Sunday, December 15, 2013

[AUDIO] DAKIKA 90 ZA DUNIA: Papa Francis atwaa tuzo ya PERSON OF THE YEAR 2013

Jumatano wiki hii, jarida maarufu na kongwe duniani la TIME, lilimtangaza kiongozi wa kanisa Katoliki duniani Papa Francis, kuwa mtu aliyekuwa na ushawishi mkubwa kwa mwaka huu wa 2013.
Tuzo hiyo, ijulikanayo kama PERSON OF THE YEAR, hutolewa kwa mtu ambaye ametawala vyombo vya habari kwa mwaka husika, iwe ni kwa mambo mema ama mabaya.
Mwaka jana, Rais Barak Obama alishinda tuzo hiyo kwa kutetea kiti chake cha urais nchini Marekani.
Na katika fainali ya tuzo za mwaka huu, walikuwemo pia Rais wa Syria Bashar al Assad ambaye amekuwa akituhumiwa kutumia gesi ya sumu kuua raia wake, pia mwanasayansi aliyevujisha siri za serikali ya Marekani Edward Snownden, Rais Obama na wengine sita.
Hii ilikuwa ripoti ya Disemba 14, 2013


Bahati Alex (L) Capital Radio Jijini Dar es Salaam na Mubelwa Bandio (R) wa Jamii Production Washington DC

No comments: