Monday, August 12, 2013

Tanzania yangu.....Yenye wasanii walio makini "kupanda chini"

Photo Credits: Reverbnation.com
Nikiwa mwanachuo katika Kituo cha Mafunzo ya Ufundi na Huduma (VTSC) chini ya VETA mjini Dodoma, tulikuwa na somo la UJASIRIAMALI.
Na licha ya kwamba miongoni mwetu hatukuonekana kuvutiwa ama kulipenda na / hata kutilia maanani yaliyofunzwa katika kipindi hicho, kuna jambo ambalo tangu lilipotambulishwa kichwani mwangu na Mwalimu wangu Mr. Lawrence Mashindano, limeendelea kuwa MSINGI wa maamuzi mengi nitendayo.
Na ni jambo ambalo sio tu limeonekana kufaa kwenye UJASIRIAMALI, bali katika mfumo mzima wa maisha. Kuanzia mahusiano mpaka maongezi.
Ni kama vile lolote linalohusisha KUFANYA MAAMUZI limehusisha jambo hili.
Nalo ni HATUA TANO katika ujasiriamali (mimi ntaita hatua tano za maamuzi) ambazo ni O.I.G.I.R
Observe the environment
Identify opportunities
Gather necessary resources
Implement activities
Rip rewards.
Kwangu, hatua hizi tano nimezitumia hata katika kuamua lile la kusema na kuandika pia.
Sasa..........
Nirejee kwenye POST yangu ya leo.
Nimekuwa nikifuatilia mahojiano ya wasanii mbalimbali wa Tanzania na nimeishia kuwaza kama nao wanachukulia kazi yao kama UJASIRIAMALI na kama ndivyo, nawaza kama wanaijua hata hadhira yao.
Yaani kuna wakati (katika hali ya kushangaza kabisa) unasikia msanii ambaye anajua fika kuwa HANA HADHIRA YA KIMATAIFA, anawasiliana na hadhira yake kwa lugha ambayo wengi wa wamsikilizao hawaielewi kwa ufasaha ama hawaitumii kila wakati.
Lakini pia, achilia mbali kuelewa na kuitumia lugha hiyo kwa hadhira yake, bado kuna jambo jingine la msanii mwenyewe kutoimudu lugha hiyo.
Limekuwa kama WIMBI la mahojiano kuhusisha majibu mengi ya kiingereza hata pale msanii anapoulizwa kwa kiSwahili, na hili limenifanya niwaze iwapo MTAZAMO wa wasanii hawa ni kuwa "kwa kujibu kwa kiingereza wanakuwa wamedhihirisha ubora ama ukomavu fulani maishani"?
Kibaya zaidi ni pale wanaposhindwa kueleweka kwa wanaojua kiingereza, wakashindwa kueleweka hata kwa wale wateja halisi wao (ambao si wote wanaielewa lugha hiyo)
Karika ukurasa wangu wa Facebook nilipata kuuliza kuwa ni msanii gani ambaye anapohijiwa kwa kiswahili hujibu kwa kiSwahili bila kuchanganya na kiingereza?
Wengi (wa walioona na kujibu) wakamtaja Diamond.
Sina hakika na uhusiano wa hili na UMAARUFU WAKE, lakini kuna ukweli kuwa ASILIMIA KUBWA YA WASANII WETU WENGI HAWAJULIKANI AMA KUTAMBULIKA KWA KILE WANACHOSEMA (kwa kuwa hawana mafunzo ya kuzungumza), BALI KWA HABARI ZA UDAKU NA KASHFA MBALIMBALI
KUMBUKA....NIMESEMA WENGI. SI WOTE
Wapo wachache ambao wanaendeleza utamaduni wa kuwasiliana vema na hadhira yao, kwa lugha ielewekayo kwao na kufikisha ujumbe wao kwa wadau wao.
Na kwa kufanya hivyo, wanajikuta waki"connect" vema na hadhira yao

Kumbuka.....Mzee Nelson Mandela alipata kusema kuwa "If you talk to a man in a language he understands, that goes to his head. If you talk to him in his language, that goes to his heart."
Kwa tafsiri isiyo rasmi anasema, ukiongea na mtu kwa lugha anayoielewa, yale usemayo yatamkaa kichwani. Ukiongea naye kwa lugha yake, yale usemayo yataelekea moyoni mwake
Ina maana....wasanii wetu waongee na wadau wao kwa LUGHA YA KWAO, ili yale wayanenayo, yawakae mioyoni na sio vichwani.
Wale wanaojitahidi kuwasiliana na wananchi kwa namna inayowa"boa", hawana tofauti na yule anayejitahidi "kukwea chini"


Ni mtazamo wangu tu kwa namna nionavyo tatizo.
Labda namna nionavyo tatizo ndilo tatizo 

Tanzania Yangu ni kipengele kinachozungumzia ytale yaendeleayo nchini Tanzania na namna ambavyo "ndivyo sivyo" inavyozidi kupamba moto nchini. Kwa matoleo yaliyotangulia BOFYA HAPA
Tuonane "Next Ijayo"

No comments: