Sunday, July 11, 2010

REKODI ZAVUNJWA.........

Lakini uvunjwaji wake wanifanya niwaze kama kuna ulazima wa kujaribu?
Wazivunjao WANAWAZA NINI?
Labda tuanze INDONESIA ambapo kumekuwa na habari ya huyu "MTOTO" ambaye aonekana kuwa mdogo zaidi kumudu uvutaji wa sigara.
Nawaza kinachomfanya avute, alivyoanza, anayemuwezesha kuzipata na hata uvutaji wake unapofanyika kama hakuna waonao haya. Na nawaza kuwa kama anaweza kuvuta kwa "ufundi" kwa namna hii, amekuwa akivuta kwa muda gani? Na kama ana miaka miwili, na aligunduliwa na wazazi wake akiwa na miezi 11, alianza lini na alianzishwaje na nani??
Nawaza tuu kuwa kwa kufikia hivi waliomzunguka WANAWAZA NINI?

Na pia niangaliapo HAWA walioingia kwenye kitabu cha MAAJABU ya dunia, WANAWAZA NINI?

Tuhamie huko uCHINA aliyeamua kuvunja rekodi ya KUVUKA NA KAMBA. Nawaza ALIWAZA NINI na waliomuacha ajaribu waliamini vipi kwamba atamaliza na kuvunja rekodi na sio "kifo kitarajiwa?
Itazame hii HAPA
NAWAZA KAMA REKODI NI LAZIMA ZIVUNJWE NA KAMA KILA IVUNJWAYO YAVUNJWA BILA "UTATA" NA "HATARI?
***"Waliwaza nini ni kipengele cha kuelimishana tukifurahia. Hiki kitakuwa kikikuletea habari za kweli na kushangaza kuhusu watu ambao wamefanya yale ambayo unaweza kujiuliza kuwa WALIWAZA NINI? wakati wanatenda haya.
Kitakuwa na habari fupifupi kutoka ulimwenguni kote. Kwa habari zaidi kuhusu kipengele hiki
BOFYA HAPA"***

1 comment:

Masangu Matondo Nzuzullima (MMN) said...

Mzee wa Changamoto. Asante kwa kunijulia hali mara kwa mara. Nimerudi kwenye chakula kitamu rasmi sasa. Tuko pamoja.