Tuesday, November 26, 2013

Ngoma Africa Band "wauteka" mji wa Bremen,Ujerumani kwa muziki

Wavuna umati wa washabiki wa kimataifa
Bendi maarufu ya muziki wa dansi barani Ulaya Ngoma Africa almaarufu FFU ughaibuni,usiku tarehe 23 Novemba 2013 walifanikiwa kwa mara nyingine kuliteka jiji la Bremen nchini Ujerumani. Kiongozi wa bendi hiyo kamanda Ras Makunja wa FFU alikiongoza jukwaani kikosi kazi chake katika jumba la Übersee-Museum akiwa na matumaini kuwa wanaenda kutumbuiza washabiki "high class" (wenye hadhi ya kibwanyenye) lakini mziki ulipoanza mdundo uliwachanganya washabiki na kila mmoja alijimwaga uwanjani !
Ngoma Africa Band walijikuta wapo katika kibarua kama kawaida yao cha kushambulia kwa virungu vya muziki na kufanikiwa kuupanua wigo wake kwa kuwanasa mashabiki wengi wa kimataifa.
Bendi hiyo iliyojiimarisha na kujenga himaya ya kimataifa kwa kutumia muziki wake, imekuwa ikitajwa kama bendi bora ya kiAfrika barani ulaya.
Bendi ya Ngoma Africa inafanananishwa sawa na kikosi maalumu cha kuzuia ghasia FFU, lakini pia ina majina mengi ya utani na kiusanii kama vile Viumbe wa ajabu  "Anunnaki Elien" n.k ambayo imepewa na washabiki au wapenzi wake.
Kiongozi wake pia ana majina kama vile kamanda Ras Makunja wa FFU ,mtawala wa Anunnaki Empire.
Ngoma Africa band wanasikika kupitia www.ngoma-africa.com
 
 
 
 
 
 

No comments: