Wednesday, November 24, 2010

Kwenu wapinzani. Ms'ojua ushindani na kukalia ukinzani uwageuzao "washindwani"

Photo Credit: Alternatives-Economiques Blog
Nilisikia msemo kuwa the moment you discover the "cool", is the same moment the "cool" thing loses it's "cool". Nikaambiwa haya hutokea zaidi katika biashara. Kwamba unapodhani umegundua kile ambacho hakijagunduliwa, kisichopatikana na kilicho "cha pekee", ni wakati huohuo ambao unafungua milango kwa "waigilizaji" walio wengi kukimbilia hapo na matokeo yake ule mfumo wa "supply vs demand" unafanya kazi yake.
Labda suala hapa ni lile lile kuwa HAKUNA NAMNA YA KUDHIHIRISHA KUWA UNAWEZA KUTUNZA SIRI, KWANI NI LAZIMA UISEME ILI MTU AJUE NI IPI ILIYOKUWA SIRI NA UKISHAISEMA UMESHAPOTEZA KILICHOKUFANYA UJIVUNIE...U-SIRI.
Bahati mbaya ni kwamba mifano hii ya kibiashara inaonekana kuwafikia hata "wafanyabiashara wa siasa" nchini Tanzania.
Yaani punde baada ya waTanzania kuamini kuwa WAMEWEKA UPINZANI HALISI BUNGENI, wale "wengine" wenye kuendekeza maslahi zaidi ya wananchi wamerejea kwenye upande ambao unawafanya wananchi wazidi kukubaliana na tafsiri ya Da Subi ya siasa kuwa "siasa si-hasa, bali visa na mikasa".
Tulianza kuyaona mapeeema baada ya uchaguzi pale tulipokubaliana kuwa yawezekana "Ni kweli Dk Shein kashinda..lakiniii..... labda Maalim Seif hajashindwa pia" (irejee hapa) na kikubwa tulichowaza hapo ni kama "kukubali" huku kuliendana na mahitaji ya wananchi ama mahitaji binafsi ya Maalim Seif ambayo hayakutimizwa katika chaguzi tatu zilizopita. Kisha likaja suala la kutangazwa uongozi wa upinzani Bungeni (hapa) ambapo tuliambiwa bayana kuwa "Vyama vingine vya upinzani vyenye wawakilishi Bungeni, TLP, CUF na NCCR-Mageuzi vimekataa kujunda ushirikiano na CHADEMA na badala yake, vinatarajiwa kutangaza safu yao baada ya makubaliano."
Hatujatulia, tukasikia kuhusu wapinzani kutaka kupelekana mahakamani kwa sababu za kampeni ya Kawe na sasa twaona vita ya "demokrasia" inaendelea.
SUALA HAPA SI NANI ANAFANYA NINI, BALI NI NANI NA NANI WANAPINGANA NA KUPIGANIA NINI?
Ni maadui wangapi ambao upinzani wanao na ni wangapi ambao wanaweza kuwa na namna mija ya kuwaondoa? Kama ni MARADHI, UJINGA, MALAZI NA MAISHA DUNI YA WANANCHI, ni kwanini WAKINZANI hawa hawaungani kuwateketeza?
Kama wote ni waenguka wa chama tawala na wanataka kufanya kile kinachozembewa kufanywa na chama tawala, ni kwanini wanashindwa kutafuta palipo na msimamo wa pamoja, wakaungana na kisha wakaweza kumng'oa huyo wapangaye kumng'oa?
Sasa yaonekana "vita dhidi ya matatizo ya wananchi" (ambayo ilistahili kuanza) ndio imekwisha (mpaka mwezi Juni 2015) na sasa ni "vita" ya kusaka umaarufu kwa migongo ya wenzao.
Hivi ni kweli "umoja" unatakiwa kuwepo wakati kila mmoja anasaka UTAWALA?

Sasa na huu ni ujumbe "Kwenu wapinzani. Ms'ojua ushindani na kukalia ukinzani ufanyao 'washindwani'", watu wanataka mabadiliko. Mkanganyiko wa nani anafanya nini kwa manufaa ya fulani na si wachagua si mwema. Hauzifai jamii zilizowaweka madarakani huko bungeni, wala hauifai nchi yetu kwa ujumla. Ni lazima mkumbuke kuwa nyote mwafanya harakati za kusaka maendeleo, lakini cha kusikitisha ni kuwa MWASAKA MAENDELEO KWA KUDIDIMIA UENDELEZI. Yaleyale NILIYOANDIKA HAPA
Kama ulikosa kilichoimbwa, sikiliza na kufuatilia mashairi yake chini.

"Listen people to a story that was written long ago,
Bout a kingdom on a mountain and the valley folks below
On the mountain sit a treasure, buried deep beneath the stone
And the valley people thought they'd have it for their very own.

Chorus
Go ahead and hate your neighbor, go ahead and cheat a friend
Do it in the name of heaven, you'll be justified it in the end
There won't be any trumpets blowing On the judgment day
On the bloody morning after one tin soldier rides away.

So the people of the valley sent a message up the hill
Asking for the buried treasure, tons of gold for which they'd kill
Came an answer from the mountain, "with our brothers we will share
All the secrets of our mountain, all the riches buried there."

Now the mountain cried with anger, "Mount your horses, draw your swords"
And they killed the valley people, so they won their just rewards
Now they stood beside the treasure, on the mountain, dark and red
Turned the stone and looked beneath it, "Peace on earth" that all it said.

Chorus
Go ahead and hate your neighbor, go ahead and cheat a friend
Do it in the name of heaven, you'll be justified it in the end
There won't be any trumpets blowing, On the judgment day
On the bloody morning after, one tin soldier rides away.".... x2

Kama huoni player BOFYA HAPA

2 comments:

emu-three said...

Siasa bwana, mmmh, sijui!

kamala Lutatinisibwa Lutabasibwa said...

hawa jamaa wakina NCCR, KAFWE na TOLOPI siwaelewi, bora KYANDEMA watakiweza