Tuesday, November 18, 2014

MISHUMAA YA KALE...Kipindi kipya kutoka VIJIMAMBO na KWANZA PRODUCTION

Photo Credits: Ye Olde Vivyl Shoppe
Baada ya pilika za wiki nzima, na mchamchaka wa maisha, sasa unakuja wakati wa kuburudika na muziki halisi wa zamani.
Katika kipindi hiki, utaweza "kuruka majoka" na "kula mangoma" kwa kusikiliza nyimbo ziliotamba miaka ya zamani, kupata historia ya wasanii na vikundi mbalimbali na pia kusikiliza mazungumzo na maDj na wasanii mbalimbali wa zamani.
Ungana na MixMaster Dj Luke Joe kwenye "one and two" na Mubelwa Bandio nyuma ya kipaza sauti kwenye kipindi kipya cha MISHUMAA YA KALE kitakachokujia kila Ijumaa kuanzia saa 11 kamili jioni mpaka saa 1 kamili usiku kwa majira ya Marekani ya Mashariki (5:00pm - 7:00pm EST)
Ungana nasi kupitia www.kwanzaproduction.com
MixMaster DJ Luke Joe. Photo Credits: IskaJojo Studios
Mubelwa Bandio


No comments: