Friday, May 14, 2010

Them, I & Them.......KNOW YOUR PAST...Morgan Heritage

"If you don't know where you're coming from, you don't know where you're heading. Past, Present and future"
Leo ni siku ya TUZO ZA MUZIKI WA TANZANIA almaarufu kama Kilimanjaro Music Award 2010. Hizi zaaminika ama kuaminishwa kuwa TUZO KUBWA ZAIDI NCHINI TANZANIA na kwa mujibu wa TOVUTI YA WAANDAAJI, "TUZO za muziki nchini maarufu kama Kilimanjaro Tanzania Music Awards (TMA) zilianzishwa na Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) mwaka 1999 kama kichocheo cha kutambua wanamuziki nchini na kazi zao."
Ni hapa kwenye "dhumuni" la tuzo nilipojisikia kuandika makala haya ya leo.
Inashangaza sana kuona tunaweza kuaminishwa kuwa tutasonga bila kujua na kuthamini kule tulikotoka. NI UONGO.
Sasa tukiangalia kwa miaka yote ambayo Kilimanjaro Premium Lager imekuwa ikiandaa tuzo, hatujaona wanalofanya baada ya "tukio" hilo la kibiashara kujali UWEPO WA WASANII hasa wale waliowafanya hawa wanaopata tuzo leo hii kupenda kazi hiyo? Hivi mmeshaangalia ORODHA YA WANAOWANIA TUZO HIZO? (Hapa) kuangalia kama kuna tuzo ya wakongwe WALIOSAFISHA NJIA KWA HAWA WAFANYA BIASHARA YA MUZIKI SASA? Watu waliojitolea kuifanya sanaa ya muziki kuthaminiwa ithaminiwavyo sasa hawaonekani kujaliwa hata kidogo. Walio hai na waliotangulia mbele ya haki kwa nini hawapewi heshima yao? Orodha ni ndefu ya watu walioimba kuiinua sanaa ya muziki, lakini hatuoni mahala ambapo hawa "wanaojifanya" kuenzi SANAA YA MUZIKI wanashindwa kuenzi walioifikisha hapa ilipo. Na ndio maana leo hii nakumbusha neno kuu lisemwalo kwenye wimbo know your past kuwa "Every man must know their past, so we can stand firm in the future"
Bila kuwaenzi walioifikisha sanaa ya muziki hapa ilipo, ina maana na hawa waliopo hawataenziwa wala kujaliwa muda mchache ujao na ndio maana HATUTAKUWA NA MUZIKI ULIOSIMAMA / KUTAMBULIKA kwa kuwa wenye dhamana ya "kupitisha" HISTORIA, ujuzi na uzoefu wa muziki hawathaminiwi.
NATOA WITO KWA WAANDAAJI WA KILI MUSIC AWARDS KUWAENZI WASANII WALIOTANGULIA KWANI BILA KUFANYA HIVYO HATUTAENDELEA WALA KUENDELEZA MUZIKI
Ndugu watano (L-R) Mr Mojo, Dada Una, Jah Petes, Gramps na Luke ambao wanaunda kundi zima la Morgan Heritage
Basi na tusikilize huku tukisoma maneno mazuri katika wimbo huu KNOW YOUR PAST wao MORGAN HERITAGE

[Intro]
What does it profit a man to gain the world
And loose his soul ?
If you don't know where you're coming from
You don't know where you're heading.
Past, Present and future

[Chorus]
Every man must know their past
So we can stand firm in the future, yes X2

[Verse 1]
History can recall, it can recall
The true essence of ourselves which we have lost
Trying so hard to attain for the future
We have let go what has kept us since creation
But through the Divine powerhouse of life
We'll know past, present and future

[Verse 2]
So many of us have gone astray
Chasing dreams which only fade away
Ignoring the blood, sweat and tears of our forefathers
Breaks the connection to our ancestors
We must all have true awareness of ourselves.
It is a part of a solution.

[Chorus x2]
Stand firm, stand firm, stand firm...

**Them, I & Them ni kipengele kikujiacho kila Ijumaa kinachoelezea kazi za wasanii (Them) kulingana na maono yangu (I) kwa ajili na manufaa ya hadhira (Them)**
Kwa nyimbo zaidi ndani ya kipengele hiki bofya hapa.
IJUMAA NJEMA

No comments: