Sunday, October 24, 2010

UZINDUZI WA BLOGU YA VIJIMAMBO........

Ni zaidi ya uzinduzi.....
Ni zaidi ya maonesho.......
Ni mjumuiko wa waTanzania na utambulisho wa ujasiriamali wa waTanzania, kwa waTanzania. Mheshimiwa Balozi akipokelewa na waandaaji wa uzinduzi huo
Usiku wa kuamkia leo, kulikuwa na kile ambacho kilitajwa kama uzinduzi rasmi wa BLOGU YA VIJIMAMBO uliofanyika katika ukumbi wa Mirage Hall mjini Hyattsville, jimbo la Maryland Marekani. Hii ni blogu changa lakini inayofanya vema saana ambayo inamilikiwa na Dj Luke Joe. Blogu hii ambayo ilianza Januari 31 mwaka huu, iliandaa uzinduzi wake rasmi ambapo mgeni wa heshima alikuwa ni Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Marekani Mhe. Mwanaidi Maajar na pia ilihusisha "maonesho" na maelezo ya bidhaa toka kwa wadau wahusikao na jamii ya waTanzania hapa nchini (kama Idhaa ya Kiswahili ya Sauti ya Amerika), mwanamitindo maarufu nchini Tanzania mama Asia Idarous na wajasiriamali wengi sana waTanzania wafanyao shughuli zao hapa nchini.Mara baada ya kuwasili ukumbini. Balozi Maajar alipata nafasi ya kutembelea meza zote za maonesho na maelezo na kuchukua mawasiliano ya wajasiriamali hao, huku akisisitiza kuwaunganisha katika mtandao mmoja kupitia ubalozi katika kufanikisha lengo lao.Baadae alihutubia mjumuiko huo mkubwa wa waTanzania na wadau wa Tanzania na kuizindua rasmi blogu ya Vijimambo kama asikikavyo na kuonekana kwenye video hii ambapo mbali na mambo mengine, Balozi Maajar
1: Aliahidi kuweka ukurasa wa kutangaza kazi za wajasiriamali waTanzania waishio hapa Marekani.
2: Alisisitiza umuhimu wa ushirikiano baina ya waTanzania kama njia pekee na kuu ya mafanikio 3: Alieleza umuhimu wa mitandao ya kisasa kama blogu
4: Alitoa ushauri kwa Dj Luke (ambao kwangu ni ushauri kwa bloggers wote)

Na hizi chini ni taswira mbalimbali zilizonaswa na camera ya CHANGAMOTO YETU zikimuonesha Balozi Maajar akipitia meza za maonesho na maelezo ya wadau mbalimbali waTanzania waliopo hapa. Mhe Balozi akipokea maelezo toka meza ya Jambo Africa Child Hope Inc
Balozi Maajar akipata maelezo katika meza ya WAMATA
Mhe Balozi akipokelewa na Dr Mwamoyo Hamza kwenye meza ya Idhaa ya Kiswahili ya Sauti ya Amerika Baada ya kupitia meza za maonesho na kupata maelezo ya shughuli mbalimbali, Mhe Balozi alielekea meza kuu akikaribishwa na mamia ya waalikwa
Balozi akiingia ukumbini
Dj Luke Joe akimkaribisha mgeni rasmi kutoa neno na kuzindua rasmi bloguMhe Balozi Maajar akitoa hotuba Mwimbaji wa nyimbo za Injili Zuleha Juma akitumbuizaMaakuli na vinywaji pia vilikuwepo bila gharama yoyote
Kisha ukaja wasaa wa maonesho ya mitindo ya mavazi ya mbunifu Asia

MUHIMU::PICHA ZOTE MALI YA CHANGAMOTOYETU BLOG

4 comments:

Masangu Matondo Nzuzullima (MMN) said...

Asante kwa taarifa.

Meza ya "Changamoto Yetu" iko wapi? Mbona zile tisheti za "The Way you see the Problem is the Problem" sizioni?

Mbele said...

Mzee wa Changamoto, taarifa yako hii ni nzuri sana. Imenifungua macho. Kumbe waBongo wa upande wenu huo wanajituma katika ujasiriamli namna hiyo. Safi sana.

Nampa hongera sana DJ Luke. Ameonyesha mfano wa kuigwa, kuwakusanya watu namna hiyo kushiriki katika shughuli murua namna hii.

Hao wanaouza vitu vya nyumbani wanafanya kazi nzuri na muhimu sana, maana ni njia ya kuongeza ajira kule nyumbani na kuingiza kipato kwa Taifa. Kinachohitajika tu ni kumpata mtu atakayewadhibiti mafisadi, ili wakome kuchota hivi vijisenti.

Anonymous said...

Hongera kwa kazi nzuri, ilipendeza sana, picha nzuri sana, hongereni wana-blog

emu-three said...

TWASHUKURU KWA KUTUPA TUKIO HILO MUHIMU! Kweli imetufumbua macho ingawaje bado sisi `bongo-blogs' inakuwa kama `window shopping', wakati wenzetu ni sehemu ya biashara! Oh, sijui tu(ni) fanyeje!