
Pengine si kazi rahisi kuwashukuru wote na kama nilivyosema awali kuwa kubwa tuwezalo kufanya ni kuwaombea, lakini pale tuwezapo, twahitaji japo kuwatembelea na kuwajulia hali katika KUONESHA KUTHAMINI MCHANGO WAO KWETU.
Msingi mzima wa kuwathamini waliotuwezesha kwa namna ya kuwajulisha kuwa twathamini mchango wao kwetu ni jambo muhimu kulifanya. Si wakati wote ambao twajua liendelealo "nyuma ya pazia" ambako wale washirikio kwenye ukuaji wetu hukumbana na makwazo na mambo mengi kupima kile wafanyacho.
Pale tuwezapo na tuwashukuru lakini kwa tusioweza kuwaona na kuwaonesha thamani ya mchango wao kwetu, basi TUWAOMBEE.
Na jumatatu ya leo tuungane na mkongwe Muhidin Maalim "Gurumo" akiwa na Orchestra Safari Sound Band ambao wanatukumbusha funzo la kuthamini waliokwenda hatua kadhaa kutufanikishia maisha yetu.
Sikiliza wimbo wao SHUKRANI KWA MJOMBA
** Zilipendwa ni kipengele kinachokujia kila Jumatatu kukuletea muziki wa kale kuhusisha na maisha, muziki ama sanaa ya sasa katika nyanja mbalimbali. Unaweza kusikiliza nyimbo nyingine ndani ya kipengele hiki kwa kubofya hapa, ama mitandao shirika hapa** . Ama ili kuweza kujua tasnia nzima ya muziki na wanamuziki wa Tanzania BOFYA HAPA
2 comments:
Swadakta kaka hii imetulia...
za kale ni safi sana Ahsante kwa kipengele hiki!!
Post a Comment