Sunday, April 6, 2014

[AUDIO] DAKIKA 90 ZA DUNIA. Mauaji kwenye kambi ya jeshi Fort Hood

Jenerali Mark Milley, Kamanda wa Fort Hood akizungumza na waandishi wa habari
Wiki iliyopita, nchi ya Marekani ilikumbwa na mauaji mengine yaliyotokea kwenye kambi ya jeshi huko Fort Hood, Texas.
Jumatano Aprili 2, askari mmoja wa Jeshi la nchi hiyo, Ivan Lopez ambaye inasemekana alikuwa na matatizo ya msongo wa mawazo, aliwafyatulia risasi na kuwaua wanajeshi wenzake 3, kujeruhi 16 kabla hajajigeuzia bastola na kujiua
Mauaji haya, yanarejesha kumbukumbu ya mauaji makubwa kabisa kutokea kwenye kambi za jeshi nchini humo, yaliyotokea kwenye kambi hiyohiyo takriban miaka 5 iliyopita.

Hii ni sehemu ya ripoti ya Jamii Production kwenye kipindi cha DAKIKA 90 ZA DUNIA kinachorushwa na kituo cha Radio cha Capital FM cha Dar Es Salaam Tanzania kila Jumamosi kuanzia saa moja na nusu asubuhi (7:30 AM).
Hii ilikuwa ripoti ya Aprili 5, 2014

No comments: