Wednesday, October 24, 2012

"You're what you eat"

Msemo huu tumekuwa tukiusikia sana.
Na pengine umekuwa kama KAWAIDA masikioni mwetu.
KWANINI?
Kwa sababu madhara ya vile tunavyokula hayaonekani ndani ya muda mfupi.
Wanaadamu tumekuwa waoga wa kile kituathiricho sasa na si siku, wiki, miezi ama miwaka kadhaa ijayo, japokuwa pale tunapopata madhara, tunajutia kila tulichotenda katika siku, wiki, miezi na miaka hiyo.
Nirejee kwenye CHAKULA.
Natambua watu wengi hufurahia aina za vyakula wanavyonunua madukani. Kuku wa "kizungu", ng'ombe wa "kisasa" na mengineyo mengi.
LAKINI JE, UNAJUA WANAKOTOKA? UNAJUA WANAVYOKUZWA, KUCHINJWA NA KUTAYARISHWA MPAKA WANAPOKUFIKIA?
Kwa wale wanaoishi maisha yasiyo na vyakula asili, HAKUNA UJANJA, lakini kwa wewe unayeamini kuwa CHA ASILI NI "USHAMBA", FIKIRIA MARA MBILI.
Karibu utazame DOCUMENTARY hii iliyokuwa ikzungumzia UTATA WA MASLAHI KATI YA AFYA NA UBEPARI.

No comments: