Monday, July 5, 2010

Old School Tanzania.......Mwanzo mzuri kuenzi sanaa na wasanii wetu

Kikosi kamili cha Old Skul Tanzania
Februari 18 niliandika kuwa NATAMANI KUONA (bofya hapa kuirejea) na kama naweza kunukuu sehemu kubwa ya toleo hilo niliposema "Nikiwa mpenzi mkubwa wa muziki wa kiTanzania, NATAMANI KUONA kitu ambacho kitakuwa kikitoa mjumuisho wa muziki huo na KUENZI KAZI NA WASANII wa muziki wa Dansi nchini.
Natamani kuona SIKU YA DANSI NCHINI ambayo bendi zitajumuika kuimba nyimbo za wasanii mbalimbali waliochangia kwa kiasi kikuuubwa kuufanya muziki wa Tanzania kuheshimika. Waliotumika kuelimisha, kuburudisha na pia kukamilisha harakati mbalimbali katika jamii.
Natamani kuona tamasha litakalowaenzi nyota wengi wanaoendelea kutuelimisha kwa miaka nenda rudi na pia waliotangulia mbele ya haki...."

Na leo ikiwa ni Jumatatu ya mwisho kabla ya Jula 7, napenda kujumuika na wanaChangamoto wote kuwapongeza wanamuziki wote waliofanikisha kwa namna yoyote uwepo wa onesho hili kubwa la muziki wa dansi liwakutanishalo wasanii wengi wakongwe waliojiita Old School Tanzania mablao lategemewa kufanyika ukumbi wa Karimjee.
Japi sitaweza kuhudhuria, bado nashukuru kuwa KILE AMBACHO NILIKIONA KAMA TAMAA NA AMBACHO NDUGU ZANGU WATOA MAONI WALINIFARIJI KUWA NAWEZA KUONA KIKITOKEA, leo kinamaliziwa.
Shukrani saana kwa washiriki woote waliofanikisha hili na siku ya leo ya Jumatatu ambayo mara nyingi huwa twaweka miziki ya kale, tunajiunga na wapenda burudani woote kupongeza juhudi hizi.
Kwanza pata ufafanuzi wake Waziri Ally kuhusu Old Skul Tanzania.

Na kisha kutazama na kusikiliza mazoezi ya kundi hili hapa chini

PICHA NA VIDEO KWA HISANI YA Michuzi Blog
** Zilipendwa ni kipengele kinachokujia kila Jumatatu kukuletea muziki wa kale kuhusisha na maisha, muziki ama sanaa ya sasa katika nyanja mbalimbali. Unaweza kusikiliza nyimbo nyingine ndani ya kipengele hiki kwa kubofya hapa, ama mitandao shirika hapa** . Ama ili kuweza kujua tasnia nzima ya muziki na wanamuziki wa Tanzania BOFYA HAPA

1 comment:

Yasinta Ngonyani said...

Zamani kweli ilikuwa safi. Na hiyo nyimbo yA TANZANIA NI NCHI YA FURAHA imenikuna sana.