Sunday, February 24, 2013

BLOGGERS.... SISI NI TATIZO NA / AMA SULUHISHO KWA JAMII

Katika maandalizi ya mkutano wa Diaspora wa mwaka 2010 nchini Uingereza, blogger Issa Michuzi alinukuliwa akisema kuwa "Kwa mahesbu ya haraka haraka hivi sasa kuna blog zinazotumia lugha ya kiswahili zipatazo 200 ambapo pia blog takriban 10 zinaanzishwa kila siku, na kuifanya Tanzania kuw nchi zinazoendelea katika tasnia ya habari kwa njia ya mtandao."
Hayo yalikuwa mahesabu ya mwaka 2010.
Sasa hivi blogu ni nyingi saana.
Yaani hata sisi bloggers hatujuani.
Na wingi wa blogs hizi hauendani na wingi wa mafunzo (japo ya awali) kuhusiana na suala zima la uandishi na maadili yake.
BLOGGERS WENZANGU....
Tuna WAJIBU KWA JAMII yetu jamani.
TUWEKE KANDO UDAKU NA MBIO ZA KUSAKA HITS NA WADHAMINI.
Tuwe macho ya wasioona na kiunganishi kwa wasiounganika
TUSAMBAZE YALIYO MAHITAJI YA JAMII WANDUGU
Ninaomba dakika 35 tu za maisha yako.
TAZAMA HILI. Kisha waza......tunao wangapi.
INAUMA, INASIKITISHA NA INATIA SHAKA SANA
Shukrani saana kwa Dada Rachel wa BLOG YA SWAHILI NA WASWAHILI kwa dokezo la post hii.
Naamini utakumbuka na VIDEO HII hapa chini niliyodokezwa na DADA SUBI WA WAVUTI.COM

No comments: