Monday, November 3, 2008

Washindi wa Bahati Nasibu ya Benki ya Posta wapatikana

Meneja wa benki ya posta tawi la Bukoba Maduhu Makoye akimzawadia muuguzi msaidizi wa hospitali ya mkoa wa Kagera Judith Kaindoa zawadi ya friji baada ya kuibuka mshindi wa kwanza wa bahati nasibu iliyochezeshwa na benki hiyo.

NA MKEBEZI RUGALABAMU,BUKOBA
MUUGUZI msaidizi wa hospitali ya mkoa wa Kagera Judith Kaindoa ameibuka mshindi wa kwanza wa bahati nasibu iliyochezeshwa na benki ya Posta tawi la Bukoba.
Kwenye bahati nasibu hiyo iliyochezeshwa na benki hiyo kuanzia julai 23 hadi septemba 30 mwaka huu muuguzi huyo alipata zawadi ya Friji ya milango miwili yenye thamani ya zaidi ya shilingi 900,000.
Zawadi hiyo kwa mshindi huyo wa kwanza ilikabidhiwa na meneja wa benki hiyo tawi la Bukoba Maduhu Makoye sambamba na washindi wengine katika sherehe fupi iliyofanyika katika jengo la Benki hiyo mwishini mwa wiki.
Washindi wengine walioshinda zawadi mbalimbali za bahati nasibu iliyochezeshwa na benki hiyo ni pamoja na Bryson Mayowa mshindi wa pili aliyepata zawadi ya television yenye thamani ya shilingi 270,000 aina ya hitachi.
Washindi wengine waliopata zawadi ni Mariath Kagambo ambaye alipata zawadi ya cherehani baada ya kuibuka mshindi wa tatu chenye thamani ya shilingi 180,000 ,mshindi wa nne ni Amani Rhodes aliyeibuka na baiskeli yenye thamani ya shilingi 130,000 na mshindi wa tani alikuwa Arosto Mstapha aliyeibuka na zawadi ya simu aina ya nokia yenye thamani ya shilingi 130,000.
Utoaji wa zawadi hizo kwa washindi wa bahati nasibu hiyo ulienda sambamba na uzinduzi wa promotion kabambe ambayo Benki hiyo imeanzisha inayojulikana kwa jina la Gazebo ambayo itamwezesha mteja anayefungua akaunti kwenye benki hiyo na kujiunga kwenye mija kwa mija kwenye shindano la bahati nasibu ambapo washindi watakuwa wanatangazwa kila mwisho wa wiki.
Akiongea baada ya kukabidhi zawadi kwa washindi meneja wa benki hiyo alisema katika promotion ya gazebo wateja 50 wa kwanza watakaofungua akiba kwenye benki hiyo watakuwa na nafasi ya kufungua akiba kwa kiazio cha shilingi 10,000 na watapigwa picha bure.
Sambamba na hilo Maduhu alisema kuwa wateja wapya watakaofunguo akiba kwenye benki hiyo kwa kiazio cha zaidi ya shilingi 40,000 watapatiwa zawadi mbalimbali ambazo ni pamoja na tshit, kalamu na miavuli na pia watashiriki moja kwa moja kwenye bahati nasibu inayochezeshwa na benki na kupata washindi kila wiki.
Alisema katika bahati nasibu ambayo washindi wake wamepatiwa zawadi zao benki hiyo ilikuwa imetenga zaidi ya shilingi milioni 2.5 kwa ajili ya washindi hao , Maduhu alisema sasa michezo ya bahati nasibu ambayo benki hiyo itaichezesha imetenga zaidi ya shilingi milioni 4.9 kwa ajili wa washindi.
Meneja huyo wa benki ya posta alisema kuwa washindi wote waliopata zawadi walipatikana kutokana na vigezo mbalimbali, alisema kuna washindi walioshinda bahati nasibu hiyo walipatikana kwa kufungua akaunti mpya na wengine walipatikana kwa kuweka fedha nyingi kwa muda mfupi kwenye akaunti zao.
Maduhu alisema benki ya posta ni benki ambayo imejizajititi kuboresha huduma zake hasa kwa wateja wake, alisema benki hiyo kwa sasa inafanya uhamasishaji wa aina mbalimbali ili iweze kuwavuti wateja wake na iweze kupata wateja wapya.
Alisema benki hiyo kwa sasa imenzisha huduma ya utumaji wa fesha kwenda nje nchi kwa gharama nafuu, Maduhu alisema kwa sasa benki hiyo inatoza dola hamsini kwa kiasi chochote cha fedha kinachotumwa kupitia kwenye benki hiyo kwenda nje ya nchi.
Habari kwa msaada wa Audax Mutiganzi

1 comment:

Anonymous said...

Hahaa Mzee wa Changamoto nimefurahi kuona hii,huyo Mariath mshindi wa tatu ni mdogo wangu.Asante kwa kuipost