Friday, November 5, 2010

Them, I & Them....SO MUCH TO COME....Morgan Heritage

"If you think the judgement started, there's so much more left to come. If you think your tears a-run yet, there are so many more tears to run, if you think you've seen the blood yet, there are so much more blood to run... WE FEEL IT FOR THE CHILDREN, FOR THE WORLD THAT THEY KNOW IT.... WILL NOT LAST FOR LONG" Morgan Heritage
Ni kauli ambayo nimeanza kuiona na kuanza kuiwaza kwa nchi yangu niipendayo TANZANIA. Uchaguzi mkuu wa Uraisi na wabunge ndio umemalizika siku 5 zilizopita na mpaka sasa KWA SABABU NINAZOJITAHIDI KUZIELEWA, hayajatangazwa. Lakini Morgan Heritage walishatuonya tangu 2003 kwa wimbo huu kuwa KUNA MENGI YAJA. Jah Petes Morgan. Lead vocalist wa Morgan Heritage
Tumeanza kusikia kauli tata kuhusu matokeo na usalama wa watu na mali jambo ambalo linasikitisha zaidi. Lakini hili si la kushangaza kwani Morgan Heritage wamesema "these are the days known as eve of destructions, with POLI-TRIX just leading every nation". Sina hakika na TUHUMA HIZI ZA DR SLAA KWA USALAMA WA TAIFA wala MAJIBU HAYA YA USALAMA WA TAIFA ama MAJIBU NA TUHUMA ZAIDI ZA DR SLAA KWA TUME YA TAIFA, lakini nijualo ni kuwa kuna mahala pema pa kujadili na kuyatatua haya.
Tatizo kubwa ni kuwa wanaoathirika si wale walio kwenye "usukani" wa tukio hili. Si wagombea walioshiriki, sio wana-tume wanaoshutumiwa "kuchakachua" kura hizo na wala si wale watakaamua nini cha kufanya, wanaoathirika zaidi ni WATOTO ambao hawakuhusika kwenye kampeni, kwenye kupiga kura, wala kwenye "kuhesabu" kura hizo. Na ni hao ninaowawaza, kuwaonea huruma na kuwaombea.
Ni wakati ambao lazima kutanguliza maslahi ya TAIFA mbele. Wakati wa kuchunguza NGUVU ZA KAULI na MATENDO yanayoweza kuathiri wengine.

Wimbo huu ufuatao ni kumbusho kuwa kuna mengi yajayo zaidi ya tuonayo. Kama ni dhuluma zikingali nyingi zikija, kama ni uhalifu, dharura na mengine yaathiriyo maisha ya watoto BADO KUNA MENI YA KUJA. Swali ni kuwa TUMEJIANDAAJE KUWASAIDIA AMA KUWAOKOA WATOTO?
Sikiliza wimbo huu wao Morgan Heritage wakisema SO MUCH TO COME wakizungumza mambo yajayo.

**Them, I & Them ni kipengele kikujiacho kila Ijumaa kinachoelezea kazi za wasanii (Them) kulingana na maono yangu (I) kwa ajili na manufaa ya hadhira (Them)**
Kwa nyimbo zaidi ndani ya kipengele hiki bofya hapa.
IJUMAA NJEMA

1 comment:

Simon Kitururu said...

Asante kwa UJUMBE! Asante kwa wimbo! Bless!