
Zamani migongano ya kifamilia ilikuwa ya kifamilia na ilisuluhishwa na wanafamilia zaidi. Heshima baina ya wanafamilia ilionekana kuwa kubwa kuliko sasa, na hata masuluhisho miongoni mwa wanafamilia nayo ilikuwa ya ndani. Sasa hivi mambo yamebadilika na sina hakika kama ni maendeleo ama la, lakini bado naamini MAMBO YA NDANI YANASTAHILI KUBAKI NDANI (japo yategemea ndani kukoje).
Ndoa zilikuwa zikisemekana kujadiliwa na kutatuliwa ndani ya nyumba / familia tofauti na sasa ambapo yaonekana "pesa" na mawakili wamechukua nafasi kubwa ya UAMINIFU WETU. Lakini tunaendelea kukumbushana kuwa japo twaishi tuishivyo, zipo zama ambazo maisha yalikuwa na MIPAKA. Na ndio maana leo tumeamua kujiburudisha, kujielimisha na kujikomboa kwa kibao hiki.
Leo katika kipengele hiki tunao DDC Mlimani Park wana Sikinde Ngoma ya Ukae ambao chini yake Cosmas Thobias Chidumule wanaeleza walivyosuluhisha "mgogoro" uliopo kati ya kaka ya Chudumule na Mke wa Kakaye huyo.Burudika ukijifunza.
** Zilipendwa ni kipengele kinachokujia kila Jumatatu kukuletea muziki wa kale kuhusisha na maisha, muziki ama sanaa ya sasa katika nyanja mbalimbali. Unaweza kusikiliza nyimbo nyingine ndani ya kipengele hiki kwa kubofya hapa, ama mtandao shirika hapa**
No comments:
Post a Comment