Thursday, August 22, 2013

''Bongo Views'' ya GENN Redio toka kwa waTanzania wanaoishi Kansas City

Global Entertainment and News Network (GENN) iliyopo Kansas City nchini Marekani, inatambulisha kwenu kipindi  kipya cha BONGO VIEWS kitakachokuwa kikiwajia moja kwa moja kila Jumamosi  kuanzia saa 11 jioni kwa saa za Marekani ya kati (12 jioni kwa Marekani ya Mashariki)
Photo
Muendesha wa kipindi cha Bongo Views Joshua Kijo Simon Madelkeka akiendelea kujadili pamoja na washiriki wake kuhusu suala la uraia wa nchi mblili na mambo mengine ndani ya Studio ya Global Entertainment and News Network (GENN)
Photo: BONGO VIEWS: ANDY MKINGA and BAVON
Wachangiaji kipindi  kushoto Mjombo Andrew Mkinga,  akiwa na Anko Bavon Mwakasungula, wakijadili Mjadala kuhusu uraia wa nchi mblili na mambo mengi kuhusu mstakabaliwa nchi yetu, wakiwa ndani ya Studia ya Global Entertainment and News Network (GENN)

Kipindi cha Bongo Views  kitawajia tena LIVE wiki hii, siku ya Jumamosi Aug 24, 2013  kuanzia Saa 11 jioni kwa Saa za Marekani ya kati.  (Saa kumi na mbili jioni kwa Saa za EST US.)
Kwa wale mtakaopenda kushiriki,  msikose kutembelea. HAPA Global Entertainment and News Network (GENN).

Mjadala utakua kuhusu tatizo la madawa ya kulevya nchini.
Ili kuchangia kwa njia ya simu, piga simu namba  (913) 662-1190

No comments: