Tuesday, November 25, 2008

Maoni ya mchambuzi Kaluse katika Majina.

Kutokana na mazoea kuna ukweli juu ya hilo( la majina kuathiri mstakabali wa maisha yetu.). Niliwahi kufanya utafiti wakati fulani juu ya dhana hiyo, nikaja kugundua kuwa majina yamepewa nguvu kutokan na watu kuamini katika hizo imani. Kiutambuzi jambo lolote likipewa nafasi katika jamii na kuaminiwa linakuwa na nguvu, ndio sababu ya watu wengi habudu mizimu na kwendakutambika katika makaburi kwa kuamini kwamba mambo yao yataanyooka, na hii inahusisha hata wale watu walioshika dini. Kwa kuwa wameaminishwa kwamba bila kutambikiamizimu hakuna kufanikiwa, basi dhana hiyo inakaa kwenye ubongo wa kina na hapo ndipo imani hiyo inapokuwa na nguvu kwelikweli. Kwa mfano uliotolewa na dada Yasinta, yote hiyo ni imani za kutengeneza tu, hakuna ukweli wowote.Kwangu mimi jina ni jina hakuna jina baya balitafsiri zetu ndio mbaya. Nimeshangaa kumsikia mwana utambuzi mwenzangu Kamala kwamba ilibidi aachane na jina lake la ubatizo kwa sababu eti lilikuwa halimfai, kwa bahati mbaya hakusema kwamba lilikuwa halimfai kivipi? kama angesema lilikuwa na mkosi, ningejua nimsaidie vipi mwanutambuzi mwenzangu lakini hakutoa sababu.Ipo mifano mingi inayodhibitisha nguvu hizi za kutengeneza>Kwa mfano Nchini Marekani, wanaamini kwamba mtu hawezi kupata Urais kama jina lake halina herufi G, O au W, na ndio sababu ukichunguza marais waliotawala katika nchi ile majina yao hayakosi herufi hizo. Na hapa nchini kwetu inaaminiwa kuwa Herufi M ndio inatawala, kwa hiyo ukichunguza marais wetu wote majina yao yana Herufi M.MWALIMU JULIAS KAMBARAGE NYEREREALI HASSANI MWINYIBENJAMINI WILLIAM MKAPAJAKAYA MRISHO KIKWETE.Na hata kwa upande wa mawaziri wakuu ni hivyo hivyo.Naomba kuwasilisha.
Mtambuzi, Shabani Kaluse

Shabani Kaluse ni Mtambuzi anaye-blog habari za kina juu ya utambuzi kupitia blog yake unayoweza kuitembelea kwa kubofya hapa

No comments: