Friday, September 4, 2009

Them, I & Them... YOUTH TODAY......Morgan Heitage

Ndugu watano (Nyuma L-R) Lukes, Gramps, Jah Petes (Mbele L-R) Una na Mr Mojo Morgan wanaounda kundi zima la Morgan Heritage a.k.a ROCKAZ. Watembelee HAPA
Nimekuwa nikisema kuwa MPAKA KESHO ItAKAPOHESABIKA KUWA LEO, BASI VIJANA HATUTAENDELEA. Maana kubwa ya sentensi yangu ni kuwa mambo ya msemo wa VIJANA NI TAIFA LA KESHO hauna maana.
Hauna maana kwangu kwa kuwa wazee wanaendelea kung'ang'ania madaraka mpaka vijana wanapoelekea kuuacha ujana na wakati huo ndipo tunapojikuta tumekosa la kufanya. Hakuna ubishi kuwa wazee wengi na hasa kwenye siasa za nyumbani wana uzoefu, lakini tusisahau kuwa "The trouble with experience is that by the time you have it you are too old to take advantage of it. " — Jimmy Connors
Ndio maana twaona namna ambavyo "wazee" wetu waliojikita kwenye siasa walivyoishiwa na kuanza kutetea yasiyo na maana na yasiyo na tija kwa taifa.
Ni wakati wa VIJANA KUAMKA NA KUANZA KUNYOOSHA MAPITO ya maumivu tunayopitishwa na "waheshimiwa" hawa.
Twaona ilivyo nchini kwetu na Afrika kwa ujumla jinsi vijana wanavyohangaika kwelikweli kutaka "kuiona kesho". Katika hili, tunawasikia Morgan Heritage katika wimbo wao YOUTH TODAY wakilizungumzia hili. Mfano ni hapa mwanzo ambapo Jah Petes anaimba namna ambavyo tunashuhudia yaendeleayo bila kutafuta suluhisho anaposema "How much more do we need to see before we realize we all need to change our lives. For the better world in this time. Now the time has come, let's not wait till it's gone. Don't wait too long". Lakini Gramps katika ubeti wa pili anazungumzia maumivu / mateso ambayo vijana wanayapata kwa maamuzi ambayo hawakushiriki kuyafanya na kisha anahimiza kuwa hakuna wa kulamu bali kuamua na kuungana kuyafanyia kazi mabadiliko. Anasema "now the youth they feel the pain, for the choices made yesterday, there's no one out to blame we all have to work towards the change"
Basi ni wakati ambao lazima VIJANA TUAMKE na kuacha kutegemea waliopitiliza kwenye nafasi ambazo hawana uwezo wa kuzishikilia. Wanatapatapa na kuhaha na ssi (bila kujijua) tunatapatapa tukiwafuata wao. Hivi unajua athari ya kumfuata asiyejua aendako? Unajua anakoweza kukufikisha kama utaendelea kumfuata ilhali yeye anaendelea kukukimbia na kutafuta pa kujificha? Tunapowaona wao kama "milima" ilhali milima inatafuta bonde la kujificha (kwa kuwa wameshaishiwa) basi ujue TUNAAIBIKA. Ndio anayofungia nayo Jah Petes anaposema
"see someone looks a hills to run to,
the youths a look somewhere to run to,
see someone looks around to run to,
the ROCKAZ looks somewhere to run to,
see someone looks a mountain top to run to, the mountain looks somewhere to run to
See someone runs out of space, what a big disgrace"
Wasikilize Morgan Heritage hapa katika kibao chao mwanana YOUTH TODAY


**Them, I & Them ni kipengele kikujiacho kila Ijumaa kinachoelezea kazi za wasanii (Them) kulingana na maono yangu (I) kwa ajili na manufaa ya hadhira (Them)**
Kwa nyimbo zaidi ndani ya kipengele hiki bofya hapa.
IJUMAA NJEMA

5 comments:

kamala Lutatinisibwa Lutabasibwa said...

eti vijana nitaifa la kesho na umeona chama cha upinzani chdema kinamkataa kijana asiwawekee kiwingu wazee kwani ndo wenye busarazaidi!!!

siasa bwana.il;a nomaipo kwa vijana kubweteka na kusubilia taifa lao la kesho wakati leomambo sio mammb!

Simon Kitururu said...

Swali kwa vijana:

Vijana wa kesho KWA MWENDO HUU hivi mtaifikia kesho?

Ijumaa njema Mkuu!

Yasinta Ngonyani said...

Ninenukuu "Ni wakati wa VIJANA KUAMKA NA KUANZA KUNYOOSHA MAPITO ya maumivu tunayopitishwa na "waheshimiwa" hawa.
Twaona ilivyo nchini kwetu na Afrika kwa ujumla jinsi vijana wanavyohangaika kwelikweli kutaka "kuiona kesho"."Mwisho wa kunukuu.

Ni kweli kabisa wakati umefika tukianza sisi basi inawezekana hilo Taifa la kesho wakapata nafasi lakini bala hivyo basi itaendelea kuwa hivyo na hivyo siku, miezi na hata miaka.

Faith S Hilary said...

Mimi kama kijana or probably still mtoto (lol), you know I think when that "tomorrow" comes, we can do it. Vijana wa jana ambao leo wanafanya mambo makubwa na still wengine wanazidi kukua na kuendeleza mambo waliyoyakuta hapa duniani. And this applies to the whole world.

Kwahiyo jamani, don't give up on us because we can actually do it. Mbona wapo vijana wa zamani na akili zao zilikuwa mbili kidogo, yet where are they now?...Hiyo ndio hoja yangu...kaka unanifanya niongee "too much"...Hahahaha...Lateeeeeer!!

Anonymous said...

omg....jamaican group