Saturday, August 30, 2008

Rais Kikwete amaliza ziara nchini Marekani

Rais Kikwete akipokea maua maua toka kwa mtoto Ninai Joseph Sokoine

Mama Salma Kikwete akipokea maua ya ukaribisho toka kwa Kelvin Masanja

Baadhi ya wageni waalikwa




Rais Kikwete akisalimiana na wawakilishi wa Jumuiya ya Watanzania DC Metro


Rais akiagana na waheshimwa mbalimbali walioshiriki naye mlo wa jioni.
Rais Jakaya Kikwete, leo amehitimisha ziara yake ya kikazi hapa nchini kwa kufanya maongezi na baadhi ya mabalozi na wawakilishi wa nchi mbalimbali na pia kushiriki chakula cha jioni na mabalozi hao pamoja na wawakilishi wa Chama cha wanajamii ya waTanzania waishio Washington DC na vitongoji vyake. Chakula hicho kiliandaliwa na ubalozi na kusanyiko hilo kufanyika kwenye makazi ya Balozi wa Tanzania hapa nchini Mheshimiwa Ombeni Sefue yaliyoko huko Maryland.

No comments: