Sunday, December 22, 2013

VizionOne Inc yafanya sherehe kuwapongeza wafanyakazi wake

Mkurugezi mtendaji wa Vizion One Inc Bw,Abdallah Kitwara Amewapongeza Wafanyakazi na Wahisani wa kampuni hiyo kwa jitihada yao ya kufanya kazi kwa bidii ili kutoa huduma bora kwa Wagonjwa na wateja wao.
C.E.O Vizion One Home Health Services Bwana. Abdallah Kitwara  akizungumza na wafanyakazi wa kampuni yake na wageni mbali mbali waliohudhuria, pembeni yake ni Mkewe Bi.Vanessa Kitwara.
Pongezi hizo alitoa wakati wa hafla maalum ya mwisho wa mwaka iliyoandaliwa na kampuni hiyo Siku ya Ijumaa Dec 20, katika Ukumbi wa Lanham hapa Washington D.C
Amesema kampuni yake ya Vizion One Home Health Services hivi sasa Mbali ya kutoa huduma yake Mjini Washington D.C,  Pia imesambaza huduma zake katika majimbo mengine hapa marekani ikiwemo Pennsylvania, Massachusetts, Kentucky na Kansas Missouri.
Aidha  amewashukuru , wafanyakazi na washirika mbali mbali waliojitolea kutoa msukumo mkubwa wa kupelekea kampuni yake ya Vizion One Inc kutoa huduma bora zaid.
Sherehe hizo zinazofanyika kila mwisho wa mwaka kampuni ya Vizion One Inc iliweza kuwatunuku cheki wafanyakazi wake kama tunzo la ufanyakazi bora na kuongeza bidi za kazi kwa mwaka unaofuata lakini pia katika hotuba yake meneja wa kampuni hiyo Abdallah Kitwara aliweza kizunguimzia historia yake kwa kifupi baada ya pongezi na shukurani kwa wafanyakazi wake.

Kwa taswira zaidi click read more.

No comments: