Wednesday, May 12, 2010

Shule Shule Shule... Twafunzwa tufunzapo

Nimekuwa "nikihubiri" kuhusu SHULE hii tuiitayo blogu. Ambayo katika kila uandikalo, kuna uandikiwalo ambalo litakuwa na uelimishaji kwa kila mwenye mtazamo chanya. Na kuna wanaojitolea kuelimisha wakiwa wanaficha utambulisho wao, na wengine wanakuja wazi kuelimisha kile wanachoamini na kukielimisha kwa nguvu zote.
Na leo napenda kuleta maoni ya Kaka Evarist Chahali aliyotoa kwenye ileeee mada niliyoandika kuwa Blog zetu na "maradhi" ya Bongo flava (irejee hapa).
Kaka Chahali anaelimisha na kuendeleza mjadala akisema
"Naomba kukupongeza kwa uchambuzi huu makini.Pamoja na pongezi hizo,naomba uniruhusu kutofautiana nawe japo kidogo.Kwa mtizamo wangu (unaoweza kuwa si sahihi) lengo la kuanzisha blogu linabaki kuwa miliki ya bloga husika.Kwa mantiki hiyo,bloga anaendelea kuwa na haki na uhuru wa kuendeleza maudhui ya awali ya kuanzisha blogu yake kama ambavyo anavyokuwa na uhuru wa kubadilika kulingana na sababu mbalimbali (kwa mfano kwenda na wakati,kutanua hadhira,nk).Blogu si Biblia au Koran kwamba kubadili cbochote ni kukufuru.
Pia,tunaweza kuwa hatuwatendei haki bloga 'wanaoendeshwa na kusaka umaarufu,au 'wanaoiga'au 'wanaokurupuka',nk kwa vile kile tunachoita kusaka umaarufu,kuiga au kukurupuka kinaweza kabisa kuwa ni sehemu ya ubunifu wao.Na katika 'kuiga' huko inawezekana wanachofanya ni kufuata mkondo wa vinara wa fani.Tunashuhudia kwenye soka,kwa mfano,wanasoka chipukizi wanavyojitahidi 'kuiga' idols wao kama Beckham,Messi,nk.Kama 'kuiga' huko kunaweza kuzaa maendeleo basi nadhani ni jambo jema.Kumuiga mzee wa changamoto ili nami niweze kuitumikia jamii kiufanisi au haya nikidhi tu mapendezeo yangu si jambo baya (kwa mtizamo wangu).
Halafu,ninahofu kuwa bloga 'wageni'au'wachanga' wanaweza kutuona hatuwatendei haki 'kwa kuhukumu kazi zao'.Wanaweza kujiuliza tumepata wapi mamlaka ya kuunda vigezo vya ubora wa blogu (kwa kuzingatia mazingira yetu).
Sambamba na hilo ni swali nililowahi kujiuliza huko nyuma: tunablogu kwa ajili ya jamii au kwa ajili yetu?Jamii ni mkusanyiko wa watu wenye akili,upeo,ladha na matamanio tofauti,na kwa hali hiyo ni vigumu 'kuiridhisha' yote.Nafsi,kwa.upande.mwingine,ni moja.Ni mimi au wewe au yeye.U-moja huu unarahisisha kuridhika.Ni rahisi kuridhisha nafsi yangu kuliko ya mtu mwengine au kundi.Kwa.mtizamo wangu,alimradi bloga 'hachafui hali ya hewa' basi anaweza kufanya 'ile kitu roho yake inapenda' iwe ni kufuata nyayo ( 'kuiga') nguli wa fani au 'kuja kivyake'.
Binafsi sina tatizo na kukopi na kupasti alimradi huyo 'mkopaji' anaweka angalizo kuwa alichoweka hapo ni kwa mujibu wa au hisani ya flani.Hivi magazeti,radio na televisheni si ndio wanaongoza kwa kukopi habari?Na si kwamba kila mara wanafanya hivyo kwa kupenda bali habari zao nyingi hupatikana kutoka chanzo kimoja,hususan 'wire services'.Si ajabu kukutana na Habari kutoka Reuters au AFP ikiwa kama ilivyo kwenye magazeti,tv,redio na tovuti mbalimbali duniani.Sanasana itakuwa imeongezwa maneno mawili matatu au picha.Nafahamu kuwa neno linalotumika ni subscription lakini kimsingi ni copy and paste.
Tukumbuke kuwa si kila anayeanzisha blogu anataka kuelimisha,kuhabarisha,kuburudisha au kukosoa.Kwa vile kimsingi blogu ni mithili ya personal diary japo kwa mazowea tu inatarajiwa kuwa kama chombo cha habari basi kilicjomo humo kinategemea zaidi matakwa ya mmiliki kuliko sisi 'tunaoamua wenyewe kutembelea diary husika' (pengine diary si neno mwafaka lakini nadhani nimeeleweka).Kama kilichomo humo hakiendani na ladha,matarajio au matakwa yetu,tunaachana na diary hiyo.
Nimalizie kwa changamoto ndogo.Ukitafuta blogu zinazojihusisha na teknolojia ya android,kisha ukatembelea japo 20 tu,naamini utaafikiana nami kuwa exclusive content kwenye chapisho ina ugumu."

1 comment:

Christian Bwaya said...

Maoni haya yamenielimisha