Wednesday, August 28, 2013

Maadhimisho ya miaka 50 ya March in Washington

Rais Barak Obama, leo ametoa changamoto kwa kizazi kilichopo kuwaenzi mashujaa walioandamana mwaka 1963 kudai haki sawa kwa watu wa rangi zote nchini Marekani.
Mubelwa Bandio ana ripoti kamili
TUKIONI, mwanaJAMII EBOU SHATRY wa Swahilivilla Blog alihudhuria na kunasa nyota kadhaa waliohudhuria wakiwasili

Tuliobahatika kuwanasa katika kamera ya swahilivilla muigizaji Jimmy Foxx, pale alipotolewa ndani ya gari na maofisa kuanza kupekua gari alilolipanda kabla ya kuingia ndani ya eneo la Lincoln Memorial  Washington DC.

Mwigizaji wa filamu Angelha Bassett Evelyn alipotolewa kwenye gari lake na maofisa kuanza kulipekua kabla ya kuingia ndani ya eneo la Lincoln Memorial  Washington DC

Mshangao mkubwa watu walioupata ni pale mtoto wa Rais wa zamani nchini Marekani John F. Kennedy, Caroline Kennedy alipoingia na Cab (Taxi).
Cha kuchangaza pia ni pale gari lake lilipopekuliwa bila ya kujali ukubwa au cheo alichonacho na kufata sheria ya upekuzi kama wengine magari yao yalivyopekuliwa.
Caroline ni Balozi mteule wa Marekani nchini Japan

Ni Oprah Gail Winfrey pekee ambaye hajatoka kwenye gari lake ambalo lilipekuliwa na kuruhusiwa kuondoka bila ya kutolewa ndani ya gari hilo alilokua amalipanda

Mwenyewe mwenyeweeee
Chief wa swahilivilla Abou Shatry akiwa katika 50th anniversary March on Washington DC Siku ya Jumatano 28, 2013
Kwa taswira zaidi BOFYA HAPA

No comments: