Friday, October 29, 2010

REMEMBERING GREGORY "The Cool Ruler" ISAACS

Kamera ya Changamotoyetu ilikuwepo kushuhudia Hayati Gregory Isaacs akitumbuiza ukumbi wa Zanzibar on The Waterfront March 16, 2008.
Jumatatu ya wiki hii ulimwengu wa reggae ulimpoteza mmoja wa wakongwe huo duniani GREGORY ISAASCS ambaye alifariki nyumbani kwake London kwa saratani ya mapafu (Lungu Cancer). Maradhi hayo aligundulika kuwa nayo mwaka jana.
Nilibahatika kuwa mmoja wa waliohudhuria onesho lake lililofanyika Machi 16, 2008 katika ukumbu wa Zanzibar hapa Washington DC ambapo licha ya kuonekana mdhoofu, bado aliweza kutuburudisha vema kwa nyimbo zake njema zilizompa umaarufu na jina la jukwani la "COOL RULER" Baadhi ya nyimbo alizotumbuiza ni zile zilizompatia umaarufu mkubwa ambazo zilitufanya tusimame muda wote. Nyimbo kama MY NUMBER ONE
Pia alitutumbuiza na nyimbo kama LOVE IS OVERDUE ambao (kama ilivyo kwa nyingine nyingi)ziliwapagawisha kinamama na kinadada.

Pia hakutuacha bila kibao OH WHAT A FEELING ambacho nachi "kilibamba"

Na kama kawaida alimzungumzia "mtabibu wake wa usiku" katika kibao ambacho pengine ndio maarufu kuliko vyote kiitwacho NIGHT NURSE.

Aliweza kutawala vema jukwaa katika muda wote ambao alitumbuiza na kwa hakika wengi wa wahudhuriaji walionekana kufurahia kazi zake na kama uonavyo hapa chini, tabasamu lilionesha kuridhishwa na uwezo wa mkongwe huyuPUMZIKA KWA AMANI GREGORY ISAACS.
KAZI ZAKO ZITADUMU MILELE

1 comment:

Simon Kitururu said...

PUMZIKA KWA AMANI GREGORY ISAACS!

Nguli pamoja na matatizo yake ya kibinadamu haki yanani simchoki!:-(

R.I.P Nguli COOL RULER!