Monday, March 15, 2010

Za Kale vs Maisha ya sasa........MASUDI

Kwa wazazi wengi, hatua za mwisho kabla ya kumuona ama kumpokea mwana wao anapozaliwa ni kumfikiria na pengine "kupiga picha" ya nini ama vipi mwana wao atakuwa pale atakapokua mkubwa.
Ni hizi hisia ambazo wazazi wengi (haijalishi wana asili ama wanaishi wapi) huwa wanafikia na wengine KUMUOMBEA MWANA WAO na kuweka MATUMAINI kuwa na mtoto mwema.
Si kila mzazi huiona "ndoto" hiyo ikitimia na kwa masikitiko wazazi wengi huona ulimwengu kama umewageuka na kujiona kama wana mikosi.
Haya ni mambo yaliyoanza zamaaani na yaliimbwa na wasanii miaka mingi iliyopita.
Jumatatu ya leo nakuacha na kisa hiki kilichosimuliwa naye Marijani Rajabu katika maisha halisi ya wana-wapotevu katika kibao hiki MASUDI.
** Zilipendwa ni kipengele kinachokujia kila Jumatatu kukuletea muziki wa kale kuhusisha na maisha, muziki ama sanaa ya sasa katika nyanja mbalimbali. Unaweza kusikiliza nyimbo nyingine ndani ya kipengele hiki kwa kubofya hapa, ama mitandao shirika hapa** . Ama ili kuweza kujua tasnia nzima ya muziki na wanamuziki wa Tanzania BOFYA HAPA

No comments: