Friday, September 14, 2012

Siku ya mTanzania Washington DC Sept, 15, 2012

Kwanza sikiliza UKARIBISHO WA Mhe. Balozi Mwanaidi Maajar.

Mahali: Tanzania House, 1232 22Nd Street, N.W. Washington D.C.; 20037
Tarehe: SEPTEMBA 15, 2012
Kiingilio: BURE
Muda: (Saa 4:00 asubuhi – Saa 12 Jioni)

Ubalozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Marekani, Washington D.C. unawakaribisha Watanzania wote waishio maeneo ya DMV (District of Columbia, Maryland na Virginia) na vitongoji vyake, kuhudhuria siku ya Mtanzania, ambapo waTanzania watashiriki kuonyesha bidhaa, tamaduni, mila na desturi za Kitanzania kwa wageni (waMarekani na wa mataifa mengine) watakaotembelea ubalozini.

Madhumuni makuu ya Ubalozi kuandaa Siku ya Mtanzania
Kwanza ni kuwaelimisha wenyeji wa Marekani kuhusu Tanzania.
Pili kuitangaza zaidi Tanzania kwa kuvutia watalii wengi kutembelea Tanzania.
Tatu ni kutambulisha na kutangaza biashara mbalimbali na huduma zitolewazo na waTanzania waishio hapa Marekani.
Ubalozi unaomba Watanzania wenye bidhaa mbambali za Kitanzania, mapishi (wenye leseni), vikundi vya ngoma, muziki, mitindo, na waTanzania wenye kampuni za utalii, kujiandikisha ubalozini kuanzia tarehe 1 hadi 15 Agosti, 2012 kwa maandalizi ya siku hiyo.
Kwa Watanzania watakaopenda kujitolea kushiriki siku hiyo au kuonyesha bidhaa mbalimbali wajiandikishe kwa wafuatao:



Ubalozi unapenda kuwahamasisha Watanzania kuvaa vazi la Kitanzania.

                                   Karibuni Wote

IFUATAYO NI RATIBA YA MATUKIO YA LEO

1 comment:

Shadrack Msuya said...

nimependa sana mnavyowasiliana mkiwa huko ughaibuni....watanzania tumeumbwa na upendo....wenye tija...pamoja na nguzo isiyoteguka.shadrack john msuya from mwanza tanzania