Wednesday, August 7, 2013

Shusho, Kilahiro kuhudumu Washington DC wikiendi hii

Watumishi wa Mungu Christina Shusho na Upendo Kilahiro, mwishoni mwa wiki hii watahudumu katika jiji la Washington DC na Vitongoji vyake (DMV).
Shusho na Kilahiro ambao ni miongoni mwa waimbaji mahiri wa muziki wa Injili Afrika Mashariki, wameshawasili Washington DC tayari kwa huduma hiyo ambayo ni sehemu siku tatu za  Maadhimisho ya miaka mitano ya kanisa la The Way Of The Cross Gospel Ministries.
Maadhimisho haya yataanza siku ya Ijumaa na kumalizika Jumapili
Maadhimisho haya yatafanyika
The Way of the Cross Gospel Ministries
(at University United Methodist Church)
3621 Campus Drive
College Park, MD 20740

Hii inakuwa ni mara ya pili kwa watumishi hawa kuhudumu pamoja kanisani hapo katika kipindi cha miaka miwili, ambapo mwaka 2011waliungana na Upendo Nkone kuhudumu katika Mkutano mkubwa wa Injili ulilofanyika kanisani hapo.
 Watazame na kuwasikiliza wanavyoelezea siku hizo
 
            USIKOSE!!!!!
Na hizi ni baadhi ya nyimbo zao mpya
NI KWA NEEMA wake Christina Shusho (hit as always)

Na huu...NKIZA
Moja ya nyimbo mpya za Upendo Kilahiro kutoka katika albamu yake mpya aliyoimba kwa lugha ya kiRundi ya SINZOGIT'ICO NTIYA
IMAGINE
Hawa wote katika JUKWAA MOJA wikiendi hii

No comments: