Wednesday, September 5, 2012

Tanzania Yangu....Yenye WIZARA ZISIZO NA MANUFAA KWA JAMII

Miaka ya karibuni tumeshuhudia kumomonyoka kwa maadili ya uandishi wa habari Tanzania. Fani nzuri na muhimu na kiungo muhimu kwa jamii yetu imeingiliwa.
Na kibaya zaidi, kama ilivyo kwa WIZARA nyingi zenye majina yasiyoendana na UTENDAJI wao, hatuoni lolote likitendeka inapotokea habari ikapotosha jamii.
Tunayo WIZARA YA HABARI, VIJANA, UTAMADUNI NA MICHEZO ambayo KWA MTAZAMO WANGU ni kati ya WIZARA MFU ZAIDI NCHINI.
Dk. Fenella Mukangara, Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo
Hii ni Wizara ambayo mpaka sasa sijajua inashughulikia vipi suala la HABARI kwa maana ya kuhakikisha NI MUAFAKA NA INAWAFIKIA WANANCHI WOTE.
Ni Wizara ambayo imeshindwa kufanya kazi ya kukuza (hata kutunza utamaduni) wa mTanzania ambao UNAMOMONYOKA KILA SIKU na pia ni Wizara yenye bajeti ya michezo lakini tunaona tunavyozidi kuwa KICHWA CHA MWENDAWAZIMU.
Vijana ndio haooooooo. Wanateseka na kuhaha kusaka maisha na HAKUNA (ama niseme hatuHABARIshwi lolote na Wizara hii kuhusu) mkakati wa kumkomboa kijana
Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo ni moja ya WIZARA MIZIGO ZAIDI Tanzania hasa kwenye suala la michezo kwani zipo nchi (kama Marekani) ambazo HAZINA WIZARA ZA MICHEZO lakini zinafanya vema kwenye sekta hiyo.
Tanzania mpaka sasa hatujaona MKAKATI WA WAZI wa wizara hiyo kuhakikisha kuwa inatengemaa kwenye HABARI, UTAMADUNI NA MICHEZO.
Nikirejea kwenye fani yangu ya habari....huko ndio KUMESAHAULIKA
Wiki kadhaa zilizopita nilibandika picha ya kurasa ya mbele ya gazeti ambalo lilikuwa na habari inayopotosha jamii lakini HAKUNA LILILOSEMWA NA WIZARA.
Ninalowaza hapa ni kuwa,
  • Ni kwanini magazeti "yanayomchafua" Rais (mmoja) yafungiwe na kuacha haya yanayodanganya na kuharibu KIZAZI KIZIMA KISOMACHO?
  • Ni upi wajibu wa WIZARA YA HABARI nchini? Haionekani kusimamia upatikanaji wa HABARI SAHIHI NA MUHIMU kwa wananchi. Haionekani kuhakikisha kuwa wananchi wanaarifiwa kila kilicho sahihi. Haionekani kuhakikisha kuwa wananchi wa pande zote za nchi wanapata habari bila kujali kiwango cha maisha waishicho.
Leo hii nimekutana na habari nyingine (miongoni mwa nyingi) inayopotosha kabisa ukweli wa jitihada za kijana mwenzetu (Diamond) na bado Wizara imekaa kimya.
Labda hawajui uhakika wa safari yake, lakini wanaweza kuuliza na kuangalia UMUHIMU WA HABARI HII KWA JAMII.
HATA KAMA NI KWELI......
  • Kuna athari gani kwa Diamond kuitwa na Freemasons wa Marekani?
  • Ni maelezo gani yanayofuata baada ya kichwa hiki cha habari?
  • Habari hii ina athari gani kwa mamilioni ya wanaomfuatilia?
  • Na pengine ina athari gani kwa jamii nzima inayomuona kama kioo?
  • Si kuna uhuru wa kuabudu? Haujaingiliwa hapa (kama uongo huu ungekuwa kweli)?
Ninaloweza kuona ni kuwa (kama ilivyokuwa kwenye habari nyingi potofu) hakuna atakayewajibika kwa kuipotosha jamii namna hii.
Labda nikumbushe alichowahi kusema Malcom X kuhusu umuhimu wa vyombo vya habari kwani hii ni zaidi ya kazi kwangu.

Tanzania Yangu ni kipengele kinachozungumzia ytale yaendeleayo nchini Tanzania na namna ambavyo "ndivyo sivyo" inavyozidi kupamba moto nchini. Kwa matoleo yaliyotangulia BOFYA HAPA

Tuonane "Next Ijayo"

1 comment:

Shadrack Msuya said...

UKWELI UTABAKI KUWA UKWELI TU HATA KAMA UKIUPAKA NA KUUNG'ARISHA KWA RANGI YA DHAHABU....www.shadrackmsuya.blogspot.com