Wednesday, January 9, 2013

Ana kwa Ana na Mhe Balozi Mwanaidi Maajar (AUDIO)

Karibu katika mahojiano kati ya JAMII PRODUCTION na Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa nchi za Marekani na Mexico (anayemaliza muda wake) Mhe. Mwanaidi Maajar
Katika mahojiano haya, Mhe Maajar anaeleza
  • Historia yake
  • Ilikuwaje akaingia katika fani ya sheria? Na ni nini alipanga kufanya kabla ya kujikita kwenye sheria?
  • Ni vipi alipokea ombi la kuwa Balozi?
  • Ni zipi changamoto alizokutana nazo kwenye kazi ya ubalozi?
  • Ni vipi amebadili mawazo ya waMarekani wanaoiona Tanzania kama nchi isiyopiga hatua?
  • Anawashirikisha vipi viongozi wa Tanzania maendeleo anayoyaona Marekani?
  • Ipi nafasi ya mwanamke katika uongozi?
  • Anazungumzia vipi suala la viti maalum kwa wanawake?
  • Je! Tanzania ipo tayari kuwa na Rais mwanamke? Na Je! Tanzania ina wanawake ambao wanaweza kuwa rais wa nchi hiyo?
  • Anazionaje jumuiya za waTanzania hapa Marekani?
  • Moja ya mambo mengi yaliyojitokeza Uingereza na Marekani wakati wa ubalozi wake ni kufunguliwa kwa matawi mengi ya kisiasa. Je! Nini wajibu wa balozi kwayo na ni upi wajibu na umuhimu wa matawi ya vyama vya siasa nchi za nje?
  • Ni kipi kipimo cha mafanikio ya balozi? Na anaamini amefanikiwa kwa kiwango gani? Ni kwanini amekaa muda mfupi hapa Marekani ukilinganisha na UK? Ni maamuzi yake ama uamuzi wa Rais?
  • Nini FANIKIO na ANGUKO kuu katika muda wake wa ubalozi?

Na mengine mengi.
KARIBU UUNGANE NASI

SHUKRANI ZA PEKEE KWA UBALOZI WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA KWA NCHI ZA MAREKANI NA MEXICO.

NB: Video ya mahojiano haya zitawajia punde

2 comments:

Israel Saria said...

Safi sana, bro...nahitaji kujifunza kitu toka kwako, hope milango iko wazi...

Unknown said...

BRO U'R NICE. U REALY SPEAK THE TRUTH.