Friday, February 25, 2011

Them, I & Them....CRY NO MORE....Beres Hammond

Hali ya maisha ilivyo sasa ULIMWENGUNI imemuathiri takribani kila mmoja. Wengi wamepoteza kazi, wengi wamepoteza ndugu ambao kwa msongo wa mawazo na kukata tamaa wameamua kukatisha maisha yao (na wengine ya wenzi na familia zao) na wengine kuteteresha afya zao kwa kuwaza kuliko wanavyoweza kuwa suluhisho.
Nami kama wengine niliwaza na kuwazua lakini nikagundua kuwa kuna baadhi ya mambo ambayo kuwaza na kufikiri hakutayabadili, bali cha kufanya ni kubadili mfumo wa maisha ulio tegemezi kwayo na kuishi bila kutegemea saaana uwepo wa hayo. Mfumo huu mpya wa maisha una msaada sana kwa sasa hasa kwa yeyote ambaye hana lolote analoweza kufanya kubadili uhalisia wa maisha ya sasa. Baadhi ya mambo hata ukiwaza na kujikwaza hayatabadilika kwa sasa, mfano kuwaza kazi / ajira wakati hakuna anayeajiri, kuwaza nyongeza ya mshahara wakati waajiri wanapunguza watu kazi, kuwaza kuongeza wateja katika biashara wakati wanunuzi wanaishi kwa kuomba na kwa msaada wa serikali, kuwaza pesa mara mbili ya mshahara ilhali unajua halitakoea. Jawabu nililopata naamini ni muafaka kuwa TWAHITAJI KUISHI KAMA TULIVYO NA KUJITAHIDI KUTENGENEZA NAFASI NJEMA YA MAISHA TULIYOPO KULIKO KUENDELEA KUOTA YASIYOWEZEKANA KUTENDEKA SASA. Kwa kifupi twatakiwa kuishi kwa namna tulivyo na si tutakavyo. Kama alivyosema "mwana mpotevu" kuwa Pa kuanzia ni pale ulipo (Bofya hapa kumsoma)
Niungane naye Beres Hammond katika kibao hiki NO MORE ambapo naye ameeleza alivyoamua kuishi bila hesabu za kile asichonacho.
Sote twaweza na itatupunguzia hali ya kujiona kama walioshindwa kuyakabili maisha kwani tutakuwa tukiishi kwa uhalisia wa maisha ya sasa.
Msikilize hapa Beres Hammond anapoanza kwa kusema
"Am gonna cry no more, i've shed my last tear,
No more worrying about what tommorow bring.I'm gonna live today the best way the best way i will have, and from now on that's how is gonna be...."
pia anaendelea kuimba kuwa
" i'm wont set myself for the worry about what i can't have
i'll have to live without......"


**Them, I & Them ni kipengele kikujiacho kila Ijumaa kinachoelezea kazi za wasanii (Them) kulingana na maono yangu (I) kwa ajili na manufaa ya hadhira (Them)**
Kwa nyimbo zaidi ndani ya kipengele hiki bofya hapa.
IJUMAA NJEMA

1 comment:

Simon Kitururu said...

Umeniwazisha Mkuu!


Sasa hivi nafikiria kama ulichofanya ni sahihi au vibaya kwa STAILI uliyotumia kuniwazisha!:-(

Nje ya tundu:

Sikumsikiliza Beres Hammond siku nyingi na asante kwa hilo pia!:-(