Wednesday, February 7, 2018

Kipindi cha JUKWAA LANGU Feb 5 2018 Pt 1 SARATANI

Katika sehemu ya kwanza ya kipindi cha Jukwaa Langu, tumezungumzia kuhusu siku ya SARATANI DUNIANI iliyoadhimishwa  Feb 4.
· Takwimu za maradhi haya zinaonyesha kwamba kifo 1 kati ya 6 hutokana na maradhi haya.
· Wajua, namna yanavyoathiri nchi zinazoendelea? Ni 20% tu zenye takwimu sahihi kuwezesha kupambana na maradhi haya.
Unajua ni tabia gani maishani zinaweza kuondoa 30% ya Saratani?
· Unafahamu harakati zinazofanywa na Diaspora katika kupambana na maradhi haya?
· Tulikuwa na Mwanasayansi na Mtafiti wa aina mojawapo ya Saratani, pamoja na mwanaharakati kujadili haya.
......
JUKWAA LANGU ni kipindi kinachoijadili TANZANIA YA SASA NA ILE TUITAKAYO. *Tanzania katika jicho la DIASPORA.*
Ungana na Mubelwa Bandio, Dj Luke Joe na waalikwa wengine studioni kujadili mambo mbalimbali kuhusu siasa, afya, uchumi, utamaduni nk.
Usikose.
Ni Jumatatu na kila Jumatatu kuanzia saa 12 kamili jioni mpaka 2 kamili usiku kwa saa za Marekani Mashariki (6:00 - 8:00pm ET)
Ni kupitia Kwanza Radio kwenye TuneIn
http://tun.in/sfwyf

No comments: