Saturday, November 29, 2008

Them, I, & Them. MORGAN HERITAGE ......... A Man Is Still A Man

Nikiwa na Gramps Morgan baada ya onesho lao la kutangaza albamu yao mpya ya Mission In Progress.
"A man is still a man whether him wear jacket and tie, or walk barefoot.The only difference is whether him good or evil.
A man is still a man whether him rich or poor black or white for sure.The only difference is whether him good or evil."
Pengine liwe funzo kuwa hatuwezi kuwaweka watu kimakundi kwa mwonekano wao wa nje. Ni yale wawazayo na kutenda na namna yanavyoathiri jamii ndivyo tunavyoweza kuwaweka katika makundi makuu mawili ambayo ni watenda mema ama mabaya. Hapa Morgan Heritage wanatukumbusha kuwa maisha ama namna tuendeshavyo maisha yetu na kupata kipato chetu cha kila siku si sababu ya kuwafanya wengine wadharauliwe ama wengine kujiona bora zaidi kwa kuwa tu wanafanya kazi masaa machache na muda ambao kila mtu anautamani. Ndivyo Jah Petes asemavyo kwenye ubeti wa kwanza kuwa "Lots of different people on the streets wiping car glass windows. This is what they do day to day just to get a little food to eat. Then you have others wearing suit and tie, work a good nine to five. And they take it for granted that they're living a better life" Ni kote kote duniani ambako kuna watu ambao hawawathamini watu kwa vile tu maisha yao ni "mema" zaidi ya wenzao. Ni jambo ambalo wengi wanasahau kuwa aliyewapa wao ndiye anayeendelea kufungua milango kwa wengine wanaoonekana kama hawana (sijasema amewanyima wengine), na kuwa kila mtu ana namna amzidivyo mwenzake katika mambo fulani mbele ya jamii fulani. Tutambue kuwa tofauti za rangi ya ngozi zetu hazimaanishi lolote juu ya yale tuwezayo kutenda kwai sote twaamuliwa na Mungu mmoja, hivyo twastahili kuchunga yale tutendayo kwa wale tusiowajua. Petes anaendelea kusema "I say the color of our skin don't mean a thing if we do good or commit to sin.We're all judged by the same, and Jah is his holy name.So lets all be aware of how we entertain angels unaware.For angels do move through men, whether here or from there". Kwa hiyo bila kujali Daraja la Maisha, Imani wala Rangi za mwili wetu, twapaswa kutambua kuwa tuna jukumu la kuishi maisha sahihi yenye heshima na kuwajali wengine kwa kuwa sote tu sawa mbele ya macho ya Muumba. Na haya ndiyo asemayo Gramps anapoimba kwenye "bridge" kuwa "Everyman has freedom, ya.For the wealth of a man. Be sure when living life. We treat all men right.For we are all of the same. In the MOST HIGH'S EYES"
Ni vema tukajifunza kuwathamini na kuwaheshimu watu FOR WHO THEY'RE AND NOT WHAT THEY ARE sababu the only Difference is whether them good or evil
Bofya Player hapa chini kusikiliza wimbo huu.

**Them, I & Them ni kipengele kikujiacho kila Ijumaa kinachoelezea kazi za wasanii (Them) kulingana na maono yangu (I) kwa ajili na manufaa ya hadhira (Them)**
Kwa nyimbo zaidi ndani ya kipengele hiki bofya hapa.
IJUMAA NJEMA

No comments: