Hawa hapa chini ndio Oysters

Na huu hapa chini ndio ufukwe huko Dar ambao waitwa Oysterbay.

Ninalowaza ni uhusiano wa Oysters hawa na Bay hiyo.
Je! Kuna mwenye taarifa kamili ama usahihi wa kwanini ufukwe huu ulipewa jina la Oysterbay? Ninaamini wengi wa wakazi wa mji wa Dar hawaelewi asili ya jina hili na sitashangaa kama wengi hawafahamu uhusiano wa jina la hao Oyster na Bay hiyo (kama upo ulio halisi kuhusisha kupatikana kwa jina lake)
Leo nimewaza kuhusu hili na kwa kuwa taarifa ama habari nyingi kuhusu mahala, vitu na nchi yetu hazipatikani mtandaoni, nimeona niweke swali langu hapa ili nisaidiwe kuwazua.
Hivi ni Oysterbay ama Oyster Bay? Na asili yake ni nini?? Nawaza tu kwa sauti..NIWAZUE.
Kumbuka hiyo Oysterbay / Oyster Bay iko Dar Es Salaam. Mji aliouimba Ras Nas
Burudika naye hapa chini huku "ukinisakia" jibu
"Tuonane "Next Ijayo"
1 comment:
kuna majina mengi ya ajabu eti kwa sababu wadhungu walishindwa kuyatamka vyema
kama vile kilimanjaro ni kilimakyaro
kuna sehemu kule moshi wachaga wanaita chekeleni kumbe ni chectrain, kiboliloni ilikuwa mdhungu akisimama pale anasema kibo aloni nk
bwagamoyo wanasema bagamoyo, mwanaumango manelumango nk nk
Post a Comment