Thursday, May 13, 2010

Tunapofelisha kizazi kwa kufaulisha mitihani

Hivi majuzi nimeona matokeo ya kidato cha sita. Matokeo hayo hayakuonekana kuwa na mafanikio saana (kama ambavyo imekuwa kwa miaka kadhaa sasa) lakini hilo wala si jambo la kunishangaza. Lakini pia kati ya waliomaliza ama kuhitimu ni wadogo zangu. Wadogo ambao kwa hakika licha ya kufanikiwa kupata alama ambazo zitawawezesha kuendelea na masomo wayapendayo, bado wanaonekana kutofurahia hilo kwa kujiona kuwa walioshindwa kufaulu.
Binafsi wadogo hawa WALIFAULU KABLA HAWAJAINGIA MTIHANINI kwa kuwa walikuwa wakifanya kila lililo ndani ya uwezo wao kufanikisha ndoto yao. NA HILI NDILO NILIONALO KAMA KUFAULU. Kwa mtu kuweka juhudi kamili kuweza kujua kile anachostahili kujua ni mafanikio hata kama kile kinachoitwa matokeo ama madaraja hayajawa kama upendavyo. Naamini KUFAULU kwa kufanikisha juhudi halisi za kuelewa ufunzwacho na kufanikisha. Na ndio maana nasema wadogo zangu hawa walishakamilisha ufaulu wa maisha (kwa kuweka juhudi katika kila nafasi waliyokuwanayo ili kufanikisha malengo yao).
Lakini mifumo iliyojengwa na waalimu wetu (ambao yawezekana wamejengewa na waalimu wao) ni kuwa unastahili kupata daraja fulani ili uonekane umefaulu. Na ndio maana msisitizo hauko kwenye kuelewa na kuweza kutumia elimu katika maisha na kutatua matatizo ya jamii, bali ni katika kufaulu mtihani kwa kupata maksi kadhaa.
Tusemeje kuhusu WASOMI wetu wa IDARA YA MAWASILIANO IKULU? Unadhani hawakufaulu? Unadhani kuna sehemu yahitaji watu "waliofaulu" vema kama sehemu nyeti kama hizo? Umeshajiuliza wafanyalo huko? Basi SOMA HAPA ama HAPA uone WAFAULU MITIHANI HAWA WANAVYOLIFELISHA TAIFA KWENYE MAMBO NYETI KAMA MAWASILIANO HUKO IKULU
Na pia nimekuwa nikiona maswali meengi kuwa "kwanini wahandisi wa Tanzania hawabuni vitu vya kuisaidia jamii wakiwa nyumbani" na nahisi hili ndilo jibu lake. Kuwa waandisi ambao wamekuwa na alama nzuri darasani na kutunukiwa vyeti mbalimbali kuonesha UFANISI DARASANI lakini wanapoingia kwenye "ulimwengu wa kazi" inakuwa ni shughuli nyingine kabisa kwani wafunzwacho kwa nadharia hakionekani kuwa halisi kwenye utendaji wao. Ni hapo waajiri wanapoanza kusaka kama waajiriwa wao wana vyeti visivyo halali ama walipata matokeo hayo isivyo halali. Lakini mwisho wa siku ni kuwa WALIFUNZWA KUFAULU MITIHANI NA SIO KUFANIKISHA KAZI WASOMEAZO.
Yaani kwa wabunge ndio yaleyaleee. Kuonekana anafaulu kwa kupigiwa makofi katika kila asemacho hata kama hakina utekelezaji. Yaani twaifelisha jamii yetu kwa kufaulisha kile tunachoamini kuwa mtihani japokuwa kitu hicho si suluhisho la matatizo tuliyonayo.

Aaaaaahhh!!! NAWAZA KWA SAUTI TUUU!!!!!!!!!!

2 comments:

Simon Kitururu said...

Wazo Kibonge hili Mkuu!Mwenye kuelewa kunauwezekano mkubwa kakuelewa.

Halil Mnzava said...

Safi sana,haya ni mawazo mazuri sana.
Tukiyatumia tunaweza kufika mbali ki maendeleo.