Monday, November 3, 2008

Hongera na Shukrani VGSS

Sote twaamini kuwa ukitaka kupata matunda mema basi anza kujali pale unapowekeza tangu hatua za mwanzo. Anza kutoa huduma bora na muhimu tangu anwali kuweza kukupa matunda bora na mengi. Na kwa hili ambapo BLOGU hii inaungana na wapenda maendeleo wote kuwashukuru na kuwapongeza Vodacom kwa mpango wao wa kuwaendeleza vijana katika soka. Tuna imani kuwa Francis Costa, Cosmas Mwazembe na Salum Bakar Saad watakuwa nyota njema sio tu kwa Tanzania, bali kwa ulimwengu kwa ujumla na ni hazina ya miaka ijayo kwa maisha na michezo nchini kwetu. Lakini pia tunapongeza na kushukuru kwa wale wote washiriki 11,000 waliojitokeza kuwania nafasi hizo. Twaamini kuwa kati yao wapo wengi walioona uwezo mkubwa walionao hivyo wataongeza juhudi ili waweze kufika mbali katika mchezo huo waupendao. Na twaamini kuwa kati ya hao hao 11,000, wapo walioonekana na kuelekea kunyakuliwa na timu zinazoshiriki ligi mbalimbali na kuwaendeleza ki-soka.
Shukrani Na Pongezi kwenu Vodacom kwa kunyakua vipaji toka kanda zote za nchi.

No comments: