Monday, February 13, 2012

Maendeleo ya msiba wa Dada Christavina

Kwa niaba ya familia ya marehemu Christavina, tunapenda kutoa shukrani za dhati kwa wale wote waliohudhuria na kushiriki katika harambee ya mazishi ya Christavina. Mungu awabariki sana na awazidishie.
Pia, tunapenda kutoa shukrani kwa waumini, waimbaji na wachungaji wa The Way of the Cross Gospel Ministries kwa ukarimu wao na moyo wao wa upendo.
Kwa kifupi harambee ilifanikiwa sana. Jumla iliyopatikana ni kama ifuatavyo:
Pesa (Cash) $4,421
Hundi (Checks) $3,250
Ahadi (Pledges) $1,520
Jumla $9,171
Kwa mara nyingine, tunashukuru sana.
Kwa wale ambao bado wangependa kusaidia, tafadhali fika kwa mume wa marehemu anuani ni 3237 75th Avenue Apt 201,
Landover (or Hayattsville), MD 20785.
Tupo kila siku jioni kuanzia saa 12 jioni (6pm). Kwa wale wa mbali, bado tunapokea michango kwa kupitia
Capital One Bank,
Account# 1351500235;
Routing # 255071981.
Jina la Account ni Lavorn Cryor.

Mipango ya mazishi:
Misa ya kumuaga marehemu itafanyika Jumapili Februari 19, saa 4 asubuhi (10 am) katika kanisa la Takoma Park Seventh Day Adventist, lililoko 6951 Carroll Avenue, Takoma Park, MD 20912. Misa hiyo itamalizika saa 6 mchana (12 noon). Baada ya hapo tutarudi nyumbani kwa mume wa marehemu kwa chakula cha mchana. Mume wa marehemu ameomba, kwa heshima, mwili wa marehemu usipigwe picha. Tutashukuru kwa hilo.
Mazishi yatafanyika Jumatatu Februari 20. Tutakutana nyumbani kwa marehemu saa 2 asubuhi (8am), na saa 2.30 (8.30) tutaelekea J.B Jenkins Funeral Home iliyoko 7474 Landover Rd, Landover, MD 20785. Pia unaweza kwenda J.B Jenkins Funeral Home moja kwa moja.
Tutaondoka J.B Jenkins Funeral Home saa 3.30 asubuhi (9.30 am) kuelekea makaburi ya Gate of Heaven yaliyoko 13801 Georgia Avenue Aspen Hill (wakati mwingine GPS itaonyesha Silver Spring), MD, 20906.

Asanteni sana na tunamtakia mpendwa wetu Christavina, pumziko la amani.

Kwa habari zaidi unaweza kuwasiliana na:
Ndg. Magoma (202.607.1976);
Ndg. Adelaida (240.602.3183);
Ndg. Matinyi (301.792.2832);
Ndg. Mkakile(240.938.3177);
Ndg. Teddy (301.254.4169);
Ndg. Makaya (202.460.1044);
Ndg. Latifah (240.603.7353); au
Ndg. Rebecca(240 898 7161).

No comments: