chama), tena toka kwa watu ambao hawajui mahitaji ya asilimia kubwa ya wananchi, wagombea hawa WAKAKACHA midahalo kwa kisingizio cha kuwafuata wananchi huko walipo. Suala si kuwafikia, bali ni KUWAPATIA ALIYE BORA KWA MATATIZO YAO. Na nina hakika wale WALIOOGOPA midahalo walikuwa hawajui namna ya kuwakomboa wananchi wa na walijua fika kuwa hawajui (rejea tafsiri ya ujinga) na kwa kuwa wao hawakuwa pale na hawako pale kumfaa mwananchi zaidi yao wenyewe, wakaona wafanye lililo bora kwao nalo ni kupanga mikakati ya kuchaguliwa hata kama hawatakuwa na manufaa kwa wananchi wao kama wale ambao wangepambanisha nao sera.

Kinachokera zaidi ni namna WANAVYOJIDAI kupata "ushindi wa kishindo" na kusingizia kuwa ushindi huo watokana kukubalika kwao. Hawa watu wanajisifia kufaulu bila kufanya mtihani. Ama kwa uhalisia zaidi niseme wanajivunia KUSHINDA KWA "KUTAZAMIA".
Nafarijiwa na Nasio Fontaine ambaye katika wimbo wake DANGEROUS (usikilize mwisho wa post hii) aliimba akisema "...i heard your speeches,... your empty promises (promise is a confort to a fool), but now that i know, your words are dangerous"
Lakini siamini kuwa wabunge wote wako hivyo. Siamini kama wote hawakuwa na suluhisho la matatizo ya wananchi. Siamini kuwa wote walikuwa hawapendeki. Siamini kuwa wote ni WAJINGA. Ila kwa wale wasio na sifa hizo mbaya hapo juu, na ambao wangeweza kuwadhihirishia wananchi kuwa wao ndio wanawafaa na wakaamua kutofanya hivyo basi hakuna ubishi kuwa WAMEWADHARAU WANANCHI WAO

Wameona hakuna haja ya kutekeleza haki ya kikatiba ya wananchi kwa kuwapa nafasi ya kuchuja kile waaminicho na wafikiriacho ukilinganisha na wenzao. Hii si dharau kwa wananchi tu, bali kwa nchi.
Na kama nilivyoonya hapo awali, usisome hapa kama huna KIFUA cha kuukubali ukweli. Na huu ni ukweli toka katika upande wa wahitaji, upande wa wasio na tumaini na upande ambao ulikuwa na imani na watawala hawa. Kama alivyosema Lucky Dube kwenye wimbo wa SOLDIRES FOR RIGHTEOUSNESS kuwa "We are the soldiers for righteousness. And we are not sent here by the politicians you drink with. We' re sent by the poor. We' re sent by the suffering. We' re sent by the oppressed"
Ni ukweli huo ambao twauona na kuusimamia sasa. Ni wakati wa kuwawajibisha waheshimiwa mliongia madarakani na naamini hakuna ubishi kuwa KWA KILA JEMA MTAKALOTENDA TUTAWAPONGEZA NA KWA KILA BAYA MTAKALOTENDA TUTAWAKOSOA. Kama isemavyo fulana hii hapa chini, tunasimama katika kilicho sahihi na si kuendekeza "mapinduzi" ya wasiojua uhitaji wa wahitaji wao.
Labda niwe wazi kuwa, sasa ni wakati ambao tutaanza KUWEKANA SAWA na kurekebishana hasa katika kipengele (label) hii ya POLITICS FIX (kama ambavyo nataraji mnirekebishe) na hii itakuwa ni njia moja muafaka na muhimu katika kulikomboa taifa.
Na kwa WABUNGE VIJANA, wale wapya ambao mlionekana kuwa na "UJANA WA MAWAZO" mtambue kuwa kuwepo kwenu hapo kumekuwa tumaini kubwa kwa wengi, kwa hiyo kushindwa kuwakilisha vema na kujikuta mnaingia katika "MFUMO WA UZEE WA MAWAZO" ULIOWACHOSHA WANANCHI mtajishushia imani kwao. Japo wapo ambao mmeshaanza hilo.
Mfano mzuri ni mwanablogu ninayeheshimu kazi zake aliyegeuka kuwa m'bunge Dr Faustine wa Faustine Baraza ambaye sasa ni m'bunge wa Kigamboni, alikuwa mkosoaji mkubwa wa matendo ya serikali na chama, aliandika kuhusu ziara za Rais na mambo mbalimbali, lakini alipoingia kwenye kinyang'anyiro cha Ubunge akaamua kuifunga blogu ambayo aliitumia kuanika uozo wa "WENZAKE WA SASA." Ukurasa wake huu hapa ulio na kumbukumbu za aliyokuwa akiyasema akiwa nje sasa umewekewa KUFULI. Nilipomuuliza katika ukurasa wake wa Facebook alinijibu kuwa alikuwa amebanwa na mambo ya kampeni lakini angeurejesha hewani punde. HAKUTIMIZA AHADI YAKE. Sasa kafungua ukurasa mpya ambao naamini utaendana na matakwa ya watawala wake kuliko wananchi aliokuwa akiwatetea kwa dhati.
NI WAKATI WA KUWEKA MBELE MASLAHI YA WANANCHI NA SI CHAMA
Tumsikilize Nasio akitukumbusha kuwa THEIR WORDS ARE
DANGEROUS

NA HIVI NDIVYO NIONAVYO TATIZO. NAMI NATUNZA HAKI YA KUKOSEA NA KUKOSOLEWA.LABDA NAMNA NIONAVYO TATIZO NDILO TATIZO