Sunday, March 14, 2010

Pacquiao amshinda Clottey kwa pointi

Usiku wa kuamkia leo, bondia Manny "Pacman" Pacquiao amedhihirisha kuwa yeye ni KING OF POUND FOR POUND pale alipomshinda kwa pointi bondia Joshua Clottey wa Ghana. Ushindi huu ambao umekuja kwa njia ya pointi, umekuja baada ya Pacquiao kushinda mapambano yake manne ya mwisho kwa KnockOut na likumbukwalo zaidi ni lile dhidi ya Miguel Cotto. Pia Clottey alipoteza pambano lake dhidi ya Cotto licha kuwa alionesha upinzani mkali na hata kumwangusha.
Lakini sasa kinachoangaliwa zaidi ni "nini chafuata baada ya pambano hili?"
Mei Mosi, Floyd Mayweather (aliyekimbia pambano dhidi ya Pacman) atapanda ulingoni kupambana na Shane Mosley. Na kwa kuwa kila mmoja wa watatu hawa ( Pacquiao, Mayweather na Mosley) alishajitangazia ama kutangazwa kama mfalme wa pound for pound, ushindi wa Pacquiao unafanya pambano la Mei Mosi kuwa la ushindani zaidi likitegemewa kutoa mpinzani wake
Je!! Ni nani atakayejipatia nafasi ya kupambana na Pacman kumsaka MFALME HALISI?
TUSUBIRI HIYO MEI MOSI
Tazama highlights za pambano la Pacquiao vs Clottey toka ESPN.COM

Na mahojiano ya Pacman baada ya pambano hapa chini

No comments: