Monday, November 10, 2008

Hongera Miriam Odemba

Miss Earth 2008 Karla Henry
Miss Earth Tz Miriam Odemba

Mshiriki na mwakilishi wa Tanzania kwenye mashindano ya kumsaka Miss Earth 2008 Miriam Odemba amefanya kile ambacho wengi walimtabiria. Kuwa miongoni mwa washindi wa shindano hilo.
Odemba ambaye ameshika nafasi ya pili katika kinyang'anyiro hicho kilichofika tamati jioni ya leo huko jijini Angeles, Pampanga nchini Phillipines, ameweza kuitangaza vema Tanzania kwa kushinda pia tuzo ndogo ya Miss Aficionado ambapo alikuwa mshiriki pekee toka Afrika aliyeshinda moja kati ya tuzo hizo 27 zilizowekwa kwenye kundi la Special and Minor Awards.
Kwa Odemba hii ni CHANGAMOTO nyingine baada ya kuwa amepitia maisha ya aina nyingi yenye vikwazo vingi na hatimaye akaweza kuvipita na kurejea katika kile anachokimudu zaidi. Urembo na Mitindo.
Twampongeza kwa kurejea katika kile amuducho na kumsihi kutumia taji hilo kama balozi mwema wa Taifa kutangaza hali ya kimazingira ambayo imekuwa mbiu kuu ya mashindano hayo yanayosemekana kuwa moja kati ya mashindano makubwa zaidi ya ulimbwende kwa idadi ya ushiriki wa nchi na washiriki wake hujihusisha zaidi na masuala ya kimazingira.
Mshindi wa shindano la mwaka huu ni Miss Phillipines Karla Paula Henry ambaye kabla ya kutwaa taji hilo, alishashinda Tuzo za Miss Earth Designers Award na Miss Photogenic.
Hongera Saaana Odemba

1 comment:

Yasinta Ngonyani said...

Hongera sana na pia asante kwa kuiwakirisha TZ