Tuesday, July 6, 2010

Sajna... Anapomuwaza machinga wa Tanzania ndani ya dk 4:32


Sajna a.k.a Mzee wa Iveta ktk pozi.
"Nilipoungwa" kuutazama wimbo huu na Kaka Sandu George "Kidbway" mtangazaji mahiri wa a Radio Free Africa na mdau mkuu wa Tetemesha Recordz iliyozalisha wimbo huu, niliamua kutulia kutazama na kusikiliza. Kama kawaida, kuhusianisha nionacho na nisikiacho ilikuwa ni sehemu kubwa ya muda wangu huo.
Na kilichonivutia si mpangilio wa ala ama sauti pekee, bali kilichozungumzwa, kilivyozungumzwa na hata kilivyooneshwa.
NI HALI HALISI YA MAISHA YA WAHANGAIKAJI WENGI NCHINI TANZANIA.
Katika wimbo huu aliouita IVETA, Sajna anamuimbia mpenziwe ambaye amemuacha kijijini kwenda mjini kusaka maisha. Ni mfumo wa maisha ambao unawakumba wengi wanaohangaika kuinua hali ya maisha nyumbani watokako. Lakini maisha hayawaendei kama ambavyo huamini yataenda huko mjini. Anakumbana na magumu ya kusaka maisha na bado anamuomba mpenziwe kumsubiri wakati huu anapotafuta yatoshayo kubadili maisha yake na wake mpenzi. Na katika msako huo huo, anapoanza kujisakia maisha kwa mtaji wake mdogo na kuijali familia yake, anakumbana na "askari wa jiji" ambao (kama ilivyo kwa wachuuzi wengi) wanaonekana kumpa wakati mgumu.
Akiwa mjini, Sajna anaeleza namna anavyokumbuka maisha ya kijijini japo hali halisi ya maisha inamlazimu kukaa mjini "kumtafutia dear" wake ambaye anaendelea kumuomba kuwa mwaminifu na mvumilivu ili waje waje kuishi pamoja.
Mbio zake ambazo zilionekana kufanikiwa kumkimbia askari lakini baadae aliishia kunyang'anywa mali na mporaji. Na swali la kujiuliza hapa ni kuwa ni vipi anaweza kumrejea askari (ambaye alitaka kumdhulumu ama kumnyanyasa) ili kuomba msaada wa kurejeshewa mali.

Na yamkutayo SAJNA ndiyo yawakutayo wajasiriamali wengi saana nchini. Na ndani ya dk 4:32 analiangalia tatizo hili na kulionesha kwa undani zaidi.
Jiunge naye hapa chini kwa kumtazama na kumsikiliza katika wimbo wake huu IVETA

Picha kutoka ukurasa wa "ufokitabu" wa SAJNA

No comments: