Tuesday, October 28, 2008

Una bahati hauko kwetu

Kwetu ni Afrika na naamini kokote kule ndani ya kwetu (Afrika) wangehitaji maelezo ya kina ya huu wimbo wako. Yaani kumuimba Rais namna hii??!!!! Ila ndo ukweli ulivyo. Sijui ni CHANGAMOTO kwa wasanii wa kwetu kuimba ukweli (unaoweza kuwatoa kafara) ama kwa wasanii wa nje kama Alecia Beth Moore (Pink) kujitahidi ama kuficha ama kukata makali ya ujumbe ndani ya nyimbo zao.
Sina jibu, ila nisemalo ni kuwa hii kila mtu atai-judge kwa mtazamo wake. No wonder video hii iliyowekea maneno kwa lugha mbalimbali ina mamilioni ya watazamaji huko You Tube. Click hapa uone yaloimbwa kisha ufikirie ingekuwa kule kwetu huyu angepewa zawadi gani http://www.youtube.com/watch?v=mQYHKILXD4k

No comments: