Saturday, November 1, 2008

Wow!!!!!!!!!!!!!

"They were brought here to protect us, They were brought here not to hurt. But now they hurt us everyday. You see, Police have joined forces with criminals..... How can we expect them to serve and protect the community, if they themselves are the bad guys" Hayo sijasema mimi. Aliimba Lucky Dube kwenye wimbo Life In The Movies ndani ya albamu yake ya Trinity. Si aliyaona yalitokuwa yanatokea kipindi cha ubaguzi kule Afrika Kusini. Sasa aibu kwetu kuwa yanatendeka miaka karibu 50 baada ya UHURU.
Hapa nausaka MSTARI HAFIFU unaotenganisha SHERIA na HAKI.
Nausaka maana nikiuona ntaukazia wino ili hawa Ma-askari waweze kuuona na kutambua kuwa wanachotakiwa ni kulinda sheria lakini hawana mamlaka ya kuamua haki ya mhisiwa, mkusudiwa ama mshukiwa. Na ndio maana wanamsongesha mbele kwenye vyombo vya haki kama Mahakama ili HAKI ITENDEKE. Lakini hili nalo hawalioni.
Si tu kwamba ma-askari hawalioni, ila yaonesha hata wenye kuhusika na kuwakumbusha hawa hawalioni pia. Kuna jambo nahisi na pia kuna jambo najua. Ninalohisi ni kuwa hawa Askari wanapokuwa CCP ama popote kulingana na utekelezaji wao (nikimaanisha Magereza, ama Mgambo ama Akari Polisi, Sungusungu nk) wanafundishwa juu ya kile kitwacho Code Of Ethics. Najua kuwa wanaelezwa kuwa hiyo ni kazi na si nafasi ya kunyanyasa wanyonge kutokana na mood unayokuwa nayo siku hiyo. Kutambua mipaka na haki za wale wahisiwao kuwa wakosaji. Hata mwenye kosa la mauaji bado ana haki na sio wajibu wenu kumhukumu just kuonesha ubabe. Ziggy Marley aliuliza "why we lose ourself just to find who we are?"
Ila pia NAJUA kuwa ni wachache wenye kutekeleza hayo wafunzwayo. Tumechoshwa na uborongaji na uvunjwaji wa haki za binadamu tunaofanyiwa, kuuona na kuusoma ama kuuangalia katika vyombo mbalimbali vya habari hapo nchini.
Tumeyaona haya kuanzia Zanzibar ambayo yamesambaa kwenye tovuti kama You Tube (bofya hapa uone yalivyo wazi ulimwenguni na yanavyotia kinyaa http://www.youtube.com/results?search_query=Tanzania+police+brutality+Zanzibar+Nov+2005&search_type=&aq=f) kisha tukaona kina Mzee wa Sumo walipigwa na Askari Magereza na juzi tu hapa Father Kidevu naye akwa mhanga.
Pamoja na kuwekwa mitandaoni kwa muda wote huo, bado mnaendelea kujichukulia sheria mkononi tena bila woga???? Come On.
Namuunga mkono Lucky Dube kuwa sasa huyo Polisi kishaungana na waovu kufanya uasi.
Pole Kaka Mroky na kwenu wanausalama (wale wachache wenye kuharibu sifa nzima ya jeshi) , ni CHANGAMOTO KUBADILI TABIA

Na huu ni mtazamo wangu kwa namna nionavyo Tatizo. Yawezekana ndilo Tatizo nililonalo.

No comments: